• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Miundombinu

 LENGO LA SEHEMU YA MIUNDOMBINU

Kuwezesha utoaji wa ushauri wa kitaalam katika maendeleo ya miundombinu kwa Halmashauri

Sehemu hii inafanya kazi zifuatazo:-

  • Kuratibu utekelezaji wa shughuli za barabara, majengo, nishati, upimaji, ardhi na mipango miji
  • Kujengea uwezo Mamlaka za Serikali za Mitaa katika masuala ya ujenzi wa barabara, majengo, nishati, upimaji na mipango miji
  • Kuandaa ramani za mipango miji
  • Kukagua na kushauri juu ya michoro ya kihandisi kwa shughuli zinazotekelezwa kwenye mkoa
  • Kumshauri Katibu Tawala Mkoa juu tathmini ya athari ya kimazingira (Environmental Impact Assessment)


 SEKTA ZA MIUNDOMBINU (ARDHI, BARABARA, MAJI, ANGA, NISHATI NA MADINI)
 SEKTA YA ARDHI

 Upimaji wa Viwanja na Mashamba na Umilikishaji

Kwa kipindi cha mwaka 2010 hadi kufikia Septe,mba 12, 2018 viwanja vilivyopimwa ni 14,171 (Bukoba Manispaa 9,991 Bukoba Vijijini 179, Biharamulo 101, Karagwe 832, Ngara 194, Missenyi 859, Muleba 792 na Kyerwa viwanja 1,203) na jumla ya viwanja 4,014 vimemilikishwa kwa wananchi.

Adha, upimaji wa mashamba yenye ukubwa wa hekta 6,613.522 yameweza kupimwa hadi Juni, 2018 (Bukoba Vijijini hekta 67.15, Karagwe hekta 1,877.565, Ngara hekta 776.222, Missenyi hekta 4,204.294, Muleba hekta 14.761 na Kyerwa hekta 36.689).


 Matumizi Bora ya Ardhi

Mkoa una jumla ya vijiji 667 kati ya hivyo Vijiji 535 vimepimwa na Vijiji 132 havijapimwa. Mipango ya matumizi bora ya ardhi imeandaliwa katika Vijiji 68 na jumla ya mashamba 11,213 yameweza kupimwa na hati 5,523 kutolewa kwa wananchi (Bukoba hati 207,  Missenyi ni mashamba 566 na hati 566,  Karagwe ni mashamba 3,238 na hati 2,100,  Ngara ni Mashamba 4,138 na hati 2001  na Muleba ni mashamba 3,271 na hati 649).


 Uboreshaji wa Makazi.

Michoro ya mipango miji ipatayo 345 imeandaliwa katika maeneo ya mijini na vituo vya kibiashara katika maeneo mbalimbali ya halmashauri kwa kipindi cha mwaka 2010 hadi kufikia mwezi Aprili, 2018 (Muleba Michoro ya mipango miji 65, Missenyi 19, Ngara 9, Bukoba 22, Manispaa ya Bukoba 128, Biharamulo 39, Kyerwa 32 na Karagwe 31).

Miji ya Mutukula, Kyaka-Bunazi na Kyerwa katika halmashauri za wilaya za Missenyi na Kyerwa imeweza kutangazwa katika gazeti la serikali kama maeneo ya mpango (Planning Area).

 Mabaraza ya Ardhi

Kufuatia hali ya kuwa na migogoro mingi ya ardhi katika Mkoa wetu, Serikali iliona ni vyema kuwa na Mabaraza karibu ili yaweze kutatua migogoro, katika Wilaya zilizo na migogoro mingi ni Wilaya ya Muleba ambapo Baraza lilizinduliwa tarehe 19 Agosti, 2016, Wilaya nyingine ni Bukoba na Karagwe, hata hivyo Wizara ilishachukua hatua ya kufungua Mabaraza ya Ardhi na Nyumba katika Wilaya ya Muleba, Karagwe na Ngara.


 SEKTA YA BARABARA

Mkoa una jumla ya kilometa 7,827.24 za barabara ikiwemo kilometa 5,909.65 zilizo chini ya Halmashauri za Wilaya na Manispaa (TARURA), Kilometa 1,917.59 za Barabara Kuu na za Mkoa zilizo chini ya TANROADS. Kati ya hizo kilometa 674.05 ni barabara za lami, kilometa 2,805.16 ni barabara za changarawe na kilometa 4,348.03 ni barabara za udongo.

Na.
Aina Ya Barabara

Lami (Km)

Changarawe (Km)

Jumla (Km)

1
Barabara Kuu

551.22

311.66

862.88

2
Barabara za Mkoa

84.60

970.11

1054.71

       Jumla

635.82

1281.77

1917.59

 




Mtandao wa Barabara Kuu na za Mkoa

Hali ya Barabara Kuu na Barabara za Mkoa

Kwa kiasi kikubwa hali ya barabara Mkoani Kagera ziko katika hali nzuri kwa barabara zote isipokuwa barabara ya Rusumo – Lusahunga ambayo imeisha muda wake, hivyo kunahitajika Ukarabati mkubwa (Rehabilitation). Aidha barabara chache hupitika kwa taabu wakati wa mvua nyingi hasa sehemu zenye miinuko mikali.

Hali ya Barabara hizi wakati wa masika zinapitika kwa asilimia 95, wakati wa kiangazi zinapitika kwa asilimia 100 na wakati wote wa mwaka zinapitika kwa asilimia 98. Asilimia hizo 2 zinatokana na sehemu chache korofi za barabara kuu ya lami ya Rusumo – Lusahunga ambayo imechakaa na kuhitaji ukarabati mkubwa na sehemu chache za barabara za Mkoa zenye miinuko.

Miradi Mikubwa ya Maendeleo ya Barabara Mkoani

Baadhi ya Miradi mikubwa ya barabara inayotekelezwa hapa mkoani ya Barabara Kuu ni kama ifuatayo;-

Na
Jina la Mradi
Tarehe ya Kuanza
Gharama Tshs.
Mkandarasi
Mhandisi Msimamizi
Utekelezaji
1
Ukarabati wa Barabara ya Ushirombo- Lusahunga (110Km) Kagera ni Km 52
18/02/2010
114,556,919,193
MS Strabag International GmbH
M/S Smec International (Pty) Ltd
53.29%
2
Ujenzi wa Barabara ya Bwanga- Biharamulo (Km 67)
28/12/2012
57,755,740,000
M/S Sinohydro Ltd Works Ltd
M/S Tanroads Engineering Consulting Unit
68%
3
Ujenzi wa Barabara ya Nyakanazi – Kidahwe (Km 50)
13/06/2014
45,985,780,766.87
M/S Nyanza Road Works Ltd
M/S Intercontinental Consultants and Technocrats Pvt Ltd
36.33%
4
Ujenzi wa Kituo cha Pamoja cha Ukaguzi (ONE STOP INSPECTION STATION) – OSIS  Nyakanazi
15/05/2017
Euro
9,582,090.10
M/S Impressa si Contruzioni Ing. E Montavani S.p.a con socio unico of Italy
M/S Trade Mark East Africa (TMEA) and M/S NimetaConsults (T) Ttd
1.2%



Aidha, ipo miradi inayosimamiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba kupitia mradi wa ULGSP chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia wa uboreshaji miji. Barabara hizi zimeanza kujengwa mwaka huu wa fedha 2018/2019 kwa kiwango cha rami nzito na utagharimu billion 7.03, barabara hizi ni zifuatazo;-

  • Binsaid – Kilimahewa (0.95km)
  • Nyangoye – Bukoba DC-Biharamulo road Junction (1.3km)
  • Bukoba Club – Shore road (1.05km)
  • Nshambya – KCDP (1.7km)


Bajeti ya Barabara kwa Mwaka wa Fedha 2018/19

Bajeti ya matengenezo ya barabara toka fedha za Mfuko wa Barabara kwa Mkoa wa Kagera kwa mwaka wa fedha 2018/19 katika barabara Kuu na Barabara za Mkoa ni shilingi bilioni 14,239,917,000. Kati ya fedha hizo shilingi bilioni 5,734,437,000 ni za matengenezo ya barabara Kuu na shilingi bilioni 8,505,480,000 ni za matengenezo ya barabara za Mkoa. Bajeti ya maendeleo kwa ajili ya matengenezo ya barabara ni shilingi bilioni 9,285,000,000.

Barabara zinazosimamiwa na TARURA

Mkoa wa Kagera una jumla ya Kilometa 6,137.20 za barabara zilizo chini ya Halmashauri za Wilaya na Manispaa ya Bukoba ambazo zinasimamiwa na TARURA.

Mtandao wa Barabara zilizo chini ya TARURA Mkoani Kagera

Na
Mamlaka

Lami (Km)

Changarawe (Km)

Udongo (Km)

Jumla (Km)

1
Biharamulo

-

106.00

317.55

423.55

2
Bukoba Vijijini

0.35

252.45

246.70

499.50

3
Bukoba Manispaa

27.20

35.70

66.60

129.50

4
Karagwe

4.30

322.60

1,044.60

1,371.50

5
Kyerwa

-

198.90

524.60

723.50

6
Missenyi

1.00

219.00

504.90

724.90

7
Muleba

-

139.52

1,265.48

1,405.00

8
Ngara

3.80

250.80

377.60

632.20

Jumla Kuu

36.65

1524.97

4,348.03

5,909.65

Aaidha, TARURA kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019 imetengewa kiasi cha Tsh. 10,152,737,884.68 kwa ajili ya matengenezo ya barabara zilizopo chini yake katika Halmashauri za Mkoa wa Kagera.


USAFIRI WA MAJI

Usafiri wa Majini umeendelea kuwa kikwazo cha Maendeleo ya Mkoa wa Kagera, Meli ya MV Victoria ilisitisha huduma zake baada ya kuharibika na inafanyiwa matengenezo makubwa Jijini Mwanza. Meli ya MV Serengeti imekuwa haifanyi kazi vizuri na mara ya mwisho kuwa safarini ni mwezi Machi, 2016.

Bandari ya Bukoba

Bandari ya Bukoba ni moja katika vituo vinavyounda Bandari ya Mwanza ambayo ndio makao makuu. Bandari hii inatoa huduma kwa abiria na mizigo ya kwenda na kutoka Mwanza na Nchi jirani kutokea Bandari ya Kisumu kwa Nchi ya kenya na Bandari ya Portbell kwa Nchi ya Uganda.

Kwasasa hivi zipo meri za mizigo kutoka Mwanza na kwa mwezi bandari hupokea wastani wa tani 113 na kwa mwaka ni wastani wa tani 1356 za mizigo.  Julai, 2018 bandari imepokea mizigo kutoka Uganda tani 461  zenye bidhaa za madukani. Aidha meri za mizigo zinazotoka mwanza hupeleka wastani wa tani 2,600 za sukari Mwanza kila mwezi

Miundombinu na Vifaa vya Bandari Bukoba

Bandari ya Bukoba ina miundombinu na vifaa vifuatavyo;-

Gati mbili kwa ajili ya meli za mizigo na abiria; moja ikiwa na urefu wa mita 82 ambayo hutumika kuegesha meli za mizigo; gati ya pili ina urefu wa mita 70 hii hutumika kuegesha meli za abiria.

Maghala mawili yenye uwezo wa kuhifadhi tani 500 za mizigo, sehemu ya kupakua/kupakia mafuta (oil jetty) ambayo kwa sasa haitumiki, jengo la abiria ambalo hutumika na abiria wanaposubiri kupanda melini.


USAFIRI WA ANGA
Kiwanja cha Ndege Bukoba

Kiwanja cha Ndege Bukoba ni miongoni mwa viwanja 58 vinavyo simamiwa na kuendeshwa na Mamlaka ya viwanja vya Ndege Tanzania (TAA). Viwanja vingine vilivyo katika Mkoa wa Kagera na vinasimamiwa na Mamlaka ni Biharamulo kikiwa chini ya usimamizi wa Meneja wa kiwanja cha Ndege cha Bukoba. Aidha kipo kiwanja kingine cha Ngara ambacho kutokana na sababu za kijiographia kinasimamiwa na Meneja wa kiwanja cha ndege cha Mwanza.

Kiwanja cha Ndege Bukoba inasemekana kilijengwa miaka ya sitini (1960). Kwa kipindi hicho ujenzi ulikuwa ni wa kiwango cha changarawe na kilikuwa na njia ya kurukia na kutua ndege chenye Urefu wa Mita 1,200 na upana wa mita 20.

Kiwanja hiki kimefanyiwa maboresho katika awamu mbili; awamu ya kwanza yalifanyika marekebisho makubwa ambayo yaliyohusisha kazi ya kuongeza urefu wa njia ya kuruka na kutua ndege kutoka mita 1,200 na kufikia mita 1,700 kwa kiwango cha changarawe (Cement stabilization) kuanzia Mwanzoni mwa mwaka 2009 na kukamilika 2011.

Maboresho ya awamu ya pili yaliyoanza mwanzoni mwa mwaka 2013, yalihusisha upanuzi wa upana wa njia ya kuruka na kutua ndege toka mita 20 na kufikia upana wa mita 30 kwa kiwango cha Lami (alsphat) ikihusisha Ujenzi wa jengo la abiria la kisasa lenye uwezo wa kuchukua abiria 150 kwa saa, uboreshaji wa Mitaro ya maji, (Airside drainage System) Ujenzi wa uzio mpya wa usalama kiasi cha mita 1,200 na ujenzi wa eneo la maegesho (Apron) lenye kuweza kuegesha ndege nne kwa wakati mmoja tofauti na eneo la awali lenye uwezo wa kuegesha ndege moja ndogo.

Kiwanja cha Ndege cha Biharamulo kilijengwa miaka ya 1950 kwa ajili ya matumizi ya wamisionari na kilikabidhiwa Serikalini baada ya vita vya Tanzania na Uganda mnamo mwaka 1979. Kina urefu wa mita 935 na upana wa mita 18 na ni cha kiwango cha nyasi, kina jengo moja tu linalotumika kwa shughuli za utawala na abiria. Jengo hilo lina uwezo wa kuhudumia abiria 40 kwa saa.

Kwa hiyo Mkoa wa Kagera unavyo viwanja vitatu ambavyo ni Bukoba, Ngara na Biharamulo vinavyoendeshwa na kusimamiwa na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania.

Hali ya Miundombinu ya Kiwanja cha Ndege Bukoba

Kiwanja cha Ndege Bukoba kina barabara mbili za kutua na kuruka ndege (“Runways”). Barabara hizo zina urefu wa mita 1,500 na upana wa mita 30, njia hizi huitwa 13/31, njia hizi za kuruka Ndege ndio zinazotumika hivi sasa. Kiwanja hiki hakina taa za kuongozea ndege nyakati za usiku hivyo huduma za kiwanja hiki ni muda wa mchana pekee yaani (sunrise and sunset operations). Aidha kiwanja hiki kina maeneo mawili ya maegesho ya ndege “Apron” ambayo ni ya lami, eneo la maegesho la zamani lenye uwezo wa kuegesha ndege 1 aina ya ATR 42 na eneo la maegesho kuu la jengo Jipya lina uwezo wa kuegesha ndege 2 aina ya ATR 42 na ndege mbili aina ya Caravan.

Pia kiwanja kina jengo la abiria la kisasa (Terminal building) moja la kuhudumia abiria na ukumbi wa watu mashuhuri (VIP). Ukumbi wa abiria wanaoondoka una uwezo wa kubeba abiria 150 kwa wakati mmoja na ukumbi wa abiria wanao wasili unauweza wa kuhudumia abiria 100, hivyo kuwa kiwanja chenye kiwango cha daraja la 3C (aerodrome code). Kiwanja cha ndege Bukoba kinapata huduma ya Usalama wa waongoza ndege kutoka Mwanza Control Tower.

Safari za Ndege na Abiria Kiwanja cha Ndege Bukoba

Kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita, kumekuwa na ongezeko la safari za ndege kutoka miruko ya ndege 1,957 kwa mwaka 2012 hadi kufikia miruko 2,706 mwaka 2016 sawa na ongezeko la asilimia 38.3. Aidha idadi ya abiria kwa mwaka 2012 ilianza kuongezeka kutoka abiria 29,736 hadi 33,128 kwa mwaka 2016 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 11.42. Kwa mwaka 2017/2018 miruko ya ndege ni 1810 ikionyesha kupungua kwa miruko lakini pia kukiwa na ongezeko la abiria hadi 47,959 sawa asilimia 18.2


NISHATI

Mkoa wa Kagera una jumla ya wateja waliounganishiwa umeme 64,453 ambapo kati yao, wateja wa LUKU ni 61,562 na wateja wa kulipia baada ya matumizi ni 2,891.

Kutokana na idadi ya wateja tulionao hadi sasa (64,453), wananchi 484,992 tayari wanafaidi huduma ya umeme moja kwa moja, ambacho ni takribani asilimia 17.2% ya wananchi wote wa Mkoa wa Kagera.

Mahitaji ya juu ya umeme kwa Mkoa sasa yamefika MW 20.1 (Bukoba 6.4 MW kutoka grid ya Uganda, Missenyi 6.3 MW kutoka grid ya Uganda, Karagwe 2.2 MW kutoka grid ya Uganda, Muleba 2.9 MW kutoka grid ya Uganda, Biharamulo 1.2MW kutoka grid ya Taifa na nguvu ya mafuta “generator” na Ngara 1.1 MW kutokana na nguvu ya mafuta “generator”

Upatikanaji wa Nishati ya Umeme

Mkoa wa Kagera kwa sasa unapata umeme kutoka vyanzo vikuu vitatu kama ifuatavyo:-

Umeme Kutoka Shirika la Umeme la Uganda

Umeme kutoka nchi jirani ya Uganda kupitia laini kubwa ya msongo wa kilovolti 132 (132 Kv).

Umeme Kutoka Gridi ya Taifa

Wilaya ya Biharamulo inapata umeme wa Grid ya Taifa kwa msongo wa kilovoti 33 (33 Kv) kutokea Mkoa wa Geita.

Umeme wa Nguvu ya Mafuta

Wilaya ya Biharamulo, licha ya kuwa na umeme wa Gridi ya Taifa, pia ina mitambo ya kufua umeme yenye uwezo wa megawati 2.5 (2.5 MW). Mitambo hii huwashwa kwa dharura pale inapobidi. Wilaya ya Ngara kwa sasa ina chanzo kimoja tu cha umeme, nacho ni mitambo ya kufua umeme yenye uwezo wa megawati 2.5 (2.5 MW).


Miradi ya Umeme
Miradi ya Kufua Umeme

Mkoa ulikuwa na miradi mitatu (3) ya kufua umeme ipo kwenye hatua  za awali za utekelezaji ambayo yote kwa pamoja ikikamilika itaweza kuongeza uwezo wa upatikanaji wa umeme katika Mkoa, na ziada kutumika katika maeneo mengine kupitia Gridi ya Taifa pindi itakapokamilika.

Mchanganuo wa Miradi hiyo ni kama ifuatavyo

Jina la Mradi
Chanzo
Eneo

Uwezo

Hatua ya Utekelezaji

Rusumo
Nguvu ya Maji
Ngara

80 MW

Uko hatua za awali

Kakono
Nguvu ya Maji
Missenyi

53 MW

Uko hatua za awali

Murongo/Kikagati
Nguvu ya Maji
Kyerwa

16 MW

Uko hatua za awali

Kukamilika kwa miradi hii kutaondoa kabisa uhitaji wa Shirika na Nchi yetu kununua umeme kutoka nchi jirani ya Uganda ili kuhudumia Mkoa huu.

Miradi ya Kusafirisha Umeme

Mradi wa kuunganisha Mkoa kwenye Gridi ya Taifa kupitia ujenzi wa line ya msongo wa kilovolti 220 kutoka Geita kupitia Runzewe mpaka Nyakanazi kama awamu ya kwanza. Mradi huu upo kwenye hatua za awali na Mhandisi Mshauri amekwisha patikana. Awamu zitakazofuata muda mfupi baadaye zitahusisha ujenzi wa laini ya msongo wa kilovoti 220kutoka Nyakanazi mpaka Rusumoa na BENACO (Ngara) hadi Kyaka (Missenyi).

Kukamilika kwa miradi hii kutaimarisha zaidi upatikanaji wa umeme katika maeneo yote ya Mkoa wa Kagera bila kutegemea umeme kutoka nchi jirani.

 

Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III)

Mradi wa REA Awamu ya tatu Mzunguko wa Kwanza (Round-1) ulifunguliwa tarehe 11 Julai, 2017 ambao unahusisha;-

Ujenzi wa Km 299.01 wa laini za 33KV

Ujenzi wa Km 574 wa laini za LV

Ujenzi wa Transfoma 287

Uunganishaji wa Wateja 9,136 katika Vijiji 141.

Mawanda ya Mradi

Mradi wa REA (REA III ROUND I) unatarajiwa kujenga laini ya msongo wa kilovolt 33 yenye urefu wa kilomita 299.01, laini ndogo yenye msongo wa volt 230/400 yenye urefu wa kilomita 574 na kunufaisha jumla ya Vijiji 143 na jumla ya wateja 9,141 (ikiwa wateja 8,226 wa njia moja na wateja 916 wa njia tatu) watanufaika wa Mkoa wa Kagera.

Mradi huu utagharimu kiasi cha takribani (Tshs. Bilioni thelathini na nane nukta tano) 38,499,922,525.73/= Chini ni jedwali linaloonyesha mchanganuo wa usambazaji wa umeme kwa kila Wilaya na Idadiya Vijiji vitakavyounganishwa, ikionyesha urefu wa laini, transfom na Idadi ya Wateja watakaounganishwa katika mzunguko wa kwanza wa (REA III Round I)

Jedwali Na. 27: Mawanda ya Mradi wa REA III

NA.

WILAYA

IDADI YA VIJIJI

UREFU WA LAINI KUBWA

UREFU WA LAINI NDOGO

TRANSFOMA

WATEJA TARAJIWA

JUMLA

50 KVA

100 KVA

NJIA MOJA

NJIA TATU

1.

Ngara

21

52.64

100

50

0

1541

171

1712

2.

Missenyi

14

26.37

36

18

0

468

52

520

3.

Kyerwa

22

47.36

94

47

0

1296

144

1440

4.

Muleba

21

9.02

78

39

0

1061

118

1179

5.

Bukoba

23

51.58

98

48

1

1361

153

1514

6.

Biharamulo

21

75.31

92

42

4

1414

157

1571

7.

Karagwe

21

36.73

76

36

2

1084

121

1205

Jumla ya Wigo

143

299.01

574

280

7

8225

916

9141


















 

Kazi inayotekelezwa kwa sasa

Hadi hivi sasa Mkandarasi amefanya kazi ya kupima njia ya Miundombinu ya umeme ili kuwafikia wateja, kazi ambayo imefikia asilimia 100 (100%) kwa Vijiji vyote na hivi sasa ameanza kusimamisha nguzo katika maeneo mbalimbali. Aidha tayali vijiji vitatu (4) vimewashiwa umeme kama ifuatavyo;-

Jedwali Na. 28: Kazi Iliyotekelezwa Hadi Sasa REA III

WILAYA

KIJIJI

Karagwe
Katanda
Kyerwa
Kyerwa
Missenyi
Rushana
Muleba
Buhaya

 

Vijiji vinavyotaraijwa kuwashiwa umeme hivi punde

Bukoba Vijijini
Burugo


Biharamulo
Nyarubungo na

Kakoma


Nguzo za laini ya msongo wa umeme mkubwa(kilovolt 33) zilizosimamishwa ni 8.27km

Kilometa za waya kwa nguzo za msongo mkubwa  (kilovolt 33) zilizovutwa ni 3.036km

Nguzo za laini ya msongo wa umeme mdogo(230/400) zilizosimamishwa ni 28.30km

Kilometa za waya kwa nguzo za msongo mdogo  zilizovutwa ni 2.7km

Mpaka sasa Mradi umetekelezwa kwa asilimia tano nukta saba (5.7%) Kimkoa. Mradi wa REA III mzunguko wa kwanza ni Mradi ambao unatakiwa kukamilika ndani ya miaka miwili (2) toka kuzinduliwa kwake.

Changomoto iliyopo ni kuwa kazi hii inatekelezwa na Mkandarasi mmoja katika Mkoa ambaye anatakiwa kuhudumia Wilaya zote saba (7) za Mkoa.


MADINI

Madini Yapatikanayo Mkoani Kagera

Mkoa wa Kagera una madini yafuatayo kama yalivyo tofautishwa kutokana na Sheria ya Madini ya Mwaka 2010:-

Madini aina ya chuma: dhahabu, bati ghafi, wolframite (WO3), Nickel, Manganese n.k.

Madini ya viwandani: Kaolini, Silica Sand na diatomite.

Madini ya ujenzi: Mchanga, mawe, moram, udongo mfinyanzi, mawe ya vigae

Madini mengine yanaendelea kugundulika kadri taarifa za utafiti zinavyoendelea kutolewa.

Utafiti wa Madini Katika Mkoa

Kwa takwimu zilizopo hadi kufikia mwezi Agosti, 2018, Katika Mkoa wa Kagera kuna jumla ya leseni hai 52 za utafiti mkubwa wa Madini. Leseni hizi zilizotolewa katika Wilaya mbalimbali kama inavyonyeshawa kwenye jedwali hapa chini:

 

Idadi ya Leseni za Utafiti wa Madini

S/N

Jina la wilaya

Jumla ya Idadi ya Leseni za utafiti

Aina ya Madini na Idadi ya leseni

Gold
Nickel
Tin
Zinc
Wolfram
Tantalite
Tangsten
Silica sand

1

Biharamulo

22

19

3

0

0

0

0

0

0

2

Kyerwa

15

0

1

9

0

2

2

1

0

3

Ngara

10

1

6

1

1

0

1

0

0

4

Karagwe

2

0

0

2

0

0

0

0

0

5

Muleba

1

0

1

0

0

0

0

0

0

6

Missenyi

1

0

0

1

0

0

0

0

0

7

Bukoba

1

0

0

0

0

0

0

0

1

Jumla

52

20

11

13

1

2

3

1

1


Leseni za Madini Zilizopo Katika Mkoa

Aina za leseni za uchimbaji zilizopo Mkoani Kagera zimegawanyika katika makundi matatu ambazo ni Leseni kubwa za Uchimbaji (SML), Leseni ndogo za Utafiti na Uchimbaji (PML) pamoja na Leseni za kushikilia eneo yaani Retention License (RL). Idadi ya leseni hizo ni kama ifuatavyo:

Leseni za Madini Zilizopo Katika Mkoa

Aina ya Madini
Idadi
Mmiliki
Leseni kubwa za Uchimbaji (SML)

1

STAMIGOLD
Leseni ndogo za uchimbaji (PML)

535

Wachimbaji wadogo
Retention License (RL)

1

Kabanga Nickel


Uchimbaji na Uzalishaji wa Madini Mkoani

Madini yanayochimbwa na mchimbaji mkubwa ni dhahabu. Madini haya yanachimbwa na kampuni ya Stamigold Company Ltd Gold Mine huko Biharamulo.  Madini mengine yana chimbwa na wachimbaji wadogo ni pamoja na Bati, Kaolin na Madini ujenzi (mchanga, kokoto).

Uzalishaji wa Dhahabu na Madini ya fedha (Silver)

Uzalishaji waMadini ya dhahabu na fedha kwa kiasi kikubwa umekuwa ukifanyika katika leseni namba SML 157/2003 inayomilikiwa na Kampuni ya STAMIGOLD wilayani Biharamulo. Katika kipindi cha mwezi Julai 2014 mgodi huo ulipoanza kuendeshwa na Serikali hadi mwezi Agosti, 2018, Uzalishaji wa Madini ulikuwa kama ilivyoainishwa kwenye jedwali hapa chini:

Uzalishaji wa Madini katika Mgodi wa Stamigold

Mwaka

Uzalishaji/Mauzo kwa Kgs

Jul-Des, 2014
                         188.33
Jan-Des, 2015
                         726.24
Jan-Des, 2016
                         655.42
Jan-Des,2017
                         289.71
Jan-Agu,2018
                         238.26
JUMLA
                     2,097.96 


Jumla ya thamani ya Madini hayo ni Dola za Kimarekani 66,745,042.04. Uzalishaji Madini katika mgodi huo umechangia Serikalini mapato ya jumla ya Dola za Kimarekani 2,809,621.75 ambapo Dola za Kimarekani 2,705,897.42 ni mrabaha na Dola za Kimarekani 103,724.33 ni ada ya ukaguzi ambayo ilianza kutozwa mwezi Julai, 2017 baada ya marekebisho ya Sheria ya Madini.

Madini ya dhahabu pia yanachimbwana wachimbaji wadogo katika maeneo ya Busiri, Mavota na Kalukwete Wilayani Biharamulo. Wachimbaji hao wanakabiliwa na changamoto mbalilmbali zikiwemo vitendea kazi na elimu duni ya masuala ya utafiti na na uchimbaji.

Tangu shughuli hizo zianze kushamiri katika maeneohayo mwezi Februari 2017 hadi Agosti, 2018, jumla ya Gramu 1,875.27 za Madini ya dhahabu yenye thamani ya jumla ya shilingi za kitanzania 126,505,000/= ziliripotiwa kuzalishwa na kulipiwa Mrabaha wa kiasi cha jumla ya shilingi 4,881,260/=.

Uzalishaji wa Bati Ghafi (Tin)

Madini haya yanachimbwa na wachimbaji wadogo hususani katika Wilaya ya Kyerwa. Katika kipindi cha mwaka 2015/16 hadi Januari 2017/ 2018 jumla ya tani 181.305 za bati ghafi zenye takribani thamani ya shilingi 3,368,168,680/= zilizalishwa katika maeneo mbalimbali wilayani Kyerwa.

Uzalishaji wa Madini ya Ujenzi na Kaolin

Uzalishaji wa madini ya kaolini unafanyika katika Wilaya ya Biharamulo na Madini Ujenzi ni katika Wilaya zote za Mkoa huu. Uzalishaji wa madini haya kuanzia 2015/16 hadi Agost, 2018 ni kama ifuatavyo:

Jedwali Na. 32: Uzalishaji wa Madini ya Ujenzi na Kaolin

Na.

Aina ya Madini

Kiasi (Tani)

Thamani (Tsh)

Mrabaha uliolipwa (Tsh)

1.
Kaolin

1,770.75

148,257,333.33

4,334,480

2.
Madini Ujenzi

162,187.83

2,081,920,184.59

55,659,242.46


Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa