• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mifugo

Mkoa wa Kagera unakadiriwa kuwa na ng’ombe wapatao 550,070 wanaofugwa ambapo ng’ombe wa asili ni 528,632 na ng’ombe wa maziwa ni 21,438. Mbuzi wafugwao ni 593,607 ambapo mbuzi wa asili ni 583,202 na mbuzi wa maziwa ni 10,405. Wanyama wengine ni kondoo 53,061 na nguruwe 44,402.

Mazao ya mifugo

a)      Maziwa

Mkoa unakadiriwa kuwa na ngo’ombe wa maziwa 21,169 na kwa mwaka 2014/2015 mkoa umeweza kupata maziwa lita 43,915,266 ukilinganisha na lita 14,870,268 kwa mwaka 2013/2014 ambapo kuna ongezeko la lita 29,044,998. Ng’ombe hawa wana uwezo wa kuzalisha maziwa wastani wa lita 5.6 kwa ngo’mbe mmoja kwa siku. Uhamasishaji wa unywaji wa maziwa unaendelea vizuri kwani hivi sasa kumekua na maduka maalumu ya uuzaji wa maziwa tayari kwa kunywa (Milk Bars) ambayo yanachangia kufanikiwa kwa biashara ya maziwa.

b)     Mayai

Ufugaji wa kuku wa mayai kwa mkoa wa kagera unaendelea kuimarika ambapo kwa mwaka 2014/2015 jumla ya mayai 10,783,016 yaliripotiwa kukusanywa na thamani yake ni Tsh 2,804,476,900. Asilimia kubwa ya mayai haya hukusanywa kutoka kwa kuku wa kienyeji. Mkoa unaendelea kutoa elimu kwa wafugaji wa kuku ili waweze kuongeza uzalishaji wa mayai na pia kupambana na magonjwa mbalimbali yanayoadhiri ndege hawa na kusababisha vifo. Kwa sasa ugonjwa unaosababisha vifo vingi vya kuku ni ugonjwa wa mdondo wa kuku. Hivyo wafugaji wanahaswa kuchanja kuku dhidi ya ugonjwa huu kwa wakati.

c)      Ngozi

Mkoa wa Kagera umeendelea kuimarisha zao la ngozi kwa kuhimiza utunzaji wa ngozi inapokua kwa mnyama hai hadi pale inapovunwa kwa ajili ya kuuzwa kama zao la ngozi. Kwa mwaka 2014/2015 mkoa umekusanya jumla ya Ngozi za Ngo’mbe 23,288 na za mbuzi pamoja na kondoo 17,464. Uwekezaji katika viwanda vya usindikaji ngozi ni mdogo na hivyo kusababisha dhamani ya ngozi kushuka, hivyo sekta hii inahimiza na kukaribisha wawekezaji kujikita katika soko la ngozi kwani likitiliwa mkazo litawafaidisha wafugaji na wafanyabiashara wa zao la ngozi pamoja na taifa kwa ujumla.

Ranchi za Taifa (NARCO)

Mkoa wa Kagera unaongoza kwa kuwa na huria nyingi za Taifa ambapo zipo huria 5 kati ya 10 zinazomilikiwa na Kampuni ya Ranchi za Taifa (National Ranching Company Ltd – NARCO). Huria hizo ni Missenyi, Kitengule, Kikulula, Mabale na Kagoma. Eneo lote la huria mkoani lina ukubwa wa hekta. 135,802. Katika harakati za kuongeza uzalishaji wa mifugo na kuongeza ufanisi katika matumizi ya huria hizi, serikali iligawanya ranchi hizi katika vitalu na kukodisha kwa wawekezaji wakubwa na wadogo asilimia kubwa wakiwa ni Watanzania. Hivi sasa wawekezaji waliokodisha vitalu hivyo wanakadiriwa kuwa na jumla ya ng,ombe 25,748, mbuzi 2,1262 na kondoo 1,269. Huria hizi zimeajiri wafanyakazi 302 ambao wengi wao ni wachungaji. Hata hivyo wawekezaji hawa wamewekeza katika ujenzi wa miundombinu kama vile nyumba za wafanyakazi, ofisi, uchimbaji wa mabwawa, kujenga uzio na pia uchimbaji wa visima vya maji. Pia baadhi ya wawekezaji hawa wamenunua usafiri wa kazi kama vile magari (pick up), pikipiki, baiskeli na matrekta. Pamoja na hayo yote bado kuna changamoto ya uvamizi wa wananchi kuanzisha makazi katika vitalu vilivyokodishwa kwa wawekezaji hawa na kuzuia uwekezaji kufanyika kwa haraka zaidi. Hata hivyo Mkoa unaendelea kutatua migogoro inayokwamisha maendeleo ya sekta ya mifugo ili wananchi wa Kagera waweze kufaidi matunda ya ranchi hizi.

Miundombinu na huduma za sekta ya mifugo

Miradi inayotekelezwa chini ya Mipango ya Maendeleo ya Kilimo ya Wilaya (District Agricultural Development Plans –DADPs) inasaidia kwa kiasi kikubwa katika ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya mifugo. Hivi sasa Mkoa una jumla ya majosho 63 kati ya 118 sawa na asilimia 53% ambayo yanafanya kazi na juhudi za kufanya ukarabati wa majosho mengine zinaendelea. Hali ya uogeshaji mifugo imeendelea kuimarika na hivyo kupunguza magonjwa yanayoenezwa na kupe.

Mkoa una jumla ya minada ya mifugo kumi na minne(14) ambapo ya Awali ni 10, la upili moja na Minada ya Mipakani mitatu (3).

Minada ya Awali inasimamiwa na Halmashauri za Wilaya na ni chanzo cha mapato ya Halmashauri. Minada ya Upili na Mipakani ni minada inayosimamiwa na Serikali Kuu. Pia kuna malambo kumi na saba, machinjio hamsini na tano (55) ambapo mkubwa ni mmoja uliopo katika Manispaa ya bukoba.

Miundombinu ya mifugo:

WILAYA
Majosho
Wataalamu wa mifugo.
idadi
Yanayofanya kazi
Yasiyofanya kazi
Ofisi za uuguzi
Daktari wa mifugo
Maafisa mifugo
Maafisa ugani
Afisa ndorobo
Liv. Field Auxiliary
Ras Kagera
0
0
0
0
1
2
0
0
0
Muleba
27
24
3
1
1
0
21
1
1
Karagwe
17
1
16
1
0
2
18
1
1
Biharamulo
5
2
3
1
1
1
12
0
0
kyerwa
6
0
6
1
1
2
14
0
1
Bukoba manispaa
0
0
0
0
0
0
6
0
1
Bukoba vijijini
24
16
8
1
2
1
27
0
0
Misenyi
19
7
12
2
1
1
17
0
0
Ngara
20
13
7
1
1
0
14
2
2
Jumla
118
63
55
8
8
9
129
4
6

 

Huduma nyingine za Mifugo

WILAYA
Masoko ya mifugo
Malambo
machinjio
Mabanda ya ngozi
Maduka ya dawa
Kliniki za mifugo
Muleba
2
0
10
10
7
7
Karagwe
3
2
10
10
13
13
Biharamulo
2
8
10
3
3
3
kyerwa
1
0
3
3
3
3
Bukoba manispaa
0
0
1
1
2
4
Bukoba vijijini
1
3
7
2
4
12
Misenyi
2
4
5
6
4
6
Ngara
3
0
9
5
6
5
Jumla
14
17
55
40
42
53

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa