• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government KAGERA REGIONAL WEBSITE

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections/Units
      • Sections
        • Management Monitoring and Ispection
        • Infrastructure
        • Education
          • Primary Education
          • Secondary Education
          • Adult Education
          • Higher Education
          • Sports
          • Youth
        • Health
          • Health
          • social welfare
        • Administration And HR
        • Planning & Coordination
          • Planning
          • Statistics
          • Community Development
          • TASAF
        • Economic and Production
          • Irrigation Farming
          • Commerce and Industries
          • Fishing
          • Livestock
          • Natural Resources, Tourism & Environment
          • Co operative
          • Agriculture
        • Investment Indusrty and Trade
      • Units
        • ICT
        • Legal Unit
        • Finance and Accounts
        • Internal Audit Unit
        • Procurement Unit
        • Government Communication
  • Districts
    • Bukoba
      • Bukoba Leaders
    • Biharamulo
      • Biharamulo Leaders
    • Karagwe
      • Karagwe Leaders
    • Kyerwa
      • Kyerwa Leaders
    • Missenyi
      • Missenyi Leaders
    • Muleba
      • Muleba Leaders
    • Ngara
      • Ngara Leaders
  • District Councils
    • Bukoba Municipal Council
    • Bukoba District Council
    • Biharamulo District Council
    • Karagwe District Council
    • Kyerwa District Council
    • Missenyi District Council
    • Muleba District Council
    • Ngara District Council
  • Investment Opportunities
    • Tourism Attractions
    • Farming Opportunities
    • Agricultural Opportunities
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • Water Services
    • Agricultural Services
    • Farming Services
  • Publications
    • By Laws
    • Client Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • News Letter
  • Media Center
    • Videos
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Profesa Kamuzora Ashauri Seminari ya Katoke Kuanzisha Masomo ya Programu za Talakilishi Ili Kuendana na Dunia ya Sayansi na Teknolojia

Posted on: May 20th, 2019

Wahitimu Kidato cha Sita 24 Sita Tu Kuendelea na Wito wa Upadre 

Profesa Faustin Kamuzora Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera aushauri uongozi wa Seminari ya Mtakatifu Karoli Lwanga Katoke alikosoma Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli kuanzisha maabara ya Talakilishi (Computer Labaratory) na kutoa elimu juu ya ubunifu na uanzishwaji wa programu (software) mbalimbali badala  ya kujikita kwenye matumizi  ya talakilishi tu (yaani namna ya kutumia Computa tu).

Profesa Kamuzora alitoa ushauri huo katika maafali ya 29 ya kidato cha sita katika Seminari ya Katoke Wilayani Biharamulo alipokuwa mgeni rasmi Mei 18, 2019 ambapo alisistiza kuwa Seminari hiyo imekuwa na mchango mkubwa kwa taifa la Tanzania ni lazima iendane na ulimwengu wa Sayansi na Teknolojia mfano kuanzisha program za  wa watu kuweka ulinzi majumbani mwao kwa kutumia simu au kuwasha na kuzima umeme ukiwa mbali na nyumbani.

Katika mahafali hayo Profesa Kamuzora aliwaasa wahitimu 24 wa kidato cha sita pamoja na wananfunzi wanaobaki kuchapa kazi kwa bidii sana kuheshimu misingi ya maadili waliyofundishwa na walimu wao ili kuyafikia mafanikio kama wanafunzi waliotangulia katika Seminari hiyo walivyopata mafanikio katika sehemu mbalimbali ndani na je ya nchi.

“Naomba kujitolea mfano mimi mwenyewe ambaye nilipita katika Seminari hii ya Katoke mwaka 1977 hadi 1980 kwa kufuata malezi na maadili ya Seminari hii nimeweza kusoma hadi ngazi za juu sana na kuwa Profesa  na nimefanya kazi sehemu mbalimbali lakini siri kubwa ni malezi na maadili niliyoyapata hapa. Pia Mhe. Rais Magufuli alipita hapa sasa unaweza kuona namna ya utendaji kazi wake ni kutokana na alichokipata hapa.” Alitoa ushuhuda Profesa Kamuzora.

Katika mahubiri yake wakati wa ibada takatifu ya kuwapongeza wanafunzi 24 wahitimu wa kidato cha sita Padre Fortunatus Bijura alisema kuwa ibada hiyo iliadhimishwa ikiwa ni ibada ya Mtakatifu Joseph mchapakazi ili kuwakumbusha vijana hao 24 pamoja na wanafunzi wengine wanaosoma katika Seminari hiyo kuwa kuchapa kazi ndiyo msingi wa mafanikio ya kila kitu katika maisha ya mwanadamu.

Padre Bijura pia aliwapongeza na kuwakumbusha wahitimu wa kidato cha sita katika ibada hiyo kuwa Mungu hujua wito wa kila mtu kabla hajazaliwa na kumaliza kidato cha sita ndiyo mwanzo wa wito wa upadre kwani baada ya hapo kuna miaka minane au tisa mpaka mtu awe padre. Wanafunzi walitakiwa kuchapa kazi kwa bidii hasa katika masomo yao na kuzingatia misingi ya maadili waliofunzwa katika Seminari hiyo.

“Maisha si starehe tu, sisi Watanzania bado tupo nyuma sana katika kuchapa kazi nitatoa mfano kwa wenzetu Wajerumani na Wamarekani hawa wanachapa sana kazi, wanakula sana na wanakunywa bia sana lakini wanaheshimu sana muda wao wa kupumzika. Lakini hapa Tanzania utawasikia vijana wakisema hebu twende kijiweni kupoteza muda kidogo, sijui muda huo wanautoa wapi.” Alisisitiza Padre Bijura ambaye ni mwalimu wa somo la Kiingereza Katika Seminari ya Katoke.

Padre Bijura alimalizia mahubiri yake kwa kuwaasa vijana 24 wahitimu wa kidato cha sita kwa kuwataka kuwa mfano bora wa kuchapa kazi na wale ambao walichagua kutoendelea na wito wa upadre kuwa mabalozi wema uraiani kwa kuchapa kazi, pia wakitunza muda wao vizuri na kutokuchagua kazi bali kuthamini na kuipenda kazi (Sense of Belonging)  lakini kazi hiyo isiwafanye wakamsahau Mungu.

Kwa upande mwingine Padre Jovine Bampabula ambaye ni Padre mlezi wa wanafunzi wa Seminari ya Katoke lakini pia alisoma katika Seminari hiyo kuanzia mwaka 1975 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuli akihojiwa juu ya Seminari hiyo kuzalisha viongozi bora alisema kuwa ni kutokana na malezi na maadili yanatolewa katika Seminari hiyo ya Katoke.

Seminari hii inazalisha Mapadre na wataalam wengine ambao huja kuwa watu wakubwa katika fani mbalimbali kwenye taifa letu na nje ya nchi. Mfano mimi nilisoma na Rais Magufuli tangu mwaka 1975 hapa mimi nilipata upadre yeye sasa ni Rais wa nchi, watu wengi wanashangaa ujasiri  wa kutoa maamuzi na kupambana na Mafisadi lakini mimi sishangai kwani najua kuwa ujasiri ule ni kutokana na maadili na malezi bora aliyoyapata kutoka katika Seminari yetu hii ya Katoke.

Wafanyakazi katika shamba la Bwana ni wengi lakini Wateule ni wachache; Wanafunzi waliohitimu kidato cha Sita Seminari ya Katoke mwaka 2019 jumla ni 24 lakini walianza kidato cha tano wakiwa 27 katika mahafali yao ya kuhitimu Mkuu wa Seminari hiyo Padre Datius Rwegoshora alisema kuwa wanafunzi ambao walikuwa tayari wamejitafakari na kuamua kuendelea na wito wa upadre kati ya 24 ni sita tu ambao walipewa barua kuendelea na wito na kuitwa Mafrateli kuanzia siku hiyo.

Tuwaombee vijana hawa ili waifikie ndoto yao ya kuwa wachungaji wa Kondoo wa Bwana na kuhudumu katika shamba la Bwana. Seminari ya Mtakatifu Karoli Lwanga Katoke ilianzishwa mwaka 1964 Wilayani Biharamulo Mkoani Kagera ikiwa chini ya Jimbo Katoriki la Rurenge.

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • View All

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
More Videos

Quick Links

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Radio Stations in Kagera Region
  • Kagera Regional Commissioners Since Independence 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • National Bureau of Statistics (NBS)
  • Government of Tanzania Website
  • Open Data Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Postal Address: S.L.P 299 BUKOBA

    Telephone: 255 28 2220215/17

    Mobile:

    Email: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Hakimiliki

Copyright ©2017 GWF . All rights reserved.