• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Uvuvi

1.0 UTANGULIZI

Mkoa wa Kagera unapatikana Kaskazini Magharibi mwa nchi ya Tanzania ambapo unapakana na nchi ya Uganda kwa upande wa Kaskazini, Rwanda na Burundi kwa upande wa Magharibi mkoa wa Kigoma na Mwanza kwa upande wa Kusini na Ziwa Victoria kwa upande wa Mashariki. Mkoa huu una jumla ya Halmashauri za Wilaya 8 ambazo ni Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba, Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba, Muleba, Kyerwa, Biharamulo, Ngara, Missenyi na Karagwe.

Sekta ya Uvuvi ni moja ya Sekta muhimu katika kuwapatia Wananchi wengi wa Mkoa wa Kagera ajira, kipato, lishe bora na hivyo kuchangia katika kumuondolea mwananchi umaskini. Shughuli za Uvuvi katika Mkoa hufanyika katika Ziwa Victoria, mto Kagera, Ngono, Ruvuvu na Mabwawa. Maeneo mengine ya Uvuvi ni katika Maziwa madogo madogo ya Burigi, Rwakajunju, Kamakala, Ikimba, Rushwa, Melula, Katwe, Luko, Karenge, Mitoma, Kaburi, Kitete, Kabindi, Ngoma na Rumanyika. Samaki wanaovuliwa katika Ziwa Victoria ni Sangara (Nile perch), Dagaa, Sato jamii ya Nile tilapia (O. niloticus, variabilis, Oesculentus na leucostictus), Kambale (Clarius gariepinus) na furu (Haplochromis).

Mkoa katika kuendeleza Sekta ya Uvuvi unasimamia utekelezaji wa Sera, Sheria na mikakati mbalimbali ya Sekta ya Uvuvi ikiwa ni pamoja na kudhibiti Uvuvi haramu na uharibifu wa mazingira, kuendeleza ufugaji bora wa samaki, kudhibiti utoroshaji wa mazao ya samaki kwenda nchi jirani, kutoa elimu juu ya madhara ya Uvuvi haramu na VVU/UKIMWI, kusimamia masoko na mialo ya samaki, kuhakiki viwango vya ubora na usalama wa mazao ya Uvuvi na kusajili mitumbwi ili kudhibiti mapato na uhalifu n.k.

Taarifa hii inaelezea muendelezo wa utekelezaji wa shughuli za Uvuvi, ambapo kwa kipindi cha Mwaka wa fedha 2017/2018 kuanzia Mwezi Julai 2017 hadi Agosti, 2018, Sekta ya Uvuvi Mkoa wa Kagera imechukua na inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za kisheria katika kulinda raslimali za Uvuvi kwa ajili ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho.


 2.0 Dira, Dhamira na Malengo ya Mkoa Kuendeleza Sekta ya Uvuvi

2.1 Dira ya Sekta ya Uvuvi Mkoa wa Kagera

Mkoa wa Kagera kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ya Sekta ya Uvuvi umedhamiria kulinda raslimali za Uvuvi kwa kufanya Uvuvi endelevu unaozingatia Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya Mwaka 2003.


2.2 Dhamira ya Sekta ya Uvuvi Mkoa wa Kagera

Dhamira ya Mkoa ni kuwajibika ipasavyo katika kulinda raslimali ya Uvuvi ikiwa ni pamoja na kutoa huduma bora kwa jamii.

2.3 Lengo Kuu la Kuendeleza Sekta ya Uvuvi

Kukuza uhifadhi, maendeleo na usimamizi endelevu wa raslimali za Uvuvi kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo.

2.4 Malengo ya Kawaida

Katika kufanikisha utekelezaji wa dira na mwelekeo wa Mkoa kuendeleza Sekta ya Uvuvi, malengo 15 yamependekezwa kama ifuatavyo:-

  • Kulinda raslimali za Uvuvi kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho.
  • Kudhibiti matumizi ya zana haramu za Uvuvi.
  • Kudhibiti biashara haramu ya mazao ya Uvuvi.
  • Kudhibiti utoroshaji wa mazao ya Uvuvi kwenda nchi jirani bila kufuata taratibu.
  • Kuendeleza Ufugaji bora wa Samaki.
  • Kuongeza uzalishaji wa samaki kwenye mabwawa.
  • Kuboresha miundombinu katika Sekta ya Uvuvi.
  • Kulinda ubora na usalama wa Mazao ya Uvuvi. 
  • Kuboresha huduma na uwajibikaji katika ulinzi wa raslimali za Uvuvi.
  • Kuongeza ushirikishaji wa jamii katika ulinzi wa raslimali ya Uvuvi.
  • Kuwawezesha wavuvi na jamii za wavuvi.
  • Kuvutia wawekezaji wa ndani na wa nje katika Sekta ya Uvuvi.
  • Kuongeza ukusanyaji wa mapato ya Sekta ya Uvuvi.
  • Kufanya tafiti mbalimbali katika Sekta ya Uvuvi.
  • Kudhibiti vitendo vyote vya wizi wa nyavu, injini na ujambazi ziwani.


3.0 Hali ya Sekta ya Uvuvi Mkoa wa Kagera

Tangu enzi za Uhuru, shughuli za Uvuvi zimekuwa miongoni mwa vyanzo muhimu vya mapato na lishe kwa wakazi wengi wa Mkoa wa Kagera. Shughuli za Uvuvi hufanyika kwa kiasi kikubwa katika Ziwa Victoria, mito na maziwa madogo madogo 15 (Satellite lakes). Shughuli hizi zinalenga kwa kiasi kikubwa kwenye Uvuvi wa Sangala wanaovuliwa kwa wingi na wenye Soko kubwa ndani na nje ya nchi. Samaki huyu ameleta faida kubwa kwa upande wa “pato la taifa” na wananchi ambapo amewafanya kuwa matajiri. Samaki wengine (Endermic Species) wanaovuliwa katika Ziwa Victoria kama vile Sato, Nembe, Gogogo, Ningu, Soga, Dagaa, Furu, Kamongo, Ngege, Mumi, Mbofu, Kuyu nk. Samaki hawa walivuliwa kwa kutumia nyavu za inchi 2½ hadi inchi 3.

Kutokana na Sensa ya Uvuvi ya mwaka 2014idadi ya wavuvi katika Mkoa wa Kagera imeongezeka kutoka wavuvi 9,616mwaka 2000 hadi wavuvi 23,740mwaka 2018. Sambamba na hilo idadi ya mitumbwi nayo imeongezeka kutoka mitumbwi 3,395mwaka 2000hadi mitumbwi 7,338 mwaka 2018.Pia idadi ya nyavu za sangala imeongezeka kutoka nyavu 51,068 mwaka 2000 hadi nyavu 98,389 mwaka 2018.

Jedwali lifuatalo linaonyesha idadi ya Wavuvi, Mitumbwi na Nyavu kimkoa

MWAKA
IDADI YA WAVUVI
IDADI YA MITUMBWI
IDADI YA NYAVU (SANGALA)
IDADI YA NYAVU DAGAA
IDADI YA MIGONZO
2000
9.616
3,395
57,068
453
295,780
2002
13,056
4,486
109,413
686
429,662
2004
12,608
4,127
102,349
586
355,239
2006
15,727
5,517
93,896
1,992
652,545
2008
19,882
7,027
314,073
726
1,041,035
2010
17,771
5,651
63,009
907
953,500
2012
19,449
6,116
81,413
1,430
1,196,717
2014
21,721
6,539
92,563
1,711
1,361,830
2016
24,122
7,321
100,288
1,836
1,492,174
2018
23,740
7,338
98,389
1,027
1,638,955

Kutokana na kuongezeka kwa nguvu ya Uvuvi (fishing effort) idadi ya samaki ziwani imekuwa ikipungua kila mara. Kwa mujibu wa sensa ya Uvuvi ya Mwaka 2014 na 2015, sangala walipungua kutoka tani 651,353 mwaka 2014 hadi tani 621,254 mwaka 2015. Wakati huo dagaa waliongezeka kwa asilimia 9% kutoka tani 698,736 Mwaka 2014 hadi tani 859,931 Mwaka 2015. Kiasi hiki cha dagaa kimekuwa kikiongezeka tangu mwaka 2007. Asilimia kubwa ya samaki hawa wanaishi mwambao wa pwani ya Ziwa.


Jedwali lifuatalo linaonyesha idadi ya dagaa na sangala waliomo ziwani.


Septemba 2011
Septemba 2014
Novemba 2015
Stratum
Eneo (km2)
Dagaa (t/km2)
Sangala (t/km2)
Dagaa (t/km2)
Sangala (t/km2)
Dagaa (t/km2)
Sangala (t/km2)
Deep
6,166

63,510

136,269

78,925

53,583

198,947

54,137

Coastal
5,786

135,971

114,563

133,657

182,085

197,207

172,113

Inshore
2,003

51,677

53,480

45,268

49,053

61,013

43,398

SG
2,909

48,289

45,090

49,744

39,388

92,617

40,747

Deep
6,251

56,884

51,258

180,654

80,013

163,253

126,056

Coastal
6,601

53,468

40,266

151,823

179,217

78,943

128,011

Inshore
3,181

33,401

27,675

50,578

61,139

57,882

52,319

EP
2,022

14,558

3,033

8,088

6,875

10,071

4,472

JUMLA

476,068

471,634

698,736

651,353

859,931

621,254

Chanzo: Tanzania Fisheries Frame survey 2014 na 2015


4.0 Fursa Zilizopo Mkoa Wa Kagera Katika Sekta Ya Uvuvi

Mkoa wa Kagera una eneo la maji lenye ukubwa wa kilomita za mraba 10,655 sawa na asilimia 27, jiografia nzuri, maeneo chepechepe yenye udongo unaotunza maji na vyanzo vingi vya maji (water bodies) kama vile mto Kagera, Mto ngono, mto Ruvuvu, mto Kanoni, Ziwa Victoria na maziwa mengine madogo madogo 15. Mkoa huu wa Kagera unasifika na kuwa Mkoa wa kwanza nchini Tanzania na wa pekee wenye maziwa madogo madogo (Satellite Lake) mengi yanayofikia 15 kama yafuatayo.

Ziwa Burigi Ziwa Burigi linapakana na Wilaya tatu ambazo ni Muleba, Karagwe na Biharamulo Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina samaki wengi aina ya Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haprochromis), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Rwakajunju Ziwa Rwakajunju linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina ukubwa wa km2 27.72. Baadhi ya samaki waliomo ni pamoja na Furu (Haprochromis), Sato (Oreochromis esculentus na Variabilis), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Kamakala Ziwa kamakala linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili linasifika kwa kuwa na samaki wengi aina Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haprochromis), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Ikimba Ziwa Ikimba linalinapatikana Wilaya ya Bukoba Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina ukubwa wa km2 38.09. Baadhi ya samaki waliomo ni pamoja na Furu (Haplochromines), Sato (Oreochromis esculentus), Kamongo (Protopterus catastoma) na Kambale (Clarius gariepinus). Ziwa hili linapatikana Bukoba Vijijini Mkoa wa Kagera. Baadhi ya changamoto zilizopo Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Rushwa Ziwa Rushwa linapatikana Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina ukubwa wa km2 10.08. Baadhi ya samaki waliomo ni pamoja na Sato (Oreochromis esculentus, leocosticus, niloticus, variabilis na Tilapia zilii), Kamongo (Protopterus aethhiopicus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Melula Ziwa Melule liko Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina ukubwa wa km2 15.21. Samaki waliomo ni pamoja na Sato (Oreochromis esculentus na niloticus), Furu (Haplochromines) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Katwe  Ziwa katwe linapatikana Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina ukubwa wa km2 2.23. Ziwa hili lina aina 6 za samaki ambao ni pamoja na Sato (Oreochromis leocostictus), Furu (Haprochromines), Kamongo (Protopterus aethiopicus), Kambale (Clarius gariepinus), (Momyrus) na Gogogo (S.afrofischeri). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Luko Ziwa Luko linapatikana Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Ziwa hili lina samaki wengi aina nyingi ya Sato (Oreochromis esculentus), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Kalenge Ziwa Karenge linapatikana Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Ziwa lina aina 9 za samaki ambao ni Sato (O.leocostictus, niloticus na variabilis), Furu (Haplochromines), B.profundus na B.sadleri, Kambale (Clarius gariepinus na C.alluaudi) na Gogogo (S.afrofischeri). Ziwa hili linakumbwa na changamoto ya Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumu na magugu maji.

 Ziwa Mitoma Ziwa Mitoma linapatikana Wilaya ya Kyerwa Mkoa wa Kagera. Kuna aina 5 za samaki ambao ni (B.sadleri), Kambale (Clarius gariepinus), Furu (Haplochromines), Kamongo (Protopterus aethiopicus) na Gogogo (Synodontis afrofischeri).

Ziwa Kaburi Ziwa Kaburi linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili linasifika kuwa na samaki wengi aina Sato (Oreochromis esculentus), Kamongo (Protopterus aethiopicus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zilinazopo ni Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na kilimo na magugu maji.

Ziwa Kitete, Ziwa Kitete linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili linasifika kwa kuwa na samaki wengi aina Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haplochromines), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Ziwa hili Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Kabindi Ziwa Kabindi linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili linasifika kwa kuwa na samaki wengi aina Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haplochromines), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Ziwa hili Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Ngoma Ziwa Ngoma linapatikana Wilaya ya Karagwe Mkoa wa Kagera. Ziwa hili linasifika kwa kuwa na samaki wengi aina Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haplochromines), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus). Baadhi ya changamoto zinazolikumba Ziwa hili ni pamoja na Uvuvi usioendelevu, uharibifu wa mazingira kutokana na shughuli za kiuchumi na magugu maji.

Ziwa Rumanyika Ziwa Rumanyika linapatikana katika hifadhi ya rumanyika Wilaya ya Kyerwa. Ziwa hili linasifika kwa kuwa na samaki aina Sato (Oreochromis esculentus), Furu (Haplochromines), Kamongo (Protopterus) na Kambale (Clarius gariepinus).


5.0 SERA, SHERIA, KANUNI NA MIKAKATI YA SEKTA YA UVUVI

5.1 SERA YA UVUVI YA MWAKA 1997 ILIYOBORESHWA MWAKA 2015

Sera ya Taifa ya Uvuvi ni chombo cha usimamizi ambacho kina himiza uvunaji, matumizi na biashara endelevu ya raslimali za uvuvi kwa ajili ya kuwapatia wananchi chakula, kipato, ajira na fedha za kigeni na ulinzi thabiti wa viumbe hai wa majini na mazingira kwa ajili ya maendeleo endelevu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo pamoja na kuhakikisha kuwa kunakuwepo na mafanikio/ufanisi. Lengo kuu la Sera ya Taifa ya Uvuvi ni kukuza uhifadhi, maendeleo na usimamizi endelevu wa raslimali za uvuvi kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo. Pia Sera hii ina malengo ya kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Kupunguza umaskini nchini (MKUKUTA II).

5.2 SHERIA YA UVUVI NAMBA 22 YA MWAKA 2003

Sheria ya Uvuvi ni chombo kinachotumika katika kusimamia utekelezaji wa Sera ya Uvuvi. Dhumuni la Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya mwaka 2003 ni kuleta maendeleo endelevu, kulinda, kuhifadhi, kuendeleza ufugaji wa viumbe hai kwenye maji, kudhibiti ubora wa samaki na mazao yake, mimea ya majini na mazao yake na masuala mengine yanayofanana na hayo kwa manufaa ya kizazi cha sasa na vizazi vijavyo. Sheria ya Uvuvi Sehemu ya Tano (V) inasisitiza usimamizi na Udhibiti wa Shughuli za Uvuvi. Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya Mwaka 2003 inalenga Uvuvi endelevu unaozingatia taratibu pamoja na kuvua samaki kwa kutumia zana halali zinazoruhusiwa kisheria. Baadhi ya zana haramu za Uvuvi zisizoruhusiwi kisheria ni:-

  1. Nyavu za makila (gill nets) zenye macho kuanzia inchi 5 na kuendelea katika ziwa Victoria kwa Uvuvi wa sato, na nyavu za nchi 6 na kuendelea kwa Uvuvi wa sangara zinaruhusiwa kisheria,
  2. Nyavu aina ya kokoro haziruhusiwi kisheria kutumika katika shughuli za Uvuvi ziwani,
  3. Nyavu aina ya timba (monofilaments) haziruhusiwi kisheria kutumika katika shughuli za Uvuvi ziwani.
  4. Nyavu za kuvulia dagaa zenye macho madogo chini ya milimita 8, haziruhusiwi kutumika kisheria katika shughuli ya Uvuvi wa dagaa,
  5. Mtumbwi ambao hauna usajili hauruhusiwi kisheria kujihusisha na shughuli za Uvuvi,
  6. Mvuvi asiye na leseni haruhusiwi kujihusisha na shughuli za Uvuvi,
  7. Samaki aina ya sato mwenye urefu chini ya sentimita  25 haruhusiwi kuvuliwa kisheria,
  8. Samaki aina ya sangara mwenye urefu chini ya sentimita 50 na mwenye urefu zaidi ya sentimita 85 haruhusiwi kuvuliwa kisheria,
  9. Kutokuwa na nyaraka halali za kusafirisha mazao ya samaki, hairuhusiwi kisheria.


6.0 UTEKELEZAJI WA SERA NA SHERIA YA UVUVI

Mkoa wa Kagera umeendelea kusimamia na kutekeleza Sera ya Taifa ya Uvuvi ya Mwaka 1997, Mikakati na Sheria ya Uvuvi na. 22 ya Mwaka 2003.

6.1 Uchangiaji wa Sekta ya Uvuvi KatikaAjira na Uchumi. 

Sekta ya Uvuvi ni moja ya Sekta muhimu kwa maendeleo ya wananchi wa Mkoa wa Kagera kiuchumi na kijamii.

6.1.1 Uchangiaji wa Sekta ya Uvuvi katika Ajira

Sekta ya Uvuvi inachangia kwa kiasi kikubwa katika kutoa ajira ambapo jumla ya wananchi26,830 wameajiriwa au kujiajiri kutokana na Shughuli za Uvuvi Mkoani Kagera. Kati ya hao waliajiriwa kwenye Viwanda vya samaki ni 462, ajira kwa wavuvi ni 23,740, wafugaji samaki ni 665 na wauzaji wa samaki ni 1,787. Kutokana na ajira hizi wananchi wameweza kujipatia kipato, fedha za kujikimu na kuboresha makazi na kuchangia maendeleo.

Jedwali Na. 3: Uchangiaji wa Sekta ya Uvuvi katika Ajira

Na
Wilaya
Ajira Kwa Viwanda
Ajira kwa Wavuvi
Ajira Kwa Wafugaji samaki
Ajira Kwa Wauzaji wa samaki
Jumla
1
Bukoba (M)

350

928

29

123

1,430

2
Bukoba (W)

112

3,475

61

241

3,889

3
Muleba

0

18,491

98

602

19,191

4
Karagwe

0

340

165

120

625

5
Missenyi

0

82

103

308

755

6
Kyerwa

0

424

40

305

769

7
Ngara

0

0

120

12

122

8
Biharamulo

0

0

49

76

49

 
Jumla

462

23,740

665

1,787

26,830


6.1.2 Uchangiaji wa Sekta ya Uvuvi katika Uchumi

Sekta ya Uvuvi inachangia kwa kiasi kikubwa katika kuinua hali ya uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na Serikali kutokana na kodi mbalimbali. Kwa kipindi cha Mwaka wa fedha 2017/2018 kuanzia Mwezi Julai 2017 hadi Juni 30, 2018 jumla ya tani 4,651.8 za samaki zilivuliwa katika Ziwa Victoria ambazo zilikuwa na thamani ya Tshs Bilioni 27.75, maziwa madogo madogo (Satellite Lakes) na kwenye mabwawa ya kufugia Samaki yaliyopo Mkoani Kagera. Samaki hao wanatumika kama kitoweo na hivyo kusaidia kuboresha afya na wengine kuuzwa kwa ajili ya kujipatia kipato. Baadhi ya Samaki wameuzwa humu ndani ya Mkoa wetu wa Kagera na zingine kusafirishwa kwenda nchi za nje hivyo kusaidia kuliingizia Taifa fedha za kigeni.

Jedwali Na. 04: Uchangiaji wa Sekta ya Uvuvi katika Uchumi

Na

Halmashauri ya Wilaya

Samaki Waliovunwa Ziwa Victoria na Maziwa Madogo madogo

Samaki waliovunwa kwenye mabwawa ya Samaki

Uzito (Kg)

Thamani (Tshs)

Uzito (Kg)

Thamani (Tshs)

1

Bukoba MC

593,490

3,264,195,000

0

0

2

Bukoba DC

967,246

6,314,147,600

383

3,255,500

3

Muleba DC

2,908,856.8

17,470,742,400

420

2,100,000

4

Karagwe DC

82,689

330,756,000

170

850,000

5

Missenyi DC

47,609

285,654,000

25

75,000

6

Kyerwa DC

51,998

83,196,800

520

2,600,000

7

Ngara DC

0

0

200

1,000,000

8

Biharamulo

0

0

0

0

 

JUMLA

4,651,888.8

27,748,691,800

1,718

9,880,500












N.B: Chanzo cha taarifa ni wavuvi, wafanya biashara na wafugaji wa samaki

6.2 Kuendeleza Uzalishaji na Ufugaji wa Samaki Kwenye Mabwawa

Katika kuendeleza ufugaji bora wa samaki Mkoani Kagera, wananchi wamehamasishwa kuchimba mabwawa hususani ufugaji wa samaki kibiashara, kutoa miongozo ya mabwawa ya mfano, kuzalisha, kusambaza vifaranga na kutoa mafunzo kwa wafugaji wa samaki.Kutokana na hamasa, elimu pamoja na juhudi za wafugaji samaki, jumla ya mabwawa 619 yamechimbwa mkoani Kagera kwa Mwaka 2017/2018 kutoka mabwawa 202 Mwaka 2008/2009 sawa na ongezeko la mabwawa 407.

Pia Vikundi 21 vimehamasishwa ufugaji bora wa samaki aina ya Sato na Kambale ambapo baadhi yao ni Kikundi cha Bugabo fish Pond, Ujamaa group, Chavuma sauti ya watu, Umoja ni nguvu, Fish pond development group (FPDG), Tujunangane Group na Jiunge, Wazee group n.k.

Jedwali Na. 5: Takwimu za Mabwawa ya Ufugaji wa Samaki Mkoani Kagera

WILAYA
Idadi ya Mabwawa Mkoa wa Kagera Kuanzia Mwaka 2008 – 2018

2008/2009

2010/2011

2011/2012

2012/2013

2013/2014

2014/2015

2015/2016

2016/2017

2017/2018
Bukoba (M)

33

33

35

61

71

72

80

77

39

Missenyi

13

13

24

41

45

61

64

61

61

Muleba

41

41

48

87

121

121

144

180

221

Bukoba (W)

32

32

36

50

56

44

71

48

51

Kyerwa

0

0

0

39

42

42

50

52

53

Karagwe

49

49

57

55

58

67

71

73

73

Ngara

25

25

30

35

39

43

55

55

79

Biharamulo

0

0

7

19

21

21

32

38

42

Chato

9

4

6

-

-

-

-

-

-

Jumla

202

197

238

387

453

471

567

584

619

 

6.3 Usajili wa Vyombo Vya Uvuvi

Vyombo vinavyotumika kwa shughuli za Uvuvi katika Ziwa Victoria na maziwa madogo madogo (Satellite lakes) yaliyopo Mkoa wa Kagera ni mitumbwi ya injini na mitumbwi midogo ya kasia.Kwa kipindi cha Mwaka wa Fedha 2017/2018 kuanzia Mwezi Julai 2017 hadi Juni 30, 2018 jumla ya mitumbwi ya kuvua samaki ni 7,338ambapokati ya hiyo, mitumbwi 3,415 ya kasia na mitumbwi 2,763 ya injini imesajiliwa na kulipia mapato sawa na asilimia 84.2 ya mitumbwi yote ya kuvua samaki.Zoezi la usajili wa mitumbwi linaendelea ili kuhakikisha kwamba mitumbwi yote imesajiliwa, kupewa namba za usajili na kulipia mapato ya Serikali.

Jedwali Na. 6: Takwimu za Mitumbwi ya kuvua Samaki Mkoa wa Kagera

Na

H/WILAYA

Jumla ya Mitumbwi yote ya Kuvua Samaki

Mitumbwi iliyosajiliwa na kulipia Mapato

Mitumbwi  ambayo haijasajiliwa

Mitumbwi ya Kasia

Mitumbwi ya Injini

Mitumbwi ya Kasia

Mitumbwi ya Injini

1

Bukoba (M)

417

79

236

69

33

2

Bukoba (W)

835

304

642

59

67

3

Muleba

5,554

2,725

1,854

696

49

4

Karagwe

196

147

5

44

0

5

Missenyi

62

25

26

11

0

6

Kyerwa

274

135

0

139

0

7
Ngara

0

0

0

0

0

8
Biharamulo

0

0

0

0

0

 
JUMLA

7,338

3,415

2,763

1,018

149

N.B: Wilaya za Biharamulo na Ngara hazipakani na Ziwa hivyo hakuna shughuli za Uvuvi ziwani bali ufugaji wa samaki kwenye mabwawa.

 

6.4 Ukusanyaji wa Mapato ya Uvuvi

Halmashauri zote zenye shughuli za Uvuvi zimedhibiti uingiaji katika shughuli za Uvuvi kwa kuzingatia ukusanyaji wa mapato, usajili na kutoa leseni kwa vyombo vya Uvuvi na wavuvi kama vile mitumbwi, nyavu, wauzaji wa samaki na mazao ya Uvuvi. Kwa Mwaka 2017/2018 jumla ya Tshs bilioni 1.86 zimekusanywa kutokana na shughuli za Uvuvi zaidi ya bilioni 1.34 zilizo kusanywa mwaka jana 2016/2017 sawa na Ongezeko la Tshs milioni 519.

Jedwali Na7: Ukusanyaji wa mapato kuanzia Mwaka 2014 – 2018.

Na

WILAYA

Mapato ya Uvuvi yaliyokusanywa Kuanzia Mwaka 2014 – 2018

2014/2015
2015/2016
2016/2017
2017/2018

1

Bukoba (M)

51,367,000

51,140,745

77,710,022

110,800,864

2

Bukoba (W)

141,293,200

175,909,000

189,591,800

240,075,650

3

Muleba

690,078,200

793,266,270

1,014,915,156

1,462,390,802

4

Karagwe

3,283,000

1,745,000

29,679,600

5,844,600

5

Missenyi

2,716,500

5,536,000

9,917,500

13,506,700

6

Kyerwa

2,885,000

14,889,100

19,443,200

17,969,300

7

Biharamulo

0

0

0

350,000

8

Ngara

0

0

0

9,655,500

JUMLA KUU

891,622,900

1,042,486,115

1,341,257,278

1,860,593,416

N.B: Wilaya za Biharamulo na Ngara hazipakani na Ziwa Victoria hivyo hakuna shughuli za Uvuvi ziwani bali ufugaji wa samaki kwenye mabwawa.


6.5 Udhibiti wa Uvuvi Haramu

Shughuli ya kudhibiti Uvuvi haramu ni mkakati endelevu katika Mkoa wa Kagera kwa ajili ya kulinda raslimali ya mazao ya Uvuvi kutokana na Sera ya Uvuvi ya Mwaka 2015 na Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya Mwaka 2003. Shughuli hii imekuwa ikifanyika kwa kushirikisha taasisi mbalimbali kama vile Uvuvi, Polisi, Mahakama, TAKUKURU pamoja na Idara ya Uhamiaji kwa kufanya doria dhidi ya Uvuvi haramu katika mialo na nchi kavu.Piautekelezaji wa mikakati ya kazi hii ulifanyika kwa kutumia mbinu mbalimbali kama vile kutafuta taarifa za uhalifu, kuweka watoa taarifa za siri (informer) kwa maeneo mbalimbali pamoja taarifa kutoka kwa maafisa Uvuvi Wilaya na wananchi ambao wanachukia suala la Uvuvi haramu.

Katika kudhibiti matumizi ya zana haramu za Uvuvi Mkoani Kagera jumla ya doria 131 zimefanyika kwa kipindi cha kuanzia mwezi Julai 2017 hadi Juni, 2018 na hivyo kuwezesha kukamatwa zana haramu za Uvuvi ambazo ni kokoro za sangala 462, nyavu ndogo za dagaa 221, nyavu za timba 4,189, nyavu za makila ()5,300, katuli 17, Ndoano 820, mitumbwi 235 na samaki wachanga wenye uzito wa Kg 16,615 ambazo kwa ujumla zilikuwa na thamani ya Tshs Bilioni 7,249,054,500 kama inavyoonyeshwa kwenye jedwali namba 4. Pia watuhumiwa 126 walikamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya Sheria ambapo wengine wamehukumiwa na wengine kesi zao bado zinaendelea.


Aidha watendaji wote wa Vijiji na Mitaa wameandikiwa barua zenye maagizo yanayolenga kudhibiti vitendo vyote vya matumizi ya zana haramu za Uvuvi kuanzia ngazi ya Vijiji/Mitaa na kuhakikisha kuwa wavuvi haramu wanasalimsha zana zao haramu za Uvuvi kwa hiari. Zoezi hili linaenda vizuri ambapo hadi kufikia mwezi Juni 30, 2018 wavuvi 62 wamesalimisha zana haramu za Uvuvi walizokuwa wakizitumia kwa shughuli za Uvuvi na wengine waliokaidi walikamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. Pia vikundi vyote vya usimamizi wa raslimali za Uvuvi (BMU) vimeagizwa kutekeleza Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya Mwaka 2003 katika mialo.

N.B: Wilaya za Biharamulo na Ngara hazipakani na Ziwa Victoria hivyo hakuna shughuli za Uvuvi ziwani bali ufugaji wa samaki kwenye mabwawa.


Jedwali Na 5: Ukusanyaji wa mapato kwa kipindi cha Mwezi Juni 2016 – Julai, 2017.

MAKUSANYO YA MAPATO KWA ROBO YA TATU YA MWAKA WA FEDHA 2016/2017 (TSHS)
Na
WILAYA
Malengo kwa mwaka (a)
Ada za Leseni/
Vibali (b)
Tozo za Faini (c)
Maduhuli (d)
Makusanyo Mengine (e)
Jumla (f=b+c+d+e)
%
(f/a)
1
Bukoba (M)

55,472,800

21,068,000

0

13,252,430

43,389,092

77,710,022

140.1

2
Bukoba (W)

273,250,000

33,317,000

2,760,000

151,208,800

0

189,591,800

69.38

3
Muleba

1,024,200,000

499,943,676

1,158,500

0

513,812,980
1,014,915,156

99.09

4
Karagwe

3,480,000

6,320,000

300,000

23,059,600

0

29,679,600

852.8

5
Missenyi

5,616,000

6,219,000

0

0

3,698,500

9,917,500

176.5

6
Kyerwa

2,500,000

16,392,200

3,051,000

0

0

19,443,200

777.1

JUMLA KUU
1,364,518,800

583,259,876

7,269,500

187,520,830

560,900,572

1,341,257,278

98.13

N.B: Wilaya za Biharamulo na Ngara hazipakani na Ziwa Victoria hivyo hakuna shughuli za Uvuvi ziwani bali ufugaji wa samaki kwenye mabwawa.


 6.5 Udhibiti wa Uvuvi Haramu

Shughuli ya kudhibiti Uvuvi haramu ni mkakati endelevu katika Mkoa wa Kagera kwa ajili ya kulinda raslimali ya mazao ya Uvuvi kutokana na Sera ya Uvuvi ya Mwaka 2015 na Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya Mwaka 2003. Shughuli hii imekuwa ikifanyika kwa kushirikisha taasisi mbalimbali kama vile Uvuvi, Polisi, Mahakama, TAKUKURU pamoja na Idara ya Uhamiaji kwa kufanya doria dhidi ya Uvuvi haramu katika mialo na nchi kavu. Pia utekelezaji wa mikakati ya kazi hii ulifanyika kwa kutumia mbinu mbalimbali kama vile kutafuta taarifa za uhalifu, kuweka watoa taarifa za siri (informer) kwa maeneo mbalimbali pamoja taarifa kutoka kwa maafisa Uvuvi Wilaya na wananchi ambao wanachukia suala la Uvuvi haramu.

Katika kudhibiti matumizi ya zana haramu za Uvuvi Mkoani Kagera jumla ya doria 65 zimefanyika kwa kipindi cha kuanzia mwezi Julai 2016 hadi Juni, 2017 na hivyo kuwezesha kukamatwa zana haramu za Uvuvi ambazo ni kokoro za sangala 422, nyavu ndogo za dagaa 57, nyavu za timba 3,231, nyavu za makila 14,141, katuli 16, Ndoano 712 mitumbwi 133 na samaki wachanga wenye uzito wa kg 3,330 ambazo kwa ujumla zilikuwa na thamani ya Tshs Bilioni 1,602,860,500 kama inavyoonyeshwa kwenye jedwali namba 4. Pia watuhumiwa 86 walikamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya Sheria.

Aidha watendaji wote wa Vijiji na Mitaa wameandikiwa barua zenye maagizo yanayolenga kudhibiti vitendo vyote vya matumizi ya zana haramu za Uvuvi kuanzia ngazi ya Vijiji/Mitaa na kuhakikisha kuwa wavuvi haramu wanasalimsha zana zao haramu za Uvuvi kwa hiari. Zoezi hili linaenda vizuri ambapo hadi kufikia mwezi Juni 30, 2017 wavuvi 43 wamesalimisha zana haramu za Uvuvi walizokuwa wakizitumia kwa shughuli za Uvuvi na wengine waliokaidi walikamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria. Pia vikundi vyote vya usimamizi wa raslimali za Uvuvi (BMU) vimeagizwa kutekeleza Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya Mwaka 2003 katika mialo.

Jedwali Na. 8: Takwimu ya Zana Haramu za Uvuvi zilizokamatwa

WILAYA
Idadi ya Doria
 
IDADI YA ZANA HARAMU ZILIZOKAMATWA 
 
Samaki Wachanga (Kg)
Watuhumiwa
Kokoro za sangala
Nyavu ndogo za dagaa
Nyavu za Timba
Nyavu za makila

Kimea (Cast net)
Ndoano
Katuli
Mitumbwi
BUKOBA (M)
4
18
0
243
728
0
0
6
32
607
2
BUKOBA (W)
24
43
29
63
169
0
0
0
8
3,236
3
MULEBA
69
379
188
3,327
3,173
0
0
0
129
10,694
93
MISSENYI
3
18
4
160
190
0
0
0
28
600
4
KYERWA
25
0
0
146
750
0
720
8
30
1,450
15
KARAGWE
6
4
0
250
290
0
100
3
8
28
9
JUMLA
131
462
221
4,189
5,300
0
820
17
235
16,615
126

N.B: Wilaya za Biharamulo na Ngara hazipakani na Ziwa Victoria hivyo hakuna shughuli za Uvuvi ziwani bali ufugaji wa samaki kwenye mabwawa.


6.6 Udhibiti wa Ubora na Usalama wa Mazao ya Uvuvi

6.6.1 Ukaguzi Katika Viwanda, Masoko na Maghala ya Samaki

Mkoa wa kagera una jumla ya viwanda vitatu ambapo viwanda viwili ni vya kusindika minofu ya samaki na kiwanda kimoja cha kuchakata mapanki na kutengeneza soseji za samaki. Viwanda hivi ni kiwanda cha Kagera Fish Company kilichoanza kazi mwezi Oktoba 2003, Kiwanda cha VICFISH Co. Ltd kilichoanza uzalishaji Juni 2005 na kiwanda cha Mapanki Company Limited. Mkoa wa Kagera umeendelea kuhakiki viwango vya ubora na usalama wa mazao ya Uvuvi kwenye viwanda, masoko na maghala ya kuhifadhi mazao ya Uvuvi ambapo jumla ya kaguzi 167 zimefanyika ikiwa ni pamoja na kuangalia ubora na usalama wa samaki kabla ya kusafirishwa kwenye masoko ya ndani na nje ya nchi. Matokeo ya kaguzi hizo yalionesha kukidhi viwango vya ubora wa samaki. 

Jedwali Na. 9: Takwimu zaViwanda vya Kuchakata Samaki

Na
Jina La Kiwanda
Uzalishaji Kwa Siku (Tani)
Uwezo Wa Kiwanda (Tani/Siku)
Aina Ya Samaki
Mahali Kilipo
01.
Kagera Fish Company Ltd
2
20
Sangala
Bukoba (W), Kemondo
02.
Supreme Perch Co. Ltd
15
60
Sangala
Bukoba (M)
03.
Mapanki Company Limited
1
10
Sangala
Bukoba (W)


6.6.2 Usimamizi wa Masoko na Mialo ya Samaki

Mkoa wa Kagera una jumla ya masoko na magulio ya samaki119. Wastani wa bei ya samaki aina ya sangala wabichi kwa kilo ni shilingi 6,200/=, 6,600/= sato wabichi, 3,000/= dagaa wabichi na shilingi 90,000/= kwa mabondo ya sangala. Mkoa wa Kagera umeendelea kuratibu na kusimamia miundombinu ya masoko ya mazao ya Uvuvi kwa kufanya kaguzi kwenye masoko makubwa na madogo ya Samaki yaliyopo Manispaa ya Bukoba, Muleba, Bukoba vijijini, Missenyi, Kyerwa, Ngara, Karagwe na Biharamulo. Pia ukaguzi umefanyika kwenye masoko madogo katika maeneo ya vijijini, mjini na katika mialo ya Ziwa Victoria, maziwa madogo (Satelite lakes) na mito. Mkoa unawawezesha wavuvi na wafanyabiashara halali juu ya soko la samaki kwa kuwepo viwanda vitatu ambavyo ni VIC-Fish, Kagera Fish na Kiwanda cha Mapanki Co. Ltd ambao hununua samaki aina ya sangara kwa uhakika, hivyo kuwawezesha wananchi kupata kipato na kuwainua kiuchumi. 

Jedwali Na. 10: Takwimu za bei ya samaki Mkoa wa Kagera

NA
WILAYA
Idadi Ya 
Masoko/ Magulio
WASTANI WA BEI YA SAMAKI KWA KILO (Tshs/Kg)
Sangala (kg)
Sato (kg)
Dagaa (kg)
Samaki wengine (kg)
Bichi
Kavu
Bichi
Kavu
Bichi
Kavu
Bichi
Kavu
1
Bukoba (M)

4

5,500

4,500

7,500

0

1,500

2,500

5,000

8,000

2
Bukoba (W)

5

6,000

7,500

8,500

9,000

1,500

2,500

4,000

1,500

3
Muleba

56

6,000

5,000

5,000

6,000

3,000

4,000

2,000

3,500

4
Missenyi

7

5,500

5,000

7,000

10,000

4,000

5,000

3,500

4,000

5
Kyerwa

35

0

10,000

5,000

12,000

0

8,000

1,600

7,000

6
Karagwe

12

8,000

10,000

7,000

10,000

5,000

9,000

5,000

8,000

 
WASTANI

119

6,200

7,000

6,600

9,400

3,000

5,100

3,500

5,300


6.7 Utendaji Kazi wa Beach Management Unit (B.M.U)

KatikaMkoa wa Kagera jumla ya BMU’s 93 zimeundwa kwa sheria ya Uvuvi Na. 22 yaMwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009ambapo Manispaa ya Bukobakuna BMU 5, Wilaya ya BukobaVijijini BMU’s 11, Wilaya ya Muleba BMU’s 70Wilaya ya Missenyi BMU’s 2na Karagwe BMU’s 5. Baadhi ya BMU zimetoa mchango mkubwa katika ulinzi wa rasilimali ya Uvuvi katika mialo mbalimbali, ingawa zipo BMU’s chache zinazofanya vibaya kwa sababu kadhaa, kwa kuwepo BMU’s shughuli zifuatazo zimefanyika.

  • Kutekeleza Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya Mwaka 2003 na kanuni zake.
  • Kutoa vibali vya kusafirisha mazao ya samakikutoka eneo moja hadi jingine,
  • Kutoa taarifa za siri juu ya vitendo vya Uvuvi haramu,
  • Utunzaji wa mazingira na usafi wa mialo,
  • Kutoa ushirikianokwa mawakala katika mialo juu ya ukusanyaji wa mapato ya halmashauri,
  • Kutoa elimu ya awali kwa wavuvi juu ya utekelezaji wa Sheria ya Uvuvi Na. 22 ya mwaka 2003 na kanuni ya mwaka 2009.


 7.0 UTEKELEZAJI WA MIRADI MBALIMBALI

Hadi kufikia mwezi Juni 2018, Mkoa wa Kagera umetekeleza miradi mbalimbali kwa lengo la kuendeleza Sekta ya Uvuvi na ufugaji wa samaki ili kuwaletea maendeleo wananchi hasa wavuvi na wafugaji wa samaki. Baadhi ya miradi hiyo imefadhiliwa na Serikali na mingine imetekelezwa kwa ufadhili wa mashirika yasiyo ya kiserikali zikiwemo Ngo’s. Ifuatayo ni baadhi ya miradi iliyotekelezwaMkoani Kagera.

Jedwali Na. 11: Takwimu za miradi mbalimbali Mkoa wa Kagera

Na
WILAYA
AINA YA MRADI
UFADHILI
UTEKELEZAJI

1
Bukoba (M)
Kujenga banda la kupokelea samaki kisiwa cha nyabesiga.
DADP’S
Mradi umekamilika

2
Bukoba (W)
Ujenzi wa Vizimba (Cages) kwa ajili ya ufugaji wa samaki Ziwa Victoria.
UNDP, ESRF na JKT
Mradi umekamilika.

3.
Muleba
Ununuzi wa boti 1 (fibre boat) kwa ajili ya doria ya shughuli za uvuvi.
H/Wilaya
Mradi umekamilika

Ujenzi wa jengo la kupokelea samaki mwalo wa Katembe.
H/Wilaya
Mradi umekamilika

4
Missenyi
Ujenzi wa karo la kupokelea na kupimia samaki mwalo wa Kabindi na Kaishebo
LVEMP II
Mradi umekamilika

Ujenzi wa mwamba wa kuanika dagaa mwalo wa kibindi.
LVEMP II
Mradi umekamilika

5.
Karagwe
Kuwezesha vikundi vya kufuga samaki kwa kuchimba mabwawa 2
World Vision
Mradi umekamilika

Kudhibiti magugu maji katika mto kagera, Ziwa Rwakajunju kijiji Kafunjo
H/Wilaya na LVEMP II
Mradi umekamilika.

6
Kyerwa
Hakuna mradi
Hakuna
Hakuna

7.
Ngara
Kuchimba mabwawa 79 ya kufuga samaki kata ya Mugoma, Bugarama, Rulenge, Bukiriro, Ngara mjini na Ntobeye.
CHEMA, TCRS,
TASAF,
Mradi umekamilika

8
Biharamulo
Hakuna mradi
Hakuna
Hakuna


 8.0 UWEZESHAJI WAVUVI WADOGO

Serikali imeendelea kuwawezesha wavuvi wadogo kwa kufuta baadhi ya tozo, kutoa ruzuku na kuboresha miundombinu ya Uvuvi ambapo jumla ya Vikundi 9 vimewezeshwa kwa kupewa ruzuku na mikopo ya shughuli za Uvuvi katika Mkoa wa Kagera. Pia Mkoa kwa kushirikiana na Halmashauri imesimamia vyema shughuli za Uvuvi na kutoa ulinzi kwa kufanya kaguzi katika maeneo ya Uvuvi. Usimamizi na uhamasishaji umewezesha kuanzishwa kwa Vyama vya Ushirika wa Wavuvi 7, BMUs 93 pamoja na vikundi vya wavuvi wadogo wadogo 6 katika Mkoa wa Kagera.


 9.0 UTEKELEZAJI WA MPANGO WA NCHI WANACHAMA WA ZIWA VICTORIA

Mkoa wa Kagera umetekeleza mpango kazi wa kanda wa nchi wanachama kwa kufanya kazi kwa kushirikiana na nchi za jirani katika mapambana ya kudhibiti Uvuvi haramu, kuboresha uratibu wa shughuli za Uvuvi na doria. Mkoa wa Kagera kwa kushirikiana na Halmashauri za Wilaya tumekuwa tukiendesha shughuli za doria katika maeneo mbalimbali ya Ziwa Victoria katika mialo yote ya Mkoa wa Kagera na dhana haramu za Uvuvi zimekamatwa.


 10.0 KUELIMISHA JAMII JUU YA ATHARI ZA UVUVI HARAMU NA UKIMWI

Katika kuhakikisha Uvuvi haramu unakomeshwa na kuwafanya wavuvi kufanya Uvuvi endelevu, wataalamu wa Uvuvi Mkoa wa Kagera wamekuwa wakitoa elimu juu ya matumizi bora ya zana za Uvuvi zinazokubalika kisheria na kuwaelimisha wavuvi kufanya Uvuvi endelevu ili kulinda rasilimali za majini kwa kizazi cha sasa na kizazi kijacho.Kwa kipindi chaMwaka wa fedha 2017/2018kuanzia mwezi Julai2017hadi Juni, 2018 njia zifuatazo zimekuwa zikitumika kutoa elimu kwa jamii ya wavuvi juu ya Uvuvi haramu na maambukizi ya VVU/UKIMWI.

  • Kutumia vitabu na vipeperushi mbalimbali vinavyoelekeza njia sahihi zinazofaa kutumika katika kufanya Uvuvi endelevu na athari zinazotokana na Uvuvi haramu.
  • Kufanya mikutano na mafunzo kwa wavuvi na wadau wa Sekta ya Uvuvi kuhusu athari za Uvuvi haramu na faida ya Uvuvi endelevu.Pia elimu juu ya njia za kujikinga na gonjwa la UKIMWI ikiwemo zoezi la kupima VVU/UKIMWI kwa hiari kwa wavuvi hasa wanaoishi kwenye mialo.
  • Kushirikiana na mashirika ya TADEPA, KADEA na ICAP kufanya mikutano ya BMUs, mikutano ya Vijiji, WDC na mikutano ya kisiasa.


 11.0 MAFANIKIO YALIYOPATIKANA

Kwa kipindi cha Mwaka wa fedha 2017/2018, Sekta ya Uvuvi Mkoa wa Kagera imepata mafanikio mengi ikiwa ni pamoja na kudhibiti Uvuvi haramu ili kulinda raslimali ya Uvuvi. Hatua mbalimbali za kisheria zimechukuliwa katika kuzuia Uvuvi haramu ikiwa ni pamoja na wahalifu kufikishwa kwenye vyombo vya sheria na wengine kupewa onyo kali. Aidha, jumla ya doria 131 zimefanyika kwa kipindi cha kuanzia mwezi Julai 2017 hadi Juni 30, 2018 na hivyo kuwezeshwa kukamatwa zana haramu za Uvuvi ambazo ni kokoro za sangala 462, nyavu ndogo za dagaa 221, nyavu za timba 4,189, nyavu za makila 5,300, katuli 17, Ndoano 820 mitumbwi 235, samaki wachanga wenye uzito wa kg16,615 na watuhumiwa 126.

Sambamba na hilo Sekta ya Uvuvi inachangia kwa kiasi kikubwa katika kutoa ajira ambapo zaidi ya wananchi26,830 wameajiriwa au kujiajiri kutokana na Shughuli za Uvuvi Mkoani Kagera. Pia katika uchumi kwa kipindi cha Mwaka wa fedha 2017/2018 kuanzia Mwezi Julai 2017 hadi Juni 2018 jumla ya tani 4,651.8 za samaki zenye thamani ya Tshs Bilioni 27.75, zilivuliwa katika Ziwa Victoria, maziwa madogo madogo (Satellite Lakes) na kwenye mabwawa ya kufugia Samaki yaliyopo Mkoani Kagera.

Pia miradi mbalimbali imetekelezwa Mkoani Kagera ambayo ni miradi ya ufugaji bora wa samaki, miradi ya ujenzi wa vyoo na maeneo ya kupokelea samaki kwenye mialo, miradi ya kudhibiti magugu maji katika Ziwa Victoria, Mto Kagera na maziwa madogo madogo yaliyopo Mkoa wa Kagera. Aidha, jumla ya Shilingi Bilioni1,860,593,416/= zimekusanywakutokana na ada za leseni za Uvuvi na vibali vya kusafirisha samaki, tozo za faini, ushuru, maduhuli na makusanyo mengine ambayo ni sawa na asilimia 128.9 ya malengo yaliyowekwayakukusanyakiasi cha shilingi 1,443,423,000/= kwa Mwakawa fedha 2017/2018 katika Mkoa wa Kagera.

Sambamba na hilo, mwanya wa kutorosha mazao ya Uvuvi kwenda nchi jirani umedhibitiwa kwa kutumia vizuizi vilivyopo mipakani maeneo ya Kyaka na Kashenye Wilaya ya Missenyi, Bugabo na Rubafu Wilaya ya Bukoba vijijini pamoja na Vituo vitano ambavyo ni Bukoba, Rusumo, Kabanga na Murusagamba Wilaya ya Ngara naKanyigoWilaya ya Missenyi.

Mafanikio mengine ni kuendeleza Ukuzaji viumbe hai kwenye maji (aquaculture) ambapo jumla ya mabwawa 619 yamechimbwa katika Mkoa wa Kagera na kupandikizwa vifaranga bora vya samaki pamoja na wananchi kuelimishwa mbinu za Ufugaji bora wa samaki.

Pia tumefanikiwa kulinda mazingira na kuendeleza uhifadhi wa Ziwa Victoria, Mito, maziwa madogo madogo(Satelite Lakes) na maeneo tengefu ambayo shughuli za Uvuvi zinafanyika ikiwa ni pamoja na kulinda Viumbe hai vilivyomo majini kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho.


 12.0 CHANGAMOTOZILIZOPO

Pamoja na mafanikio yaliyopo Sekta ya Uvuvi ina changamoto zifuatazo:-

  • Uvuvi wa zana haramu kama makokoro, nyavu za macho madogo na nyavu za timbahasa nyakati za usiku na wavuvi hao hujihami kwa siraha za asili kama mapanga,mishale, mawe na rungu au nondo.
  • Kukua kwa soko la samaki katika nchi za Ulaya hivyo kusababisha Uvuvi usio endelevu kwa kuvua kupita kiasi.
  • Uharamia ziwani, wizi wa nyavu, mashine na mitumbwi na jamii kujiunga kwa wingi katika shughuli za Uvuvi.
  • Kutokuwa na mipaka inayoonekana ziwani hivyo kusababisha Wavuvi wa nchi moja kuingilia mipaka ya nchi nyingine na kufanikisha utoroshaji wa samaki kwenda nchi njirani hasa usiku.


 13.0 Mkakati wa Kutatua Changamoto zilizopo

  • Kuendelea kutekeleza Sera, Sheria, Kanuni na mikakati mbalimbali ili kulinda raslimali ya Uvuvi kwa ajili ya kizazi cha sasa na kijacho.
  • Kuendelea kudhibiti Uvuvi haramu, biashara haramu ya samakina kudhibiti utoroshaji wa samaki kwenda nchi jirani bila kufuata taratibu;
  • Kuendelea kutoa elimu kwa wavuvi na jamii kwa ujumla kuhusu athari za Uvuvi haramu na namna ya kufanya Uvuvi endelevu;
  • Kuendeleza ufugaji bora wa samaki kwenye mabwawa na Vizimba (Cage culture) kwa kutilia mkazo ufugaji wa samaki kibiashara na kuwashauri wafugaji kuingia katika vikundi (SACCOS) ili wapate mikopo katika taasisi za kifedha.
  • Kuimarisha mtandao wa ushirikiano kwa wadau wote wa maendeleo ngazi ya Serikali,wahisani, NGOs, Wavuvi na Wananchi kwa ujumla.
  • Kudhibiti utoroshaji wa mazao ya samaki kwenda nchi jirani bila kufuata taratibu.
  • Kushirikiana na polisi,uhamiaji na wananchi kubaini na kudhibiti wahamiaji haramu wanaovua kwetu bila taratibu.
  • Kuimarisha mfumo wa kukusanya mapato ya hamlashauri kwa kutilia mkazo usajili wa vyombo vya Uvuvi na kuwa na takwimu halisi.
  • Kuimarisha mfumo wa kukusanya takwimu za Uvuvi (Frame survey) zinazoonyesha idadi ya zana za Uvuvi kama vile mitumbwi, nyavu, samaki na wavuvi wanaovua ziwani.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa