- Mwanzo
- Kuhusu Sisi
- Utawala
- Wilaya
- Halmashauri
- Fursa za Uwekezaji
- Huduma
- Machapisho
- Kituo cha Habari
Thursday 25th, April 2024
@Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera
Uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kuwa tumeandaa kliniki tembezi ya Madaktari Bingwa wa fani mbalimbali itakayofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa (Government) kuanzia tarehe 05 – 11 Novemba, 2018.
Mgonjwa kumuona Daktari Bingwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera itakuwa ni shilingi 10,000/= (Elfu kumi tu) kwa magonjwa yote isipokuwa magonjwa ya moyo itakuwa ni shilingi 15,000/= (Elfu kumi na tano tu). Gharama hizi ni nafuu sana ukilinganisha na gaharama ya shilingi 25,000/= hadi 40,000/= kumuona Daktari Bingwa akiwa katika kituo chake cha kazi kwa magonjwa yote na magonjwa ya moyo shilingi 40,000/= hadi shilingi 50,000/=.
Aidha, gharama za upasuaji nazo zitakuwa nafuu sana, upasuaji katika magonjwa yote gaharama yake itakuwa katai ya shilingi 60,000/= hadi 100,000/= tu ambapo itakuwa nafuu sana ukilinganisha na gharama za upasuaji Madaktari Bingwa wakiwa katika vituo vyao vya kazi ambapo huanzia shilingi 300,000/= hadi shilingi 1,500,000/=.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera
Anwani: S.L.P 299 BUKOBA
Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17
Simu ya Mkononi:
Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz
Haki zote zimehifadhiwa