• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Utawala na Rasilimali Watu

LENGO LA SEHEMU YA UTAWALA NA RASILIMALI WATU

Kutoa usaidizi wa utaalam na huduma za utawala na Menejimenti ya Utumishi kwenye Sekretarieti ya Mkoa

Sehemu hii inafanya kazi zifuatazo:-

  • Kuratibu utekelezaji wa Sera ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma pamoja na    sheria zinazotawala uendeshaji wa Utumishi wa Umma.
  • Kushirikiana na OR-MUU-Sekretarieti ya Ajira katika masuala yote yahusuyo ajira za watumishi.
  • Kutoa huduma za masjala na Utunzaji wa Kumbukumbu.
  • Kutoa huduma za Ki-protokali.
  • Kuratibu huduma za ulinzi, usafi, matengenezo, nyumba na usafiri.
  • Kusimamia masuala yote ya ajira na utumishi wa watumishi (kuthibitisha, kupandisha vyeo, kuendeleza watumishi, mpango wa raslimali watu, upimaji wa Wazi (OPRAS), mishahara na stahiki zinginezo, likizo, hitimisho la ajira, nidhamu malalamiko nk.) katika Sekretarieti ya Mkoa
  • Kumshauri Katibu Tawala Mkoa kuhusu masuala ya Utawala, Utumishi na raslimali watu.
  • Kusimamia masuala ya nidhamu kwa watumishi.

UTANGULIZI

Wakati tunapata UHURU, mkoa wa Kagera ulikuwa na jumla ya wilaya nne (4), wilaya hizo ni Ngara ambayo ilianzishwa mwaka 1947, Biharamulo, Bukoba, na Karagwe mwaka 1958 ambayo ilizinduliwa rasmi na gavana wa kiingereza Sir Richard Turnbul. Aidha, mwaka 1975 wilaya mpya ya Muleba ilianzishwa kutoka kwenye wilaya ya Bukoba na mwaka 2007 wilaya ya Chato na Missenyi zilianzishwa na kuunda jumla ya wilaya 7 za mkoa wa Kagera.

Mwaka 2011, Wilaya ya Chato ilihamishiwa mkoa mpya wa Geita. Aidha, mwaka huo huo wa 2011 mkoa wa Kagera ulipata wilaya mpya ya Kyerwa ambayo ilipatikana baada ya kuigawa Wilaya ya Karagwe. Kwa sasa mkoa wa Kagera una jumla ya wilaya saba (7) na halmashauri 8. Wilaya hizo ni Bukoba, Muleba, Biharamulo, Ngara, Kyerwa, Karagwe, Missenyi na Ngara. Halmashauri ni Bukoba Manispaa, halmashauri ya wilaya ya Bukoba, Muleba, Biharamulo, Ngara, Kyerwa, Karagwe na Missenyi.

Kisiasa mkoa una jumla ya majimbo 10 ya uchaguzi (Muleba 2, Karagwe 1, Ngara 1, Biharamulo 1, Missenyi 1, Bukoba Manispaa 1, Bukoba Vijijini 1 na Kyerwa jimbo 1).

IDADI YA WATU

Kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 1967 mkoa ulikuwa na watu 658,712, mwaka 1978 watu 1,009,379, mwaka 1988 mkoa ulikuwa na watu 1,326,183 na mwaka 2002 watu 2,033,888. Ongezeko la idadi ya watu lilikuwa kwa wastani wa asilimia 2.7. Aidha, mwaka 2012 kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 mkoa ulikuwa na jumla ya watu 2,458,023.

MAJIMBO YA UCHAGUZI

Mkoa unayo majimbo ya Uchaguzi 10 na wapo Wabunge 9 wa kuchaguliwa na Wabunge 3 wa viti maalum. Jumla ya Wabunge 11 wanatoka chama cha Mapinduzi (CCM) na Mbunge 1 anatoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo.

HALI YA UCHUMI NA MAENDELEO YA MKOA

Uchumi wa mkoa unategemea zaidi kilimo ambapo zaidi ya asilimia 70 ya watu wanajishughulisha na kilimo cha mazao ya chakula na biashara. Shughuli za uvuvi, mifugo,viwanda na madini zinachangia pia katika uchumi wa mkoa.

Kwa kuzingatia malengo ya Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza Umaskini (MKUKUTA) , Dira ya Taifa ya mwaka 2025 na malengo ya Milenia, Mkoa wa Kagera unaendelea kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo na umepiga hatua katika sekta za uchumi, miundo mbinu na huduma za jamii. Hata hivyo pamoja na hatua hizi zilizopigwa, juhudi za wananchi mkoani za kujiletea maendeleo zinakumbana na matatizo na vikwazo mbalimbali ambavyo vimeendelea kupatiwa ufumbuzi kwenye mipango ya maendeleo ya Mkoa.

KANDA ZA IKOLOJIA (ECOLOGICAL ZONES) :

Mkoa wa Kagera umetenganishwa katika Kanda tano za kilimo kuzingatia mwinuko wa maeneo hayo kutoka usawa wa bahari na kiwango cha unyeshaji wa mvua.

•Ukanda wa kwanza : Ukanda huu unajumuisha maeneo ya mashariki ya wilaya ya Bukoba na Muleba yanayoambaa kandokando ya ziwa victoria na uko katika mwinuko wa mita 1,300 mpaka 1,500 kutoka usawa wa bahari. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800 - 1,750 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi katika eneo hili ni kilimo cha ndizi, maharagwe, mahindi na kahawa. Eneo la ukanda huu ni asilimia 17 ya eneo la Mkoa.

Ukanda wa pili : Huu ni ukanda wa juu ulioko kwenye mwinuko wa mita 1,400 mpaka 1,800 kutoka usawa wa bahari. Ukanda huu unajumuisha maeneo ya juu ya wilaya ya Karagwe na Ngara na mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800-1,000 kwa mwaka. Mazao yanayolimwa kwenye ukanda huu ni ndizi, maharagwe, mahindi na kahawa. Eneo la ukanda huu ni asilimia 19 ya eneo la mkoa.

Ukanda wa Tatu : Ukanda huu uko katika mwinuko wa mita 1,000 kutoka usawa wa bahari na unajumuisha wilaya ya Ngara ,Biharamulo. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 750-800 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi ni uzalishaji wa mazao ya mahindi, mihogo, mpunga, mtama, karanga na pamba. Eneo la ukanda huu ni asilimia 27 ya eneo la mkoa.

Ukanda wa Nne : Ukanda huu upo kwenye mwinuko wa mita 1,000 kutoa usawa wa bahari na unajumuisha maeneo ya mashariki ya wilaya ya Karagwe,wilaya ya Misenyi na maeneo ya magharibi ya wilaya ya Bukoba. Mvua zinanyesha kwa wastani wa milimita 800-1,000 kwa mwaka. Shughuli kuu za kiuchumi ni kilimo cha mazao ya mahindi,maharagwe na ufugaji. Eneo la ukanda huu ni asilimia 10 ya eneo la mkoa.

Ukanda wa Tano :Ukanda huu unajumuisha maeneo ya kaskazini ya wilaya ya Karagwe na Misenyi na uko kwenye mwinuko wa mita 1,000 kutoka usawa wa bahari .Ukanda huu unapata mvua za wastani wa milimita 750-800 kwa mwaka.Sehemu kubwa ya ukanda huu ni misitu ya hifadhi na mapori ya akiba. Eneo la ukanda huu ni asilimia 27 ya eneo la mkoa.



Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa