• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government KAGERA REGIONAL WEBSITE

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections/Units
      • Sections
        • Management Monitoring and Ispection
        • Infrastructure
        • Education
          • Primary Education
          • Secondary Education
          • Adult Education
          • Higher Education
          • Sports
          • Youth
        • Health
          • Health
          • social welfare
        • Administration And HR
        • Planning & Coordination
          • Planning
          • Statistics
          • Community Development
          • TASAF
        • Economic and Production
          • Irrigation Farming
          • Commerce and Industries
          • Fishing
          • Livestock
          • Natural Resources, Tourism & Environment
          • Co operative
          • Agriculture
        • Investment Indusrty and Trade
      • Units
        • ICT
        • Legal Unit
        • Finance and Accounts
        • Internal Audit Unit
        • Procurement Unit
        • Government Communication
  • Districts
    • Bukoba
      • Bukoba Leaders
    • Biharamulo
      • Biharamulo Leaders
    • Karagwe
      • Karagwe Leaders
    • Kyerwa
      • Kyerwa Leaders
    • Missenyi
      • Missenyi Leaders
    • Muleba
      • Muleba Leaders
    • Ngara
      • Ngara Leaders
  • District Councils
    • Bukoba Municipal Council
    • Bukoba District Council
    • Biharamulo District Council
    • Karagwe District Council
    • Kyerwa District Council
    • Missenyi District Council
    • Muleba District Council
    • Ngara District Council
  • Investment Opportunities
    • Tourism Attractions
    • Farming Opportunities
    • Agricultural Opportunities
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • Water Services
    • Agricultural Services
    • Farming Services
  • Publications
    • By Laws
    • Client Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • News Letter
  • Media Center
    • Videos
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Profesa Kamuzora Afanya Ziara Visiwani Awaelimisha Wavuvi Kuzingatia Ubora Katika Uchakataji wa Mazao ya Samaki

Posted on: April 3rd, 2019

Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Profesa Faustin Kamuzora katika kusimamia maendeleo ya mkoa kupitia sera ya kila mwananchi kujikwamua kiuchumi kwa kuzalisha na kujiingizia kipato halali kupitia kazi anayoifanya atembelea na kukagua miradi ya maendeleo Visiwani Wilayani Muleba na kuongea na wavuvi kwa kuwaelimisha juu ya uvuvi wa kisasa wenye tija na kukuza uchumi.

Akifanya ziara ya siku mbili Machi 28 hadi 29, 2019 katika visiwa vinne vya Kimoyomoyo, Mulumo, Kassenyi, na Chakazimbwe katika Kata za Mazinga na Ikuza Prof. Kamuzora alikagua miradi ya maendeleo hasa ujenzi wa ghati katika visiwa hivyo na kushauri miradi hiyo isimamiwe vizuri na ujenzi uzingatie viwango vya ujenzi ili mara baada ya kukamilika ziweze kudumu zaidi ya miaka 100.

Pamoja na kutembelea na kukagua miradi ya maendeleo pia Prof. Kamuzora alimtembelea Bw. Issa Jiwa Mjasiliamali  anayechakata dagaa kwa kuowaongezea thamani na kuuza katika masoko ya ndani na nje ya nchi. Pia Prof. Kamuzora alijionea wavuvi wengine wanavyochakata mazao ya samaki hasa uanikaji wa dagaa.

Katika mikutano yake na wananchi waishio visiwani Prof. Kamuzora mara baada ya kutembelea na kukaua miradi ya maendeleo aliwaelimisha wananchi hao kuzingatia ubora wa mazoa wanayoyazalisha hasa ubora wa samaki au dagaa wanapochakatwa kabla ya kufikishwa sokoni.

Prof. Kamuzola alikaripia vikali wavuvi wanaoanika dagaa chini kuwa hairusiwi kufanya hivyo kwani dagaa wakianikwa chini kwenye mchanga ubora wake unapungua katika masoko ya ndani api masoko ya nje ya nchi. Dagaa hao huwa na mchanga jambo ambalo huleta usumbufu mkubwa kwa watumiaji.

“Hapa nchini Tanzania tuna tatizo kubwa la uharibifu baada ya mavuno (Post Harvest Loss) yaani unakuta mwananchi anahangaika kuzalisha bidhaa zake ili akauze sokoni lakini anashindwa kuziandaa bidhaa hizo katika hatua za mwisho wakati wakuzipeleka sokoni jambo ambalo linapelekea hasara kubwa kwa mhusika na wakati mwingine kusababisha madhara kwa watumiaji.” Alitahadharisha Prof. Kamzora

Prof. Kamzora aliwaagiza Maafisa Uvuvi na Maafisa Afya visiwani humo kuhakikisha wanatekeleza sheria ya uvuvi Namba 22 ya mwaka 2003 na kanuni zake za mwaka 2009 katika kusimamia masuala ya uvuvi na uchakataji wa mazao yake na kuchukua hatua kali kwa wale wote ambao wanaoendelea kukiuka sheria, taratibu na kanuni za uvuvi.

Pia Prof. Kamuzora akiongea na wananchi katika mikutano ya hadhara aliwaelimisha juu ya lishe hasa wazazi kuhakikisha wanapata elimu juu ya lishe ili kuondoa utapiamlo kwa watoto ambapo madhara ya utapiamlo ni makubwa katika makuzi ya watoto na madhara yake huonekana hata kama mtu akiwa mtu mzima.

Vilevile wananchi waishio visiwani walielimishwa kuhakikisha wanajiunga na bima ya afya iliyoboreshwa ili iweze kuwasaidia pale wanapokuwa wagonjwa au pale wanapokuwa wamepoteza uwezo wakufanya kazi kuvua samaki badala ya kurudishwa nyumbani nchi kavu badala yake wapatiwe matibabu au huduma ya afya hukohuko visiwani.

Katika hatua nyingine Prof. Kamuzora aliwapongeza wananchi katika visiwa alivyotembelea kwa kuchangia shilingi milioni 17 kwaajili ya ununuzi wa boti ya doria za ulinzi na kuwaomba kuendelea kuchangia ili boti hiyo yenye thamani ya jumla ya shilingi milioni 29 iweze kununuliwa na kuanza kazi mara moja kuondoa maharamia wanaowasumbua wavuvi katika shughuli zao.

Mwisho Prof. Kamzora aliwaasa wavuvi kuachana na uvuvi haramu au kutumia zana haramu katika kuvua ambapo alichoma nyavu haramu katika kisia cha Chakazimbwe. Pia aliwasisitiza wananchi kuendelea kushirikiana na Halmashaur ya Wilaya ya Muleba kutekeleza miradi ya maendeleo kama kujenga shule na zahanati ili wapate huduma nzuri za kijamii.

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • View All

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
More Videos

Quick Links

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Radio Stations in Kagera Region
  • Kagera Regional Commissioners Since Independence 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • National Bureau of Statistics (NBS)
  • Government of Tanzania Website
  • Open Data Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Postal Address: S.L.P 299 BUKOBA

    Telephone: 255 28 2220215/17

    Mobile:

    Email: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Hakimiliki

Copyright ©2017 GWF . All rights reserved.