• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Rais John Magufuli Akikagua Shehena ya Sukari Katika Kiwanda cha Kagera Sugar Missenyi Mkoani Kagera

Imewekwa : November 9th, 2017

Rais Magufuli Ardhishwa na Uwekezaji wa Kiwanda Cha Kagera Sukari Asema Serikali Itaendelea Kukiunga Mkono

Rais Magufuli akiendelea na ziara yake  Mkoani Kagera leo Novemba 8, 2017 katika siku ya tatu alitembelea Kiwanda cha Kagera Sukari kilichopo Wilayani Missenyi ambapo amempongeza mwekezaji wa kiwanda hicho Bw. Seif Seif  kwa kuwekeza mtaji mkubwa katika kiwanda hicho.

Akiwa katika kiwanda hicho Rais Magufuli alitembelea mashamba ya kiwanda na kujionea jinsi mashamba yanavyoandaliwa kisasa kwa kutumia teknolojia ya hali ya juu katika umwagiliaji na jinsi sukari inavyozalishwa aidha na kujionea shehena ya sukari ambayo tayari imezalishwa  tayari kuingizwa sokoni.

Aidha Rais Magufuli alipongeza uongozi wa kiwanda hicho kwa kutoa kipaumbele katika ajira kwa Watanzania wazalendo waliohitimu masomo yao katika Vyuo Vikuu vya hapa nchini na kuwaendeleza kielimu katika nchi za nje mara baada ya kuajiriwa katika kiwanda cha Kagera Sukari ili kupata ujuzi wa kilimo cha miwa ambapo hadi sasa kiwanda hicho kimeajiri wafanyakazi 5,000.

Hadi sasa Kiwanda cha Kagera Sukari kinazalisha tani 65,000 hadi tani 67,000 kwa mwaka ambapo Rais Magufuli alitoa maelekezo kiwanda hicho kizalishe tani 75,000 kufikia mwaka kesho 2018 na kuwahakikishia wenye viwanda vya sukari nchini kuwa soko la sukari lipo kubwa kwahiyo wanatakiwa kuzalisha zaidi.

“Kiwanda cha Mtibwa kinzalisha tani 30,000 TPC tani 100,000 Kilombero tani 109,000 Manyara tani 6,000 ukiunganisha na tani za Kagera Sukari kwaujumla  tani zinazozalishwa nchini ni 320,000 wakati mahitaji tani 450,000 na upungufu ni tani 130,000. Ukiangalia wingi wa watu Afrika Mashariki ni milioni 165 na nchi za SADC ni milioni 400 hilo ni soko kubwa la sukari,” Alibainisha Rais Magufuli.

Rais Magufuli aliwataka wenye viwanda kumhakikishia kuwa wanao uwezo wa kuzalisha sukari kwa kiwango chote cha mahitaji tani 450,000 ili Serikali ipige marufuku uingizwaji wa sukaria nchini ambapo alisema kuwa sukari hiyo inayoingizwa nchini wakati mwingine ni ya viwandani na wafanyabiashara waroho wanaiuza kama sukari ya matumiazi ya binadamu.

“Nawataka mnihakikishie kuwa mna uwezo wa kuzalisha sukari tani 450,000 na wakati mnapofunga viwanda kama kutakuwepo na upungufu nyie wenyewe muagize sukari toka nje hapo nitakuwa tayari kufuta uingizwaji Sukari nchini. Lakini sharti ni kwamba sukari toka nje muiagize nyinyi wenye viwanda na siyo kuwapa vibali wafanyabaiashara,” Alisistiza Rais Magufuli.

Aidha Rais Magufuli aliwaagiza Mawaziri wa Kilimo, Waziri wa Viwanda Biashara na Uwekezaji kufanya upembuzi yakinifu katika viwanda vyote vinavyotumia sukari ili kujua matumizi halisi katika viwanda vyao na atakeyebainika anaagiza sukari ya viwandani zaidi ya matumizi yake afikishwe mahakamani kwa hatua za kisheria

Aidha Bw. Seif Seif kwaniaba ya Bodi ya Wakurugenzi wa Kiwanda cha Kagera Sukari na wafanyakazi wa Kiwanda hicho aliishukuru Serikali ya Rais magufuli kwa kuwapa ushirikiano katika kuendesha kilimo na kuzalisha sukari.

Aidha rais Magufuli alimwagiza Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano kuhakikisha wakandarasi wanakuwepo katika eneo linapotakiwa kujengwa daraja katika mto Kagera litakalozinganisha Wilaya za Karagwe na Missenyi ili kurahisisha usafirishaji wa miwa kutoka katika Wilaya ya Karagwe kuja kiwandani.

Raisi Magufuli alimalizia hotuba yake kwa wananchi na wafanyakazi wa Kiwanda cha Kagera Sukari kwa kuwaomba wawekezaji kuwekeza katika Mkoa wa Kagera na ili uwe Mkoa wa uwekezaji ambapo aliwataka Kagera Sukari kuanziasha Kiwanda kingine cha Kutengeneza pombe kali kutokana na morasisi na wananchi kuanzisha viwanda vidogovidogo kama vya senene na vinginevyo.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa