• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government KAGERA REGIONAL WEBSITE

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections/Units
      • Sections
        • Management Monitoring and Ispection
        • Infrastructure
        • Education
          • Primary Education
          • Secondary Education
          • Adult Education
          • Higher Education
          • Sports
          • Youth
        • Health
          • Health
          • social welfare
        • Administration And HR
        • Planning & Coordination
          • Planning
          • Statistics
          • Community Development
          • TASAF
        • Economic and Production
          • Irrigation Farming
          • Commerce and Industries
          • Fishing
          • Livestock
          • Natural Resources, Tourism & Environment
          • Co operative
          • Agriculture
        • Investment Indusrty and Trade
      • Units
        • ICT
        • Legal Unit
        • Finance and Accounts
        • Internal Audit Unit
        • Procurement Unit
        • Government Communication
  • Districts
    • Bukoba
      • Bukoba Leaders
    • Biharamulo
      • Biharamulo Leaders
    • Karagwe
      • Karagwe Leaders
    • Kyerwa
      • Kyerwa Leaders
    • Missenyi
      • Missenyi Leaders
    • Muleba
      • Muleba Leaders
    • Ngara
      • Ngara Leaders
  • District Councils
    • Bukoba Municipal Council
    • Bukoba District Council
    • Biharamulo District Council
    • Karagwe District Council
    • Kyerwa District Council
    • Missenyi District Council
    • Muleba District Council
    • Ngara District Council
  • Investment Opportunities
    • Tourism Attractions
    • Farming Opportunities
    • Agricultural Opportunities
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • Water Services
    • Agricultural Services
    • Farming Services
  • Publications
    • By Laws
    • Client Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • News Letter
  • Media Center
    • Videos
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Sports

MAENDELEO YA MICHEZO MKOA WA KAGERA

 UTANGULIZI

Michezo ni kielelezo na utambulisho wa Utamaduni wa mtu, watu, jamii au Taifa; michezo ni chombo kinachokuza ustawi wa maendeleo ya jami,kujenga utimamu wa akili na mwili. Kutokana na umuhimu huo michezo na Utamaduni vimepitia katika hatua mbalimbali za mabadiliko yakiwemo ya kisayansi na kiteknolojia mfano watanzania wanashirikisha katika michezo ya jadi iikiwemo bao, kulenga shabaha na mishale. Baada ya ukoloni michezo michezo mipya ilitambulishwa ikiwemo mpira wa miguu, netiboli, ngumi, mpira wa meza na mpira wa mikono michezo hii ilienea Tanzania na duniani kote ikitambulika kama michezo ya ridhaa (Sports Ameuture) ambapo hivi leo michezo ni ajira na ni biashara duniani nzima.

 

HALI MAENDELEO YA MICHEZO MKOA WA KAGERA;

Mkoa una kiwanja kikuu cha mpira wa miguu cha kisasa cha Kaitaba kilichopo mjini  (Artificial glasses play ground pitch)  ambacho kilijengwa kwa ufadhili wa FIFA. Aidha, Mkoa una kiwanja dada cha Halmashauri ya Wilaya ya Muleba. Halmashauri za Wilaya zimetenga maeneo wazi “Open spaces and recreation” kwa ajili ya maendeleo ya michezo kwa lengo la ubuaji vipaji.


TAKWIMU ZA KIMAENDELEO TASNIA YA MICHEZO MKOA KAGERA

S/N
        ENEO   LA MAENDELEO

       JUMLA

1.
VYAMA
VILIVYOSAJILIWA

69

69

 VISIVYO NA USAJILI

11

11

2.
WAAMUZI (REFEREES)
DARAJA LA  IV

52

52

DARAJA III

61

61

DARAJA  LA  I

4

4

3.
MAKOCHA
DARAJA LA  IV

48

48

DARAJA LA III

148

148

DARAJA LA  I

2

2

4.
VILABU
DARAJA LA IV

82

                                        82

DARAJA LA III

18

18

LIGI KUU  I

1

1

5.
VIWANJA
VIKUU (STANDARDs)

2

2

VYA SHULE NA VYUO

826

                                             826

MAFUNZO YA MUDA MREFU - DIPLOMA

6

6

MSINGI/SEKONDARI

505

505

 

USHIRIKI KATIKA MASHINDANO YANAYOANDALIWA NA VYAMA VYA MICHEZO NCHINI;-

Mkoa wa Kagera unashiriki kwenye ligi kuu ya soka (TPL) ambapo timu ya Kagera Sugar Football Club inashiriki ligi hiyo kwa mafanikio sanjari na timu za mpira wa wavu, netiboli na ngumu zimekuwa zikiuwakilisha mkoa vema. Aidha, kwa upande wa waamuzi mkoa unawakilishwa vema na Jonesia Rukyaa mwamuzi wa ligi kuu ya Tanzania ambaye anatambuliwa na TFF, CAF na FIFA.

MAENDELEO YA MICHEZO KATIKA TAASISI ZA SERIKALI;-

Katika mashindano ya Shule za Msingi (UMITASHUMTA) na Shule za Sekondari (UMISSETA) mkoa umekuwa ukifanya vizuri kwa kupeleka idadi kubwa ya wanamichezo wanaounda timu ya Mkoa na hatimaye kuchaguliwa katika timu za Taifa kwenye mashindano mbalimbali. Aidha, katika mwaka 2019 Mwanafunzi Kassim Ibrahim aliibuka kuwa mfungaji bora kwa Afrika mashariki kwenye mashindano ya shule za Sekondari yaliyofanyika mkoani Arusha.

 

 MCHANGO WA MICHEZO KATIKA USTAWI WA JAMII, AFYA NA NGUVU KAZI YA TAIFA.

Ili kutoa mchango wenye tija kwa jamii na Taifa kwa ujumla mkoa una programu ya kudumu ya mazoezi kwa afya kwa wananchi na watumishi wa umma ambayo hufanyika kila siku ya jumamosi yakihusisha mamlaka zote za Sekali za Mitaa, Taasisi, Idara na watu binafsi. Mazoezi yanalenga kudhibiti magonjwa yasiyo ya kuambukiza (kisukari, shinikizo la Damu). Kutoa mafunzo ya namna bora ya kujikinga na magonjwa nyemelezi na ulaji sahihi na bora kwa wananchi ili hatimaye kupunguza vifo kwa wananchi na kuipunguzia gharama Serikali katika kutibu magonjwa yanayotibika kupitia mazoezi.


MIKAKATI YA KUINUA NA KUENDELEZA MICHEZO MKOA KAGERA MWAKA, 2020

Kuwepo kwa programu ya mafunzo ya michezo kwa walimu wa michezo mbalimbali.

Kuwepo kwa programu ya michezo kwa watumishi wa Serikali kuu na Mamlaka za Serikali za Mitaa kila mwisho wa mwaka

Kuanzisha vilabu vya mozezi mepesi (Jogging clubs, beach Clubs n.k)

Kuendelea kuwahamasisha Mamlaka za Serikali za Mitaa kupeleka walimu wa michezo katika mafunzo ya muda mrefu na mfupi katika vyuo vya maendeleo ya michezo nchini.

Kuhamasisha taasisi na Idara za Serikali kushiriki katika michezo.

Kuandaa mabonanza yanayoshirikisha  mikoa jirani na mikoa ya iliyopo katika nchi jirani

Kusudio la vituo vya michezo kwenye shule za msingi na sekondari

Ngoma za asili za kabila la Wahaya hazijasahaulika sana, vikundi mbalimbali vya ngoma kama vile Lugoloile, Zikolwe Engozi, Mikoni pamoja na Kikundi cha Muziki wa Dansi - KAKAU BENDI.

 

HALI YA MAENDELEO YA USTAWI WA UTAMADUNI KATIKA MKOA;

Mkoa una maeneo mbalimbali ya Makumbusho pamoja na Vivutio vya Utalii  kwa ajili ya kuhifadhia mila  na Utamaduni wa Mkoa  huu pamoja na kusaidia ukuaji wa uchumi ambapo maeneo hayo ni yanavyooneka kwenye jedwali hapa chini;

TAKWIMU ZA VIVUTIO VYA UTALII KATIKA MKOA WA KAGERA;-

S/N
ENEO
SHUGHULI
 MAHALI LILIPO
1.
Katuruka
Uhunzi na Ufuaji wa Vyuma
Bukoba (V)
2.
Bwanjai
Mapango na Maandishi ya Watu wa kale
Missenyi
3.
Kanazi
Jengo la Makumbusho
Bukoba (V)
4.
Radio Tower
Makumbusho ya Wajerumani
Ujirani mwema - Bukoba
5.
Germany Cemetries
Makaburi ya Wajerumani
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa- Kagera
6.
Kiroyera Tours
Makumbusho pamoja na Utalii
Bukoba (M)
7.
Germany Building
Duka la Bishara
Bukoba (M)
8.
Nyumba ya Msonge
Makumbusho ya Watu wa Kale
Muleba


Mkoa una jumla ya vikundi vya sanaa na utamaduni thelathini na tatu (35) vikihusisha Muziki wa Asili “AKASIMBO” na “AMAYAGA’ pamoja na Bendi ya Muziki wa Dansi ya Kakau Bendi iliyopo Manispaa ya Bukoba pamoja na vikundi mbalimbali vya filamu na maigizo pamoja na vichekesho;-


HALI YA VIVUTIO VYA UTALII KATIKA MKOA; 

Mkoa unavivutio mbalimbali vya  Utalii kama inavyoonekana hapa chini

  • Ibanda Game Reserve - Wilaya ya Kyerwa
  • Kimisi Game Reserves - Wilaya ya Karagwe
  • Maporomoko ya Maji ya Bogonzi “bugonzi water falls” yaliyopo Kamachumu Wilaya ya Muleba.
  • Msitu wa Minziro ulio na Vipepeo ambao hawapo duniani pamoja na nyoka anayesadikiwa kuishi miaka zaidi ya miamoja.
  • Rusumo Water Falls - Wilaya ya Ngara
  • Visiwa vya Musira, Rubondo, Bumbile, Goziba,Kerebe vinavyofanya Mkoa huu uwe na vivutio vingi vinavyoweza kutoa ajira kwa vijana na kuongeza pato la Mkoa na Taifa kwa ujumla.

CHANGAMOTO ZA SEKTA YA UTAMADINI NA MICHEZO KATIKA MKOA 

 Jamii kuiga tamaduni za nje pamoja na kutofanya utalii kwenye vivutio kwa ajili ya kujifunza na kukuza uchumi wa Mkoa.

Vyama vya michezo kukosa udhamini wa programu na mashindano ya michezo mbalimbali.

Ukosefu wa Wataalamu wa mambo ya kale unaotokana na vifo na waliopo kutotembelea Mkoa wa Kagera kwa ajili ya kutoa Ushauri wa namna ya uhifadhi mambo ya kale kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Wizi wa makusudi wa kazi za Wasanii unaotokana na kukuwa kwa kasi kwa Teknolojia ya Habari na mawasiliano duniani.

Uvamizi wa maeneo wazi ya viwanja vya Michezo na kutumika katika shughuli nyingine.

Vyama vya michezo kushindwa kujiendesha kutokana na ukosefu wa fedha

‘‘KAGERA, KAZI AMANI NA MAENDELEO“

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • View All

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
More Videos

Quick Links

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Radio Stations in Kagera Region
  • Kagera Regional Commissioners Since Independence 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • National Bureau of Statistics (NBS)
  • Government of Tanzania Website
  • Open Data Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Postal Address: S.L.P 299 BUKOBA

    Telephone: 255 28 2220215/17

    Mobile:

    Email: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Hakimiliki

Copyright ©2017 GWF . All rights reserved.