• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government KAGERA REGIONAL WEBSITE

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections/Units
      • Sections
        • Management Monitoring and Ispection
        • Infrastructure
        • Education
          • Primary Education
          • Secondary Education
          • Adult Education
          • Higher Education
          • Sports
          • Youth
        • Health
          • Health
          • social welfare
        • Administration And HR
        • Planning & Coordination
          • Planning
          • Statistics
          • Community Development
          • TASAF
        • Economic and Production
          • Irrigation Farming
          • Commerce and Industries
          • Fishing
          • Livestock
          • Natural Resources, Tourism & Environment
          • Co operative
          • Agriculture
        • Investment Indusrty and Trade
      • Units
        • ICT
        • Legal Unit
        • Finance and Accounts
        • Internal Audit Unit
        • Procurement Unit
        • Government Communication
  • Districts
    • Bukoba
      • Bukoba Leaders
    • Biharamulo
      • Biharamulo Leaders
    • Karagwe
      • Karagwe Leaders
    • Kyerwa
      • Kyerwa Leaders
    • Missenyi
      • Missenyi Leaders
    • Muleba
      • Muleba Leaders
    • Ngara
      • Ngara Leaders
  • District Councils
    • Bukoba Municipal Council
    • Bukoba District Council
    • Biharamulo District Council
    • Karagwe District Council
    • Kyerwa District Council
    • Missenyi District Council
    • Muleba District Council
    • Ngara District Council
  • Investment Opportunities
    • Tourism Attractions
    • Farming Opportunities
    • Agricultural Opportunities
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • Water Services
    • Agricultural Services
    • Farming Services
  • Publications
    • By Laws
    • Client Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • News Letter
  • Media Center
    • Videos
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

ICT

LENGO LA KITENGO CHA TEHAMA

Kuwezesha utoaji wa ushauri wa kitaalam katika sekta za uchumi na uzalishaji kwenye Halmashauri

Sehemu hii inafanya kazi zifuatazo:-

  • Kushauri Menejimenti juu ya mausala ya TEHAMA na utekelezaji wa e-government/serikali mtandao
  • Kufuatilia na kusaidia Mamlaka za Serikali za Mitaa juu ya masuala TEHAMA
  • Kutoa msaada wa kiufundi katika matumizi ya vyombo vya kielektroniki
  • Kushauri Menejimenti juu ya utekelezaji wa sera ya TEHAMA

Kwa kuzingatia umuhimu wa TEHAMA na lengo la serikali la kuwa na serikali mtandao, Mkoa wa Kagera ni miongoni mwa taasisi za serikali ambao unafanya vizuri katika eneo la TEHAMA.

Teknolojia ya Habari na Mawasiliano Mkoani Kagera ni ya kuridhisha kwa sasa.

MAWASILIANO YA SIMU

Kampuni kongwe ya TTCL ndio inayotoa huduma za mawasiliano ya njia ya simu katika ofisi zote za serikali na mashirika Mkoani Kagera. Makampuni mengine ya simu za mkononi yametawanyika vizuri hadi katika baadhi ya vijiji na hivyo kufanya mawasiliano kuwa rahisi zaidi. Hali hiyo imewasaidia wakulima kujua bei halali ya soko la mjini kwa mazao yao na hivyo kuondoa adha ya kuibiwa na wafanyabiashara kwa kisingizio kuwa soko la bidhaa husika ni mbaya.

TELE-CENTERS

Mkoa una vituo viwili hadi sasa vinavyotoa huduma ya TEHAMA vijijini. Kituo kimoja kipo wilaya ya Bukoba vijijini katika kijiji cha Kibegwe kata ya Bugabo, na kingine kipo katika wilaya ya Ngara. Vituo hivyo vimekuwa vikitoa huduma nzuri kwa wanavijiji wa maeneo husika, ingawa vimekuwa havitoi huduma ipasavyo kutokana na mwamko duni wa wanavijiji katika matumizi ya TEHAMA.

VITUO VYA REDIO

Kutokana na mabadilko ya sera za habari na mawasiliano ambapo vituo binafsi vya radio vimeruhusiwa kuanzishwa, mkoa wa Kagera sasa una vituo vitano (5) vya radio. Vituo hivyo ni

Kasibante FM Redio iliyoko Bukoba

Radio Vision iliyoko Bukoba

Karagwe FM iliyoko Karagwe

Redio Fadeko iliyoko Karagwe

Radio Kwizera iliyoko Ngara

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa imejenga miundombinu ya TEHAMA iliyo bora kwa ajili ya kuwa na serikali -mtandao .Aidha Ofisi nyingi hapa Mkoani hutumia teknolojia ya kompyuta katika kufanikisha shughuli za kila siku.

Hadi kufikia Septemba, 2013 mifumo mbalimbali ya kompyuta zaidi ya ishirini imefungwa katika Ofisi za serikali mkoani Kagera ili kurahisisha utendaji kazi wake. Ofisi moja ya mkuu wa wilaya ya Muleba imefungiwa miundombinu ya intaneti na hivyo kurahisisha mawasiliano kati ya Ofisi ya mkuu wa Mkoa na ofisi hizo. Aidha, mkoa unaendelea na juhudi za kuhakikisha kila Ofisi ya mkuu wa wilaya inafungiwa miundombinu ya intaneti ili kurahisisha mawasiliano.

Halmashauri za Ngara, Biharamulo, Kyerwa na Bukoba hazina miundombinu ya TEHAMA iliyo bora hadi sasa isipokuwa Manispaa ya Bukoba na halmashauri za Karagwe na Misenyi. Juhudi nyingi zinafanywa ili kujenga miundombinu hiyo kabla ya mwaka 2015 kwa lengo la kuharakisha lengo la serikali la kuwa na Serikali -Mtandao.

HUDUMA YA INTANETI

Huduma ya intaneti Mkoani Kagera hutolewa na makampuni mbalimbali. Kampuni kongwe ya TTCL ndiyo inayotoa huduma ya intaneti katika ofisi nyingi za serikali na mashirika. Aidha, makampuni ya simu za mikononi kama Vodacom, Tigo, Airtel na Zantel yanatoa huduma muhimu ya intaneti kupitia simu za mikononi na "moderm". Zipo pia baadhi ya ofisi ambazo hutumia makampuni mengine kwa ajili ya kupata intaneti. Makampuni hayo ni pamoja Simbanet ya jijini Dar es Salaam.

MKONGO WA TAIFA

Mkongo wa Taifa ambao tayari umefika mkoani Kagera, umeweza kuongeza ufanisi wa huduma ya intaneti kwa kiwango kikubwa. Hadi sasa kampuni ya simu ya TTCL imeweza kutoa huduma bora zaidi za intaneti baada ya mkongo wa Taifa kuanza kufanya kazi hapa mkoani Kagera. Uwepo wa mkongo wa Taifa umepunguza gharama za intaneti katika ofisi za Serikali na pia umeongeza watumiaji wa intaneti katika Mkoa wa Kagera. Baadhi ya mabenki Mkoani Kagera, ofisi za TRA, Ofisi ya madini, NSSF zimeungwanishwa kwenye mkongo kupitia TTCL.

MIFUMO YA KOMPYUTA INAYOTUMIKA HADI SASA MKOANI KAGERA

Hadi kufikia Septembal, 2013 ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kagera, Halmashauri za mkoa na manispaa ya Bukoba zimefungiwa mifumo ifuatayo;

Epicor--Mfumo huu hutumika katika kuandaa na kutoa malipo. Mfumo huu umesaidia sana na umepunguza hoja za ukaguzi kwa kiwango kikubwa. Mfumo huu umeunganishwa kwa kutumia mkongo wa Taifa.

SBAS--Huu ni mfumo kwa ajili ya kuandaa mipango ya serikali kuu.Bajeti ya Sekretariet ya Mkoa huandaliwa kwa kutumia mfumo huu.

PlanRep--Mfumo huu ni sawa na SBAS, tofauti ya mifumo hii miwili ni kuwa mfumo huu wa PlanRep hutumiwa na Halmashauri pamoja na Manispaa wakati wa kuandaa bajeti za Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

CDR na CFR--Hii ni mifumo inayotumika kutolea taarifa za miradi ya maendeleo katika ngazi za Mamlaka ya Serikali za Mitaa.

ETR--Huu ni mfumo unaotumika kutunza takwimu za wagonjwa wa kifua kikuu

LGHRIS-Mfumo huu unatumika katika kutunza taarifa za watumishi na unatumika katika ngazi ya mkoa na halmashauri.

Lawson-Huu ni mfumo unaotumika katika mishahara, kwa kutumia mfumo huu, serikali imeondoa tatizo la mishahara hewa, kuchelewa kwa stahili za watumishi n.k.

LGMD- Mfumo huu unatumika katika kukusanya na kutunza takwimu katika ngazi ya halmashauri. Takwimu hizi ndizo hutumika katika kuandaa mipango ya halmashauri.

MVC Database-Mfumo huu hutumika katika kutunza taarifa za watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi katika ngazi ya halmashauri.

Aidha, ipo mifumo mingine ambayo si rahisi kuiweka hapa ambayo inapatikana katika baadhi ya halmashauri.

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • View All

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
More Videos

Quick Links

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Radio Stations in Kagera Region
  • Kagera Regional Commissioners Since Independence 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • National Bureau of Statistics (NBS)
  • Government of Tanzania Website
  • Open Data Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Postal Address: S.L.P 299 BUKOBA

    Telephone: 255 28 2220215/17

    Mobile:

    Email: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Hakimiliki

Copyright ©2017 GWF . All rights reserved.