• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Profesa Kamuzora Ahitimisha Wiki ya Utumishi wa Umma Kagera Kwa Kuwakumbusha Watumishi Wajibu Wao wa Kuchapa Kazi Kwa Uadilifu

Imewekwa : June 25th, 2019

Wiki ya Utumishi wa Umma Mkoani Kagera yahitimishwa na Katibu Tawala Mkoa Profesa Faustin Kamuzora ambaye ni msimamizi mkuu wa watumishi wa umma katika Idara na taasisi zote za umma mkoani humo ambapo alihitimisha kwa kuongea na watumishi hao katika viwanja vya ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera.

Profesa Kamuzora akiongea na watumishi hao kutoka Idara, Taasisi, Serikali za Mitaa na Serikali Kuu aliwakumbusha wajibu wao wa  kuwahudumia wananchi kwa kutumia muda mfupi sana lakini kutekeleza majukumu au shughuli nyingi za kuwaletea wananchi hao maendeleo.

“Sote tunajua kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imefanya uhakiki na kuwaondoa watumishi ambao walikuwa hawastahili kuwa watumishi wa umama na sisi tuliobaki tunatakiwa kuufurahia utumishi wa wetu kwani sasa Serikali imeanza kurekebisha maslahi yetu kwa kupandisha vyeo na kurekebisha miundo ili kila mtumishi apate anachostahili kulingana na miundo ya utumishi wa umma iliyopo.” Alisisitiza Profesa Kamuzora.

Kwa upande mwingine Profesa Kamuzora alitoa rai kwa Watumishi wa Umma mkoani Kagera kuhakikisha wanatumia fursa za uwepo wa Hifadhi za Taifa za Chato - Burigi, Ibanda na Rumanyika kuzitembelea hifadhi hizo ili kupumzisha akili lakini pia kuangalia fursa ambazo zinaweza kuingiza kipato kwao kuzichangamkia ili kujiongezea kipato kuliko kuacha na fursa hizo zinachukuliwa na watu toka nje ya mkoa wakati zipo wazi kwa kila mmoja.

Fursa ya pili alioingelea kwa watumishi Profesa Kamuzora ni kuhusu Bomba la mafuta kutoka Ohima nchini Uganda kwenda mkoani Tanga litakaloingilia  Mkoani Kagera kuhakikisha kila mtumishi anatimiza wajibu wake na kufanya kila liwezekanalo katika nafasi yake kutokwamisha bomba hilo kuanza kufanya kazi kama inavyotarajiwa kufanyika.

Tatu Profesa Kamuzora aliwakumbusha watumishi wa umma kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu 2019 lakini watumishi hao wanatakiwa kuzingatia kanuni na taratibu za utumishi wa Umma ambazo zinaelekeza namna mtumishi anavyoweza kushiriki katika Uchaguzi bila kuvunja sheria zilizowekwa.

Aidha, Profesa Kamuzora aliwataka viongozi wa taasisi, na mbalimbali za Serikali kuhakikisha wanatoa motisha kwa watumishi walio chini yao ili kuwatia moyo na morali wa kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi mahala pa kazi na kufikia lengo la Serikali ya Awamu ya Tano la kuufikia Uchumi wa Kati.

Profesa Kamuzora aliendelea kusisitiza watumishi wa Umma wa Mkoa wa Kagera kuongeza jitihada za kutoa elimu ya lishe kwa wananchi kwani mkoa pamoja na kuwa na vyakula vingi lakini tatizo la udumavu bado lipo juu. Tatizo si vyakula bali elimu kwa wananchi kujua namna bora ya kula au kutumia vyakula vya aina mbalimbali walivyonavyo.

“Unaweza kuona kuwa kuna shida katika hili na sitaki kuamnini au kulilinganisha hili la udumavu na ninacotaka kukisema , juzi nilikwenda Mkoani Ruvuma kuona timu yetu ya Mkoa ya UMISETA inavyoshiriki mashindano lakini namba walioshika vijana wetu inaedana na namba ya udumavu katika mkoa wetu, sasa sisi kama watumishi wa umma tunalo jambo lakufanya inamaana kwenye ligi ya maendeleo kuna sehemu hatutimizi majukumu yetu ipasavyo.” Alikazia Profesa Kamuzora  

Naye Bw. Abbas Marikela Mkuu wa Hazina Ndogo Mkoani Kagera akitoa maoni yake katika kuhitimisha Wiki ya Utumishi wa Umma alitoa wito kwa Maafisa Utumishi katika Idara na Taasisi mbalimbali za Serikali kutunza nyaraka za watumishi hasa wastaafu kwani wanapata shida sana wanapokutana na malezo tofauti na nyaraka zao walizonazo.

Bw. Abbas alitoa mfano kuwa watumishi wastaafu wengi unakuta hawapo katika masharti ya kudumu ya utumishi wa umma lakini wanakuwa hawajui na Maafisa Utumishi wao hawawaelezi jambo ambalo huleta usumbufu kwa mstaafu mwenyewe lakini pia na ofisi za hazina za mkoa kumbe kama Afisa Utumishi kama angetekeleza wajibu wake tatizo hilo lisingejitokeza.  

Mwisho katika kuhitimisha Wiki ya Utumishi wa Umma Mkoani Kagera iliyoanza Juni 19 hdai 25, 2019 watumishi wa umma walikumbushwa na kushuriwa kula vizuri, kupumzika kwa mda mrefu na kuomba ushari pale wanapokwazika au kukumbwa na matatizo kuliko kukaa kimya  kuwa ni tiba kwa kiwango kikubwa  kwa afya zao bila kusahau kufanya mazoezi ya mara kwa mara kuiweka miili yao imara.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa