• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government KAGERA REGIONAL WEBSITE

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections/Units
      • Sections
        • Management Monitoring and Ispection
        • Infrastructure
        • Education
          • Primary Education
          • Secondary Education
          • Adult Education
          • Higher Education
          • Sports
          • Youth
        • Health
          • Health
          • social welfare
        • Administration And HR
        • Planning & Coordination
          • Planning
          • Statistics
          • Community Development
          • TASAF
        • Economic and Production
          • Irrigation Farming
          • Commerce and Industries
          • Fishing
          • Livestock
          • Natural Resources, Tourism & Environment
          • Co operative
          • Agriculture
        • Investment Indusrty and Trade
      • Units
        • ICT
        • Legal Unit
        • Finance and Accounts
        • Internal Audit Unit
        • Procurement Unit
        • Government Communication
  • Districts
    • Bukoba
      • Bukoba Leaders
    • Biharamulo
      • Biharamulo Leaders
    • Karagwe
      • Karagwe Leaders
    • Kyerwa
      • Kyerwa Leaders
    • Missenyi
      • Missenyi Leaders
    • Muleba
      • Muleba Leaders
    • Ngara
      • Ngara Leaders
  • District Councils
    • Bukoba Municipal Council
    • Bukoba District Council
    • Biharamulo District Council
    • Karagwe District Council
    • Kyerwa District Council
    • Missenyi District Council
    • Muleba District Council
    • Ngara District Council
  • Investment Opportunities
    • Tourism Attractions
    • Farming Opportunities
    • Agricultural Opportunities
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • Water Services
    • Agricultural Services
    • Farming Services
  • Publications
    • By Laws
    • Client Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • News Letter
  • Media Center
    • Videos
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Kama Una Wazo la Kukigawa Chama Kikuu Cha Ushirika KDCU LTD ni Bora Uhame Mkoa wa Kagera Sipo Tayari Kuona Hilo Linatokea – RC Gaguti

Posted on: March 5th, 2019

“Kama kuna mwananchi, kundi la watu, baadhi ya wanachama wa Vyama vya Ushirika au kiongozi yeyote ana wazo la kukigawa Chama Kikuu cha Ushirika cha Wilaya ya Karagwe na Kyerwa Development Co-operative Union Limited (KDCU LTD) ahame mara moja Mkoa wa Kagera au akafanye hivyo nje ya mkoa huu lakini sipo tayari kuona jambo hilo linatokea.” Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti akitoa onyo katika Mkutano Mkuu wa 32 wa KDCU LTD Kayanga Wilayani Karagwe.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa onyo hilo Machi 5, 2019 Wilayani Karagwe kwenye Mkutano Mkuu wa 32 wa KDCU LTD katika ukumbi wa CCM akiwa mgeni rasmi wakati akiongea na wajumbe wa Mkutano huo ambapo alisema kuwa tayari ameanza kusikia fununu za baadhi ya watu kutaka kukigawa chama cha KDCU LTD katika vyama viwili ambavyo vitawakilisha Wilaya za Karagwe na Kyerwa na kuonya kuwa jambo hilo haliwezi kutokea na halitakiwi kufikiriwa wala kujadiliwa.

Pia Mkuu wa Mkoa Gaguti alisistiza kuwa kwasasa anatamani Mkoa wa Kagera ungekuwa na Chama Kikuu cha Ushirka kimoja chenye nguvu na kuwahudumia wakulima lakini si kuwa na Vyama vya Ushirika vingi ambavyo vitauingiza mkoa katika migogoro na haviwezi kuwasaidia wakulima kuendeleza kilimo cha kahawa lakini pia kuwanufaisha wakulima na zao la kahawa ambalo linatakiwa kuwainua kiuchumi wananchi  wa Kagera.

“Serikali itaendelea kuweka misingi na mikakati iliyo imara ili kuhakikisha kahawa inapata bei bora na fedha za wakulima kupatikana mapema ili mkulima asihangaike wakati tayari amekusanya kahawa yake katika Chama cha Msingi. Pia Serikali ingependa kuona zao la kahawa linaboreshwa zaidi na kuongeza uzalishaji mkoani Kagera kutoka uzalishaji wa sasa wa kilo milioni 58.9 hadi kilo milioni 100”. Alisistiza Mkuu wa Mkoa Gaguti

Katika hatua nyingine Mbunge wa Kyerwa Innocent Bilakwate akiongea na wajumbe wa Mkutano huo aliwaonya vionozi wa KDCU LTD kuhakikisha wanafanya ukaguzi wa fedha za wakulima katika Vyama vya Msingi vya chama kikuu hicho kwani ambapo alisema alisema kuwa kwa utafiti wake baadhi ya viongozi wa vyama hivyo wamehujumu au kutumia vibaya fedha za wakulima katika maeneo yao.

Jambo hilo lilimfanya Mkuu wa Mkoa Gaguti kuagiza Vyama vya Msingi vya  Nyakatuntu, Kaina, na Kamuli kukamatwa mara moja na kuchukuliwa hatua za kisheria kwa ubadhilifu wa fedha za wakulima na ifikapo Machi 6, 2019 saa 3:00 asubuhi awe amepata taarifa ni hatua gani zimechukuliwa kwa viongozi hao na kutoa rai kwa baadhi ya viongozi ambao wamejipanga kuhujumu mfumo wa ushirika kuwa Serikali itachukua hatua kali sana dhidi yao.

Katika msimu huu wa mwaka 2018/19 ulioanza mwezi Mei Mosi 2018 na utakamilika Aprili 30, 2019 Mkoa wa Kagera umekusanya na kuuza  jumla ya kilo milioni 58.9 za kahawa na Chama Kikuu cha  KDCU LTD kimekusanya asilimia 67%  kahawa zote. Chama cha KDCU LTD kilikuwa kimeotea kukusanya tani elfu 40 na kufanikiwa kukusanya tani elfu 39 sawa na asilimia 98% na tayari chama hicho kimepata faida ya shilingi milioni 260.

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • View All

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
More Videos

Quick Links

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Radio Stations in Kagera Region
  • Kagera Regional Commissioners Since Independence 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • National Bureau of Statistics (NBS)
  • Government of Tanzania Website
  • Open Data Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Postal Address: S.L.P 299 BUKOBA

    Telephone: 255 28 2220215/17

    Mobile:

    Email: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Hakimiliki

Copyright ©2017 GWF . All rights reserved.