• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government KAGERA REGIONAL WEBSITE

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections/Units
      • Sections
        • Management Monitoring and Ispection
        • Infrastructure
        • Education
          • Primary Education
          • Secondary Education
          • Adult Education
          • Higher Education
          • Sports
          • Youth
        • Health
          • Health
          • social welfare
        • Administration And HR
        • Planning & Coordination
          • Planning
          • Statistics
          • Community Development
          • TASAF
        • Economic and Production
          • Irrigation Farming
          • Commerce and Industries
          • Fishing
          • Livestock
          • Natural Resources, Tourism & Environment
          • Co operative
          • Agriculture
        • Investment Indusrty and Trade
      • Units
        • ICT
        • Legal Unit
        • Finance and Accounts
        • Internal Audit Unit
        • Procurement Unit
        • Government Communication
  • Districts
    • Bukoba
      • Bukoba Leaders
    • Biharamulo
      • Biharamulo Leaders
    • Karagwe
      • Karagwe Leaders
    • Kyerwa
      • Kyerwa Leaders
    • Missenyi
      • Missenyi Leaders
    • Muleba
      • Muleba Leaders
    • Ngara
      • Ngara Leaders
  • District Councils
    • Bukoba Municipal Council
    • Bukoba District Council
    • Biharamulo District Council
    • Karagwe District Council
    • Kyerwa District Council
    • Missenyi District Council
    • Muleba District Council
    • Ngara District Council
  • Investment Opportunities
    • Tourism Attractions
    • Farming Opportunities
    • Agricultural Opportunities
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • Water Services
    • Agricultural Services
    • Farming Services
  • Publications
    • By Laws
    • Client Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • News Letter
  • Media Center
    • Videos
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Huduma za Madaktari Bingwa Mkoani Kagera Tayari Zawafikia Wananchi 429 Siku ya Kwanza na Wengi Bado Wafurika Kupata Matibabu

Posted on: November 6th, 2018

Huduma za Madaktari Bingwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera zawafanya wananchi wengi wenye matatizo ya kiafya kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Kagera kufurika katika Hospitali hiyo ili kupata huduma za Kibingwakutoka kw Madaktari Bingwa.

Katika uzinduzi rasmi wa utoaji wa huduma hizo za Kibingwa Novemba 6, 2018 Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera Dk. Felix I. Otieno alitoa taarifa kwa Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhandisi Richard Luyango ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Muleba kuwa tangua zoezi lianze Novemba 5, 2018 siku ya Jumatatu tayari wagonjwa 858 walikuwa wamejiandikisha kuwaona Madaktari Bingwa wa magonjwa mbalimbali.

Aidha, Dk. Felix alisema kuwa tayari Madaktari Bingwa 27 walikuwa wamewasili katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera kwaajili ya kutoa huduma za kibingwa  na siku ya kwanza ya Jumatatu Novemba 5, 2018  wagonjwa 429 walikuwa wamepatiwa huduma za Kibingwa katika vitengo vya kuhudumia magonjwa mbalimbali katika Hospitali hiyo ikiwa ni pamoja na kuwaadaa baadhi ya wagonjwa kwajili ya upasuaji.

Akizindua rasmi zoezi la kutoa huduma za Kibingwa Katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhandisi Richard Luyango ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhandisi Richard Luyango aliwashukuru Madaktari bingwa 27 ambao tayari wamewasili katika Hospitali hiyo na kuanza kutoa huduma za Kibingwa na kusema kuwa huo ni uzalendo mkubwa waliuonesha wa kuwahudumia wananchi wa Kagera.

“Nawapongeza sana Madaktari Bingwa ambao mmefika hapa kuwahudumia wananchi wetu mmekuwa wazalendo kweli kweli kama mnavyowaona wananchi wetu hapa kuwa wanahitaji huduma zenu kwasababu ya matatizo ya kiafya waliyonayo. Wito wangu kwenu ninyi Madaktari Bingwa niwaombe muongeze siku mbili zaidi katika kutoa huduma kwani siku sita (tarehe 5 hadi 11 Novemba, 2018) hazitatosha ukiangalia wananchi waliohudhuria hapa.”  Alisisitiza Mhandisi Luyango.

Pia Mhandisi Luyango aliwaomba wananchi ambao ni wagonjwa waliohudhuria katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera kupata huduma za Kibingwa kuwa wavumilivu katika kupata huduma hizo kutokana na wingi wao na pia walitakiwa kusikiliza maelekezo wanayopewa na Wataalamu wa Afya ili kuwafikia Madaktari Bingwa kwajaili ya kupatiwa huduma.

Naye Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Bw. Projectus Rutabanzibwa aliwataka watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera kuhakikisha wanatoa ushirikiano wa kutosha katika kutoa huduma kwenye zoezi hilo na kusisitiza kuwa Serikali imetoa fedha nyingi kugharamia zoezi hilo kwa ajili ya kutoa Huduma za kibingwa kwa Wananchi wa Mkoa wa Kagera.

Kwa upande mwingine Daktari Bingwa Kiongozi wa timu ya Madaktari Bingwa wanaotao huduma za Kibingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera Dk. Samwel Rweyemamu ambaye ni Daktari Bingwa wa magonjwa ya moyo alisema timu yao ya Madaktari Bingwa inaendele vizuri na utoaji wa huduma kwa wananchi wa Mkoa wa Kagera.

Dk. Rweyemamu alisema kuwa kwa upande wa magonjwa ya moyo siku ya kwanza Jumatatu Novemba 5, 2018 walikuwa wamehudumia wagonjwa watu wazima 60 lakini siku ya pili ya Jumanne Novemba 6, 2018 huduma za Kibingwa kwa upande wa magonjwa ya moyo zilikuwa zikitolewa kwa watoto ambao nao ni wengi. Aidha, Dk. Rweyemamu alisema tayari wagojwa 10 walikuwa wameshauriwa kwenda katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kutokana na matatizo yao kuwa makubwa zaidi.

Nao wananchi ambao wamefurika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera walikiri mbele ya Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa Mhandisi Richard Luyango ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Muleba kuwa wanaishukuru Serikali kwa kuwasogezea huduma za Kibingwa karibu. Pia krahisisha namna ya kuwaona Madaktari Bingwa ukilinganisha na kuwafuata katika vituo vyao vya kazi pamoja na gharama za malazi na chakula.

Katika kutekeleza zoezi hilo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera ikishirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera wamejipanga vizuri kuhakikisha huduma za Kibingwa zinatolewa kwa uhakika ambapo wananchi wenye kadi za Bima Hawatozwi chochote bali wanalipia gharama zao kupitia kadi hizo lakini mfumo wa kukusanyia mapato unatumika kuhakikisha fedha ya Serikali inakusanywa kwa usahihi ili kukuza mapato ya Hospitali hiyo.

Ikiwa ni mara ya pili zoezi la huduma za Madaktari Bingwa kutolewa Mkoani Kagera mwaka 2017 jumla ya wagonjwa 3,146 walihudumiwa na mwaka huu 2018 huduma hizi zinalenga kuwahudumia wagonjwa 4,000 hadi 5,000 kwa magonjwa ya Uzazi na kizazi kwa wanawake, Magonjwa ya upasuaji kwa Ujumla, Magonjwa ya njia ya mikojo ikiwemo tezi Dume, Magonjwa ya pua, sikio na koromeo.

Magonjwa mengine yatakayoshughulikiwa na Madaktari Bingwa ni pamoja na Magonjwa ya mifupa, Magonjwa ya moyo, Magonjwa ya ndani ikiwemo sukari na figo, Magonjwa ya watoto, Magonjwa ya Afya ya kinywa na meno, Magonjwa ya macho, Magonjwa ya Ngozi, Magonjwa ya afya ya akili, na Saratani ya Mlango wa kizazi.

 

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • View All

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
More Videos

Quick Links

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Radio Stations in Kagera Region
  • Kagera Regional Commissioners Since Independence 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • National Bureau of Statistics (NBS)
  • Government of Tanzania Website
  • Open Data Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Postal Address: S.L.P 299 BUKOBA

    Telephone: 255 28 2220215/17

    Mobile:

    Email: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Hakimiliki

Copyright ©2017 GWF . All rights reserved.