• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Agriculture Services

HALI YA HEWA 

Hali ya hewa ya Mkoa wa Kagera kwa ujumla ni ya joto la wastani wa 26.02 sentigredi. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 600 – 2,000 kwa mwaka kati ya mwezi Septemba na Januari na kati ya mwezi Machi na Mei. Mvua hizi ndizo zinazowezesha kuwepo kwa uoto wa asili wa kuvutia katika maeneo mengi ya Mkoa. Kwa miaka ya kawaida Mkoa hupata mvua za uhakika za vuli na masika ambazo ni muhimu kwa shughuli za kilimo na ufugajiA

Kanda za Ikolojia (Ecological Zones)

Mkoa wa Kagera umegawanyika katika kanda tano (5) za kilimo kuzingatia mwinuko wa maeneo hayo kutoka usawa wa bahari na kiwango cha unyeshaji wa mvua.


(a)   Ukanda wa Kwanza

Ukanda huu unajumuisha maeneo ya Mashariki ya Wilaya za Bukoba na Muleba yanayo ambaa kando kando ya Ziwa Victoria na uko katika mwinuko wa mita 1,300 mpaka 1,500 kutoka usawa wa bahari. Mvua katika ukanda huu zinanyesha kwa wastani wa milimita 800 - 1,750 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi katika eneo hili ni kilimo cha ndizi, maharagwe, mahindi, kahawa, uvuvi na ufugaji. Eneo la ukanda huu ni asilimia 17 ya eneo la mkoa.

 

(b)   Ukanda wa Pili

Huu ni ukanda wa juu ulioko kwenye mwinuko wa mita 1,400 mpaka 1,800 kutoka usawa wa bahari. Ukanda huu unajumuisha maeneo ya juu ya Wilaya ya Karagwe, Kyerwa na Ngara na mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800 - 1,000 kwa mwaka. Mazao yanayolimwa kwenye ukanda huu ni migomba, maharagwe, mahindi, kahawa n.k. Eneo la ukanda huu ni asilimia 19 ya eneo la Mkoa.

 

(c)   Ukanda wa Tatu

Ukanda huu uko katika mwinuko wa mita 1,000 kutoka usawa wa bahari na unajumuisha Wilaya ya Biharamulo. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 750 - 800 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi ni uzalishaji wa mazao ya mahindi, mihogo, mpunga, mtama, karanga, tumbaku na pamba. Eneo la ukanda huu ni asilimia 27 ya eneo la Mkoa.

 

(d)   Ukanda wa Nne 

Ukanda huu upo kwenye mwinuko wa mita 1,000 kutoka usawa wa bahari na unajumuisha maeneo ya Mashariki ya Wilaya ya Karagwe, Wilaya ya Missenyi na maeneo ya Magharibi ya Wilaya ya Bukoba. Mvua za ukanda huu zinanyesha kwa wastani wa milimita 800 - 1,000 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi ni kilimo cha mazao ya mahindi, maharagwe, miwa na ufugaji. Eneo la ukanda huu ni asilimia 10 ya eneo lote la Mkoa.

 

(e)   Ukanda wa Tano 

Ukanda huu unajumuisha maeneo ya Kaskazini ya Wilaya ya Karagwe na Missenyi na uko kwenye mwinuko wa mita 1,000 kutoka usawa wa bahari ukanda huu unapata mvua za wastani wa milimita 750 - 800 kwa mwaka. Sehemu kubwa ya ukanda huu ni misitu ya hifadhi na mapori ya akiba. Eneo la ukanda huu ni asilimia 27 ya eneo lote la Mkoa.

Utoshelevu wa Chakula

Mahitaji ya chakula kwa mkoa wa Kagera ni tani 842,936 (wanga tani 771,239 protein tani 71,697) kwa mwaka. Kwa miaka minne mfululizo uzalishaji wa mazao ya chakula ulikuwa kati ya tani 3,000,000 hadi tani 3,359,276. Hivyo kumekuwa na utoshelevu wa zaidi ya 255% - 300% ambapo ziada inauzwa nje ya mkoa na nje ya nchi. 

Maendeleo ya Zao la Kahawa

Uzalishaji katika zao la kahawa kwa miaka minne ni tani 387,464.64 kuanzia msimu wa mwaka 2020/21 hadi msimu wa mwaka 2023/2024 aidha bei imeongezeka kutoka wastani wa Tsh. 1100  hadi kufikia Tsh. 6153 eongezeko la bei 82%.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa