• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Uwekezaji

UWEKEZAJI KATIKA MKOA WA KAGERA

Mkoa wa Kagera umekuwa na mikakati mbalimbali ya kuvutia wawekazaji kwa kushirikisha wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na Halmashauri za Wilaya. Mkoa umekuwa na wawekezaji mbalimbali wa ndani na nje ya nchi ingawaje uwekezaji huu unaendelea kufanyika kwa kiwango kidogo cha asilimia 5% hadi mwaka 2014

Dhana ya wananchi wengi katika uwekezaji hufikiria zaidi uwekezaji kutoka nje ya nchi badala ya wananchi wenyewe na pia hufikiria uwekezaji hufanywa na Serikali pekee. Ni wazi kuwa uwekezaji hauwezi kuendeshwa na uchumi wa Serikali na wala hakuna uchumi wa nchi yoyote unaoweza kukua kwa kutegemea uwekezaji wa umma bila kushirikisha wawekezaji binafsi. Sekta zote mbili zinabidi zishirikiane kwa pamoja kwa manufaa ya jamii.

MAENEO YA UWEKEZAJI

Wilaya zimeainisha maeneo takribani hekta 28,783 kwa ajili ya uwekezaji katika kilimo cha umwagiliaji na ujenzi wa viwanda vya kusindika mazao ya kilimo (Agro Processing Industries) ili kuongeza thamani ya mazao pamoja na uwekezaji wa biashara ndogo. Mengi ya maeneo haya bado hayajapimwa na kumilikiwa na Halmashauri zenyewe.

Fursa za Uwekezaji

Mkoa wa Kagera unazo fursa nyingi na muhimu kwa ajili ya kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Uwekezaji unaweza kufanywa katika sekta za kilimo, viwanda, utalii, uvuvi, ufugaji na maliasili. Mkoa unayo maeneo mengi ya uwekezaji kama yalivyoainishwa hapo juu, hali ya hewa nzuri pamoja na fursa ya kijiografia ya Mkoa wa Kagera kupakana na nchi za Jumuiya ya Af rika Mashariki (Rwanda, Burundi na Uganda). Hata hivyo fursa hizo bado hazijatumika ipasavyo kutokana na hali ya uwekezaji Mkoani kuwa bado katika kiwango cha chini. Mkoa wa Kagera ni miongoni mwa mikoa 10 ya Tanzania bara ambayo uwekezaji wake uko chini ya asilimia moja (1%).

• Kutokana na uzalishaji mkubwa wa ndizi kiasi cha wastani wa tani milioni 1.4 kwa mwaka, tani 15,000 za mpunga, tani 250,000 za mahindi, tani 106,000 za maharage na tani 830,000 za mihongo; ipo fursa kubwa ya kuanzisha viwanda vya usindikaji na uongezaji thamani mazao haya ya kilimo.

• Mkoa unayo fursa ya kuanzisha mashamba makubwa ya mahindi na mpunga katika bonde la mto Nkenge na Mto ngono wilayani Missenyi kwa ajili ya uzalishaji utakaokidhi mahitaji makubwa ya chakula katika soko la Afrika Mashariki na Kati.

• Mkoa unayo fursa ya uwekezaji katika unenepeshaji wa mifugo kama ng'ombe, mbuzi na kondoo kutokana na maeneo ya malisho yaliyopo katika huria (ranches) za Kikulula, Missenyi,      Kagoma, Mabale na Kitengule zenye ukubwa wa jumla ya Hekta 136,028.

• Uwekezaji katika viwanda vya kusindika nyama, ng'ozi na bidhaa zake kutokana na uwepo wa idadi kubwa ya mifugo; ng'ombe 520,000, mbuzi 580,000, kondoo katika wilaya za Ngara, Bukoba, Karagwe, Biharamulo, Muleba na Missenyi.

• Fursa ya uwekezaji katika ujenzi wa viwanda vya kusindika asali, uongezaji thamani asali na a mazao yake pamoja na viwanda vya kutengeneza vipodozi na madawa kutokana na matumizi ya asali.

• Uwekezaji katika ujenzi wa hoteli za kitalii, camping sites, kumbi za mikutano, na vivutio mbalimbali vya utalii.

• Kwa kuwa Mkoa umepataka na nchi za Uganda, Rwanda, Burundi na Kenya kwa upande wa ziwa Victoria kuna fursa ya ujenzi wa Vituo vya kubadirishia fedha (Beural De Change) kwa kuwa hadi 2014 hakuna kituo rasmi kilichoanzishwa.

• Uwekezaji katika sekta ya usafiri na usafirishaji kwa njia ya maji na ujenzi wa bandari ya kisasa katika visiwa vya Bumbile and Karebe Bukoba, Muleba na Missenyi.

• Uwekezaji katika ujenzi wa nyumba za kuishi za kisasa na majengo ya kibiashara katika maeneo ya Bukoba Manispaa, Missenyi (Mutukula) na Muleba kutokana na viwanja vipatavyo 7,000 vilivyopo ambavyo vimepimwa katika maeneo hayo.

Maeneo ya uwekezaji

Mkoa kwa kushirikiana na Mamlaka za Serikali za Mitaa zimeainisha na kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya uwekezaji yenye ukubwa wa hekta 16,000.

Bonyeza hapa upate maeneo ya uwekezaji mkoani Kagera

UWEKEZAJI KISEKTA

Mkoa wa Kagera una Viwanda vikubwa saba (7) ambavyo ni Bukop Ltd, TANICA, Kagera Tea Company, Kagera Sugar Company, Amir Hamza (T) Ltd, Kagera Fish Company na Vic Fish Company. Kutokana na serikali kubinafsisha Viwanda viwili vya Kagera Sukari na Kiwanda cha Chai cha Maruku vimendelea kufanya vizuri katika uzalishaji na kuchangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa uchumi wa Mkoa na kuongeza ajira. Pamoja na viwanda hivyo vikubwa kuna viwanda vidogo mfumo wa SIDO vipatavyo 6,844 ambavyo vimeajili zaidi ya watu 80,000.

Uwekezaji katika usafirishaji

Wadau wa maendeleo wamewekeza katika huduma za usafiri na usafirishaji kama ifuatavyo:

• Usafiri wa anga: Precissionair, Auric Air

• Usafiri wa majini: Marine Services Co. Ltd

• Usafiri wa Barabara: Magari ya abiria na mizigo

Uwekezaji katika mawasiliano: Mawasiliano haya ni pamoja na:

• Mawasiliano ya simu: TTCL, Vodacom, Tigo, Airtel na Zental.

• Mawasiliano ya Radio: Redio Tanzania, Radio Free Africa, Kasibante, Radio Vision, Radio Kwizela, Radio Karagwe na FADECO.

• Mawasiliano ya TV (Luninga): TBC, ITV na Chaneel Ten.

• Mawasiliano ya Mtandao (Internet providers):Yanapatikana katika kila Wilaya kupitia kampuni za Simbanet, TTCL, Vodacom,Tigo na Airtel.

ix) Uwekezaji katika mazao mbadala: Uwekezaji katika kilimo cha maua ni moja ya sekta muhimu kwa maendeleo ya taifa kutokana na kuchangia katika pato la taifa ikiwa ni pamoja na kutoa ajira kwa watu wengi.

Pamoja na uwekezaji huu, bado Mkoa unahamasisha uwekezaji katika maeneo kama vile Kilimo cha kibiashara, ujenzi wa viwanda vya kusindika mazao, huduma za kijamii zikiwemo ujenzi wa shule za sekondari na vyuo vya elimu ya juu na ufundi, zahanati na Hospitali na uzalishaji umeme.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa