• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

RC Gaguti Awataka Mawakili wa Kujitegemea Kuwa Wakweli Kwa Wateja Wao na Wananchi Kagera Wayaamini Maamuzi ya Mahakama

Imewekwa : February 1st, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti azindua rasmi maadhimisho ya Wiki ya Sheria nchini Mkoani Kagera kwa kupokea maandamano ya wadau mbalimbali wa Sheria wakiongozwa na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Bukoba  Mhe. Lucia Gamuya Kairo.

Katika hotuba yake ya uzinduzi Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa kilio chake kwa Mawakili hasa wale wa kujitegemea kuwa wakweli na kumtanguliza Mungu katika kutekeleza majukumu yao ya huduma kwa wananchi katika masuala ya kisheria.

“Kwa moyo wa dhati kabisa niwaombe Mawakili hasa wa kujitegemea muwe wakweli kwa wateja wenu, mwananchi anapokuja kwako na hoja yake msikilize kwa umakini ukiona hoja yake haina mashiko mbele ya sheria mwambie ukweli  kuwa hata akienda Mahakamani hawezi kushinda kesi hiyo kuliko kumdanganya na kupoteza muda na fedha zake Mahakamani. “ Alisisitiza Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Pia Mkuu wa Mkoa gaguti aliwataka Mawakili hao kumtanguliza Mungu katika kazi zao ili wanapokuwa wanatoa msaada wa kisheria kwa wananchi wasiongozwe na tama za kibinadamu ili wateja wanaowatetea washinde mashauri yao kwa haki bila dhuruma au kupindisha haki.

Kwa upande wa wananchi Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa rai kwao hasa katika Mkoa wa Kagera kuwa nao wanapaswa kuridhika na maamuzi ya Makama pale yanapotolewa. “Unakuta kesi ilishaamuliwa mpaka Mahakama ya Rufani lakini mwananchi haridhiki akiona huko hakushinda anakuja kwa Mkuu wa Mkoa au Mkuu wa Wilaya kushinikiza kufuta hukumu jambo ambalo si sawa.”  Alisema Mhe. Gaguti.

Katika hatua nyingine Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Bukoba  Mhe. Lucia Gamuya Kairo alisema kuwa katika Maadhimisho ya Wiki ya Sheria Mahakama itatembelea maeneo mbalimbali  mkoani Kagera kutoa msaada wa kisheria  kwa wananchi na maeneo hayo ni Magereza, Shule mbalimbali za Sekondari, na maeneo ya wazi kama soko kuu na kituo kikuu cha Mabasi Bukoba.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa Gaguti alivitaka Vyombo vya Habari Mkoani Kagera hasa Redio za Kijamii kuitumia Wiki ya Sheria nchini iliyozinduliwa rasmi Mkoani Kagera  Februari 1, 2020 kurusha vipindi mubshara kutoka katika maeneo mbalimbali wadau wa Sheria watakakokuwa wanatoa misaada ya kisheria ili kutoa elimu kwa wananchi  walioko manyumbani.

Mwisho Mkuu wa Mkoa Gaguti akizungumzia Kaulimbiu ya Mwaka huu 2020 isemayo “Uwekezaji na Biashara: Wajibu wa Mahakama na Wadau kuweka Mazingira Wezeshi ya Uwekezaji.”  Aliwasisitiza wadau wote wa uwekezaji wanaopenda kuja kuwekeza katika mkoa wa Kagera kuhakikisha wanafuata na kukamilisha taratibu zote za kisheria ili kuepuka migogoro isiyokuwa ya lazima hapo mbeleni.

Maadhimisho ya Wiki ya Sheria  imezinduliwa leo Februari  1, 2020 na kilele chake kitakuwa tarehe 6/02/2020. Ikumbukwe kuwa mkoa wa Kagera unahitaji watendaji wa kutosha katika masuala ya kisheria kutokana na wingi watu. Kagera ni mkoa wa tatu kwa  wingi wa watu ukiacha mikoa ya Dar es Saalam  na Mwanza kwa takwimu za mwaka 2019 ambazo zimetolewa hivi karibuni, Kagera kuna jumla ya watu 3,127,908 ukilinganisha na takwimu za mwaka 2012 watu 2,458,023.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa