• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government KAGERA REGIONAL WEBSITE

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections/Units
      • Sections
        • Management Monitoring and Ispection
        • Infrastructure
        • Education
          • Primary Education
          • Secondary Education
          • Adult Education
          • Higher Education
          • Sports
          • Youth
        • Health
          • Health
          • social welfare
        • Administration And HR
        • Planning & Coordination
          • Planning
          • Statistics
          • Community Development
          • TASAF
        • Economic and Production
          • Irrigation Farming
          • Commerce and Industries
          • Fishing
          • Livestock
          • Natural Resources, Tourism & Environment
          • Co operative
          • Agriculture
        • Investment Indusrty and Trade
      • Units
        • ICT
        • Legal Unit
        • Finance and Accounts
        • Internal Audit Unit
        • Procurement Unit
        • Government Communication
  • Districts
    • Bukoba
      • Bukoba Leaders
    • Biharamulo
      • Biharamulo Leaders
    • Karagwe
      • Karagwe Leaders
    • Kyerwa
      • Kyerwa Leaders
    • Missenyi
      • Missenyi Leaders
    • Muleba
      • Muleba Leaders
    • Ngara
      • Ngara Leaders
  • District Councils
    • Bukoba Municipal Council
    • Bukoba District Council
    • Biharamulo District Council
    • Karagwe District Council
    • Kyerwa District Council
    • Missenyi District Council
    • Muleba District Council
    • Ngara District Council
  • Investment Opportunities
    • Tourism Attractions
    • Farming Opportunities
    • Agricultural Opportunities
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • Water Services
    • Agricultural Services
    • Farming Services
  • Publications
    • By Laws
    • Client Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • News Letter
  • Media Center
    • Videos
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Mkuu wa Mkoa Atekeleza Agizo la Rais Magufuli la Kugawa Vitambulisho Kwa Wajasiliamali Wadogo Katika Mkoa wa Kagera

Posted on: December 20th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti atekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli la kugawa vitambulisho kwa Wajasiliamli Wadogo ili waweze kufanya shughuli zao za ujasiliamali na kujiingizia kipato chao cha kila siku bila kusumbuliwa na mtu yeyote.

Mkuu wa Mkoa Gaguti ametekeleza agizo hilo la Rais Magufuli Desemba 20, 2018 katika Uwanja wa Uhuru (Maarufu kama Mayunga) Manispaa ya Bukoba ambapo alivigawa vitambulisho hivyo kwa Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa Kagera na Halmashauri zake nane.

Kabla ya kugawa vitambulisho hivyo kwa Wakuu wa Wilaya na Baadhi ya wajasiliamali wachache wa Manispaa ya Bukoba Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa Mkoa wa Kagera ulipewa vitambulisho jumla 25,000 vilivyotolewa na Rais Magufuli na kusisitiza  kuwa vitambulisho hivyo vikigawiwa na kuisha uongozi wa mko utaomba vingine zaidi ili kuhakikisha kila Mjasiliamali Mdogo anapata kitambulisho hicho.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa angalizo kuwa vitambulisho hivyo vinawalenga Wajailiamali au Wafanyabiashara Wadogo na  wanatakiwa kuwa walinzi wao wenyewe kujilinda ili waweze kujiingizia kipato chao bila kusumbuliwa lakini wasiwe mawakala wa wafanyabiashara wakubwa ili kuwafanyia biashara kwa kutumia vitambulisho hivyo.

“Rais Magufuli alitoa maelekezo kuwa hakuna Mjasiliamali yeyote ambaye atakuwa na kitambulisho na kusumbuliwa, pia na mimi Mkuu wa Mkoa wa Kagera narudia na kuagiza kuwa Mjasiliamali Mdogo yeyote ambaye atakuwa na kitambulisho na kusumbuliwa na mtu yeyote katika mipaka ya Mkoa wa Kagera.” Alisisitiza Mkuu wa Mkoa Gaguti

Aidha, Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwatahadharisha wafanyabiasha wadanganyifu kuwa tayari ofisi yake imepata taarifa kuwa kuna baadhi ya Wafanyabiashara wasio waaminifu kuwa wameanza kupunguza bidhaa kwenye chanja za maduka yao ili waweze kutambuliwa kama Wajasiliamali Wadogo wakilenga kupata vitambulisho. “Ukibainika umefanya mchezo huo hatua kali zitachukuliwa kwa kuzingatia sheria na katika zoezi hili Serikali itasimaia sheria ipasavyo.” Alitahadharisha Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Hatua zitakazochukuliwa ni pamoja na wafanyabiashara watakaogundulika kufanya mchezo wa udanganyifu ni pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzani kuwafutia moja kwa moja leseni za biashara. Aidha, Viongozi wa Serikali za Mitaa na Watendaji wa Kata walitakiwa kutenda haki katika utambuzi wa Wajasiliamali Wadogo katika maeneo yao. Pia wananchi walitakiwa kupaza sauti pale watakapoona zoezi hilo linaendeshwa bila kutenda haki.

Naye Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Kagera Bw. Adam Ntoga alitoa ufafanuzi wa ni Mjasiliamali yupi Mdogo anatakiwa kupata kitambulisho ambapo alisema kuwa ni Wajasiliamali wadogo ambao hawajawahi kutambuliwa na mfumo wa kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania na mzunguko wao wa fedha haufikii kiasi cha shilingi milioni nne. Pia Bw. Ntoga alisema kuwa malipo ya kitambulisho hicho ni shilingi 20,000/- tu.

Katika Mkoa wa Kagera Wilaya ya Bukoba ilipatiwa jumla ya vitambulisho 3,580 na Wilaya za Missenyi, Karagwe, Kyerwa, Ngara, Biharamulo na Muleba kila Wilaya kupitia Wakuu wa Wilaya zilipatiwa vitambulisho 3,570 na kukamilisha jumla ya Vitambulisho 25,000 vilivyotolewa katika Mkoa wa Kagera na Rais Magufuli Desemba 10, 2018

Ikumbukwe kuwa Desmba 10, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli  akiwa Ikulu Jijini Dar es Salaam alitoa vitambulisho vya wajasiliamali wadogo 670,000 kwa Wakuu wa Mikoa yote na kila Mkoa ulipatiwa vitambulisho 25,000 na Mkoa wa Kagera ukiwemo ambapo Rais Magufuli alisema kuwa kila Mkuu wa Mkoa atakusanya shilingi 500 milioni kupitia vitambulisho hivyo.

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • View All

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
More Videos

Quick Links

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Radio Stations in Kagera Region
  • Kagera Regional Commissioners Since Independence 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • National Bureau of Statistics (NBS)
  • Government of Tanzania Website
  • Open Data Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Postal Address: S.L.P 299 BUKOBA

    Telephone: 255 28 2220215/17

    Mobile:

    Email: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Hakimiliki

Copyright ©2017 GWF . All rights reserved.