• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Kilimo cha Umwagiliaji


UTANGULIZI

Mabadiliko ya Tabianchi.

Dunia imekuwa na mabadiliko makubwa ya tabianchi yanayosababisha uhaba wa mvua na hatimaye kuleta upungufu mkubwa wa uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara.

Hali ya mabadiliko ya tabianchi imefanya majira ya mvua katika Mkoa wa Kagera kubadilika ambapo msimu wa mvua za vuli unaanza kunyesha mwezi Novemba badala ya mwezi Septemba wakati msimu mvua za masika unaanza kunyesha mwezi Aprili badala ya mwezi Februari hadi Juni.

Sera na Maelekezo ya Serikali.

Hali hii imefanya Serikali kuanzisha Sera ya umwagiliaji ya mwaka 2010 kwa lengo la kuinua Kilimo cha umwagiliaji.

Pamoja na sera ya Umwagiliaji yapo maelekezo mengine yanayosisitiza Kilimo kama vile:

Mpango wa Serikali wa Maendeleo wa Miaka Mitano kuanzia 2015 hadi 2020.

Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2015 ambayo imesisitiza kilimo cha umwagiliaji kupitia Ibara Na. 21(m) na 22(c) i-vii.

Uongozi imara wa Sekretariet ya Mkoa wa Kagera unaongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera (Mh. Mej. Jen.Mstaafu Salum M. Kijuu) pamoja na Katibu Tawala Mkoa (CP. Diwani Athuman) unaosimamia utekelezaji wa Sera,Miongozo na Maelekezo yote ya Serikali Kuu kuhusu sekta ya kilimo cha umwagiliaji.

Aina mbalimbali za Kilimo cha Umwagiliaji.

Umwagiliaji unaweza kufanywa kwa kutumia njia mbalimbali ambazo ni pamoja na:

1. Njia ya mafuriko(Surface Irrigation).

2. Njia ya mabomba(Sub surface Irrigation).

3. Njia ya Mtawanyo (Sprinkler Irrigation).

4. Njia ya matone(Drip Irrigation).

Ambapo kwa Mkoa wa Kagera umwagiliaji wa njia za mafuriko,mabomba na matone ufanywa na wakulima wadogowadogo katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri za Wilaya ila umwagiliaji wa njia ya sprinkler unafanyika hasa katika mashamba makubwa ya Kiwanda cha Sukari Kagera(Kagera Sugar) kwani njia hiyo umwagiliaji ni nzuri hasa kwa mashamba makubwa kwa kuwa unamwagilia eneo kubwa kwa muda mfupi ingawaje inagharimu fedha nyingi katika kuendesha jenereta na mitambo mengine saidizi ya mfumo huo.

MIKAKATI INAYOTUMIKA.

Mkoa kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya pamoja na wadau wengine wa maendeleo umejiwekea mikakati mbalimbali ya utekelezaji wa kilimo cha umwagiliaji.

Mikakati hiyo ni pamoja na:

Kuhamasisha umma na sekta binafsi katika Kilimo cha umwagiliaji.

Kuhakikisha kwamba mifumo ya umwagiliaji (Inayoanzishwa na itakayoanzishwa) inazingatia sheria na taratibu za nchi.

Kuhamasisha matumizi bora ya rasilimali maji katika mifumo ya Kilimo cha umwagiliaji.

Kuhakikisha kwamba Maendeleo ya Kilimo cha umwagiliaji yanazingatia masuala ya kiufundi, kiuchumi, kijamii na kimazingira.

Kuhakikisha kwamba rasilimali maji ya umwagiliaji yanatumika kikamilifu kwa kiwango cha juu kwa kuzingatia tija.

Kuhakikisha kwamba miundo ya maendeleo ya kilimo cha umwagiliaji(Irrigation development models) inatumika kuzalisha mazao yenye tija kulingana na mahitaji ya soko.

Kuhuisha masuala mtambuka kama vile jinsia, ukimwi, mazingira, afya, ardhi na maji katika maendeleo ya Kilimo cha umwagiliaji.

Kuendelea kutekeleza Kilimo cha umwagiliaji kupitia programu ya maendeleo ya Sekta ya Kilimo (ASDP) kwa kuongeza eneo lenye miundo mbinu ya umwagiliaji kutoka hekta 19,831 za Desemba 2016 hadi hekta 50,000 ifikapo mwaka 2020. Sekta binafsi itashirikishwa katika uendelezaji na uwekezaji kwenye kilimo cha umwagiliaji.

Kuzihimiza Halmashauri kukamilisha kutunga sheria ndogo za umwagiliaji.

Kujenga na kukarabati miundombinu ya umwagiliaji ya wakulima wadogo na wakati ili kuongeza uzalishaji na ufanisi wa matumizi ya maji.

Kujenga na kukarabati mabwawa ya kuvuna na kuhifadhi maji ya mvua na mito kwa ajili ya umwagiliaji kwa kila Halmashauri ya wilaya.

Kujenga uwezo wa Taasisi zinazohusika na umwagiliaji katika ngazi ya Halmashauri za wilaya na wakulima katika usimamizi na uendeshaji endelevu wa miradi ya umwagiliaji.

 

Wilaya
Eneo linalofaa kwa umwagiliaji(Ha)
Eneo linalotumika kwa umwagiliaji(Ha)
Asilimia ya matumizi(%)

Bukoba
10,300
497
4.8

Muleba
5,895
400
6.78

Missenyi
20,463
15,564
76.05

Ngara
5,000
3,200
64

Biharamulo
1300
50
3.8

Karagwe
3750
177.7
4.7

Kyerwa
250
50
20

JUMLA
43,918
19,831
45.15

 

 












MAENEO YANAYOFAA KWA KILIMO CHA UMWAGILIAJI 

Hapo juu ni takwimu za maeneo yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji pamoja maeneo yanayolimwa kwa sasa Mkoani Kagera hadi kufikia Desemba, 2016.

NB: Serikali Mkoani kagera inaendelea kufanya mwasiliano na Wizara ya Maji na Umwagiliaji kupitia Ofisi ya Tume ya Umwagiliaji Kanda-Mwanza ili ifanyike National Irrigation Master Plan kwa ajili ya kubaini maeneo zaidi yanayofaa kwa Kilimo cha Umwagiliaji.

Pia Serikali ya Mkoa wa Kagera kwa kushirikiana na OR-TAMISEMI,Kituo cha Uwekezaji Tanzania pamoja na Wizara ya Maji na Umwagiliaji inaendelea na utaratibu wa kutangaza maeneo ya uwekezaji hasa yale yanayofaa kwa Kilimo cha umwagiliaji yakiwemo mabonde ya:Kyabalamba(500ha)-Bukoba,Katoro(515.2ha)-Bukoba,Kiijongo(961.2ha)-Bukoba,Kazinga(18ha)-Bukoba,Buterankuzi(221.6ha)-Bukoba,Kaibanja(654.4ha)-Bukoba,Ngarama(506.4ha)-Bukoba,Burigi(400ha)-Muleba, Nkenge(1300ha)-Missenyi,Bulembo(662.4ha)-Missenyi,Kabajuga(783.6ha)-Missenyi,Butulage(402.4ha)-Missenyi,Byeju(500ha)-Missenyi, Kajunguti(1000ha)-Missenyi, Buchurago(2000ha)-Missenyi, Kabingo(500ha)-Missenyi,Ngono(1300ha),Mpanyula(110ha)-Ngara, Rwinyana(40ha)-Ngara, Mubuhenge(86ha)-Ngara, Mugozi(120ha)-Ngara, Magamba(88ha)-Ngara,Mwiruzi(1000ha)-Ngara,Ngundusi(110ha)-Ngara,Muhongo(170ha)-Ngara,Ruvubu(300ha)-Ngara,Kagera(580ha)-Ngara,Mukafigiri(60ha)-Ngara,Murutabo(100ha)-Ngara,Nyarulama(110ha)-Ngara,Nzaza(150ha)-Ngara Bujuruga(300ha)-Karagwe, Nyakakika(100ha)-Karagwe na Kibogoyizi(375ha)-Karagwe, Mato(600ha)- Karagwe, Mkakajinja(500ha)-Karagwe, Nyakahita(450ha)-Karagwe, Bwelanyange(45ha)-Karagwe,Bukangara(570ha)-Karagwe na Mushabaiguru(210ha)-Karagwe.

MIRADI YA UMWAGILIAJI INAYOTEKELEZWA.

Serikali kupitia Mpango wa Kuendeleza Sekta ya Kilimo nchini(ASDP) kwa kushirikisha wadau wa maendeleo kama vile Benki ya Maendeleo ya Afrika(AfDB), World Vision Tanzania pamoja na Shirika la Maendeleo la Watu wa Japan (JICA) imeweza kutekeleza uanzishwaji wa Miradi ya Umwagiliaji katika maeneo mbalimbali ikiwa inamilikiwa na Serikali pamoja na wananchi wa maeneo husika kama ifuatavyo;-

Missenyi-Kyakakera (163ha/watu156), Karagwe-Mwisa (300ha/Watu 180), Ngara-Bigombo (110ha/Watu160), Biharamulo-Mwiluzi (120ha/Watu 200), Muleba-Kyamyorwa (500ha/Watu 300), Buyaga (80ha/Watu 150), Buhangaza (95ha/Watu 130) na Kyota (120ha/Watu 190)

NB: Mazao makubwa yanayolimwa katika maeneo ya miradi hiyo ni Mahindi, Mpunga,Mazao ya mizizi(Mihogo,Viazi vitamu,Viazi vikuu & Viazi Mviringo), Mazao ya mafuta(Alizeti & Ufuta) pamoja na Mbogamboga(Mchicha,Matango,Chainizi,Spinachi,Maboga,Vitunguu,Nyanya,pilipili,matikiti maji).

 

 CHANGAMOTO

Zipo changamoto kadhaa zinazojitokeza katika utekelezaji wa mikakati ya kilimo cha umwagiliaji Mkoani kagera ikiwemo na:-

Bajeti ndogo ya uwekezaji katika kilimo cha umwagiliaji.

Uwezo na ushiriki mdogo wa taasisi binafsi katika maendeleo ya kilimo cha umwagiliaji.

Ujuzi mdogo kwa wakulima kuhusu kilimo cha umwagiliaji.

Uwezo mdogo wa Halmashauri za wilaya katika uwekezaji na utekelezaji wa Kilimo cha umwagiliaji.

Utumiaji mdogo wa maji (insufficient water use) unaosababisha ukosefu wa tija katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji.

Ukosefu wa mifumo bora ya kuendeleza kilimo cha umwagiliaji.

Ukosefu wa vihifadhi bora vya maji (Water storage facilities) kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya kilimo cha umwagiliaji.

Kukauka kwa vyanzo vya maji kunakosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

Upungufu wa wataalamu wa umwagiliaji katika Halmashauri za wilaya.

MIKAKATI YA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO.

Katika kukabiliana na changamoto zilizopo, Serikali Mkoani Kagera imepanga kufanya yafuatayo ili kuendeleza kilimo cha umwagiliaji katika msimu wa mwaka 2016/17:-

Kuzishauri Halmashauri za Wilaya kutenga bajeti ya kutosha katika sekta ya umwagiliaji ili zisaidie katika zoezi la Tathimini na Ufuatiliaji wa shughuli za Umwagiliaji.

Kuhamasisha taasisi binafsi ili ziweze kushiriki vema katika kuendeleza sekta ya kilimo cha umwagiliaji.

Mfano: Kagera Tea Co. Ltd, KSL,MAYAWA,Igabiro Agric Institute n.k

Kuwawezesha wakulima mbinu mpya na bora zitakazosaidia kuendeleza kilimo cha umwagiliaji kupitia Wataalamu wa Ugani waliopo katika kila Kata na Vijiji.

Kuhamasisha matumizi bora na endelevu ya rasilimali maji kwaajili ya kufanikisha kilimo cha umwagiliaji kupitia Wataalamu wa Sekta ya Umwagiliaji waliopo katika Halmashauri za Wilaya pamoja na Tume ya Umwagiliaji ya Taifa.

Kuandaa mifumo bora, endelevu na yenye tija kwa ajili ya kuendeleza kilimo cha umwagiliaji.

Kuzihimiza Halmashauri kuandaa mipango bora na matumizi bora ya ardhi kwa sekta ya umwagiliaji.

Kusimamia ujenzi wa vihifadhi bora vya maji (Water storage facilities) vitakavyosaidia kuendeleza kilimo cha umwagiliaji.

Kuhamasisha na kuendeleza juhudi za utunzaji wa mazingira hasa maeneo yazungukayo miradi ya umwagiliaji ili kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi (Climatical Change) kwa ushirikiano wa Baraza la Utunzaji wa Mazingira Tanzania.

Kuzishauri Halmashauri za wilaya ili zitenge bajeti za kuajiri wataalamu wa umwagiliaji kulingana na tange pamoja na ikama ya Halmashauri.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa