• complaint |
    • Contact Us |
    • FAQ |
    • Staff Mail |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

The United Republic of Tanzania President's Office Regional Administration and Local Government KAGERA REGIONAL WEBSITE

  • Home
  • About Us
    • History
    • Mission and Vision
    • Core Values
    • Strategies
  • Administration
    • Organization Structure
    • Sections/Units
      • Sections
        • Management Monitoring and Ispection
        • Infrastructure
        • Education
          • Primary Education
          • Secondary Education
          • Adult Education
          • Higher Education
          • Sports
          • Youth
        • Health
          • Health
          • social welfare
        • Administration And HR
        • Planning & Coordination
          • Planning
          • Statistics
          • Community Development
          • TASAF
        • Economic and Production
          • Irrigation Farming
          • Commerce and Industries
          • Fishing
          • Livestock
          • Natural Resources, Tourism & Environment
          • Co operative
          • Agriculture
        • Investment Indusrty and Trade
      • Units
        • ICT
        • Legal Unit
        • Finance and Accounts
        • Internal Audit Unit
        • Procurement Unit
        • Government Communication
  • Districts
    • Bukoba
      • Bukoba Leaders
    • Biharamulo
      • Biharamulo Leaders
    • Karagwe
      • Karagwe Leaders
    • Kyerwa
      • Kyerwa Leaders
    • Missenyi
      • Missenyi Leaders
    • Muleba
      • Muleba Leaders
    • Ngara
      • Ngara Leaders
  • District Councils
    • Bukoba Municipal Council
    • Bukoba District Council
    • Biharamulo District Council
    • Karagwe District Council
    • Kyerwa District Council
    • Missenyi District Council
    • Muleba District Council
    • Ngara District Council
  • Investment Opportunities
    • Tourism Attractions
    • Farming Opportunities
    • Agricultural Opportunities
  • Services
    • Health Services
    • Education Services
    • Water Services
    • Agricultural Services
    • Farming Services
  • Publications
    • By Laws
    • Client Service Charter
    • Strategic Plan
    • Reports
    • Forms
    • Guidelines
    • News Letter
  • Media Center
    • Videos
    • Press Release
    • Speeches
    • Photo Gallery

Ujue Mkoa wa Kagera Katika Uchumi wa Viwanda Tofauti na Viwanda Vya Kusindika Zao la Kahawa

Posted on: November 5th, 2018

Tangu Awamu ya Tano kuingia Madarakani mwaka 2015 Rais wa Jamuri ya Muungano wa Tanzania John Pombe Joseph Magufuli amekuwa akisisitiza Uchumi wa Viwanda ili nchi ya Tanzania ifikapo mwaka 2025 iwe na uchumi wa kati.

Katika kutekeleza Sera hiyo ya Serikali ya Awamu ya Tano  ya Uchumi wa Viwanda Mkoa wa Kagera haujabaki nyuma unatekeleza kikamilifu Sera hiyo kwa kuanzisha, kujenga na kundesha viwanda vya aina mbalimbali lakini pia kuendelea na juhudi za kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji na kuwakaribisha wawekezaji mbalimbali kuja Kagera kuwekeza katika viwanda vya aina mbalimbali.

Leo katika makala hii fupi mbali nakuujua Mkoa wa Kagera kuwa umejikita katika uchumi mkubwa wa viwanda vya Kahawa lakini pia Mkoa huo unafanya maajabu katika Nyanja ya viwanda vingine kikiwemo kiwanda cha kuchenjua madini ya bati kinachojulikana kwa jina la TANZAPLUS kilichopo Wilayani Kyerwa.

Kiwanda cha TANZAPLUS kilichopo Kijiji cha Kagenyi Kata ya Kyerwa Wilayani Kyerwa kimeleta mapinduzi makubwa ya uzalishaji wa madini ya bati hasa kwa kuongeza samani ya madini hayo yanayochimbwa katika Kata ya Kyerwa na kuuuzwa kwa bei stahiki lakini kuongeza ajira kwa wachimabaji wadogo kwa kuwa madini hayo sasa yana soko linaloaminika hapo hapo Wilayani Kyerwa.

Kwa miaka mingi madini ya bati yanayochimbwa Wilayani Kyerwa yalikuwa yakitoroshwa na kuuzwa katika nchi jiarani ya Rwanda tena kwa bei ndogo sana jambo ambalo lilikuwa likiinufaisha nchi hiyo wakati madini yanachimbwa hapa nchini katika Mkoa wetu wa Kagera.

Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Bw. Rashid Mwaimu akitembelea kiwanda hicho kuonesha jinsi Wilaya ya Kyerwa inavyotekeleza Sera ya Tanzania ya Viwanda alisema kuwa TANZAPLUS imekuwa mkombozi sana kwa vijana ambao ni wachimbaji wadogo kujihusisha zaidi na uchimbaji wa madini ya bati kwani sasa wamepata soko ambapo wanauza madini yao wakiwa ndani ya nchi na madini hayo yanachenjuliwa Wilayani hapo kwa ajili ya kuuzwa nje ya nchi yakiwa tayari yameongezwa thamani.

“Tumekuwa tukinyonywa sana hasa katika Wilaya yetu ya Kyerwa madini haya ya bati yanachimbwa hapa lakini yalikuwa yakiuzwa nje ya nchi tena hapa kwetu walikuwa wananunua kilo moja shilingi 15,000/= hadi 18,000/= tu lakini madini hayo hayo yakivushwa tu mpaka na kupelekwa nchini Rwanda yanauzwa hadi shilingi 48,000/= kwa kilo moja unaweza kuona unyonyaji ulivyo tene bila kulipa kodi ya Serikali.” Alieleza Mkuu wa Wilaya Rashid Mwaimu.

Mwekezaji Mzalendo ambaye ni Mtanzania Bw. Salim Mhando amabye ndiye Mkurugenzi Mkuu wa Kiwanda cha TANZAPLUS alisema kuwa pamoja na kuchenjua madini ya bati lakini kiwandani hapo lakini wameanza kutengeneza nyaya ambazo zinatumika katika matengenezo ya Kompyuta, Mashine za X ray, kutengeneza vipuli vya Tansfoma za kufua umeme, pia kutengenzea nyaya za kuyeyuesha katika uchomeleaji wa vifaa vya electronics (zijulikanazo kama risasi)

Bw. Salim alisema kuwa Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi sana kununua vifaa vinavyotengenezwa na madini ya bati kutoka nchi za nje lakini kwa kuanzisha kiwanda cha TANZAPLUS vifaa hivyo vitakuwa vinapatikana Mkoani Kagera Wilayani Kyerwa ambapo sasa wameanza majaribio ya kutengeneza vifaa hivyo na kuvipeleka katika majaribio kuona kama vitakidhi mahitaji.

Kuwepo kwa kiwanda cha TANZAPLUS Wilayani Kyerwa kutaongeza ajira kwa vijana lakini pia kubadilisha mtazamo wa wananchi wa Wilaya hiyo katika kunufaika na madini yanayochimbwa katika Wilaya yao pia Mkoa wa Kagera nao unakua kiuchumi kwa kuongeza ajira kwa vijana na  kuzalisha bidhaa kutoka Kagera.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti akizungumzia Sera ya Tanzania ya Viwanda na Kagera ya Viwanda anasema kuwa Mkoa wa Kagera umepiga hatua kubwa katika viwanda ambapo hadi kufikia Mwezi Oktoba 2018 Mkoa ulikuwa na viwanda 502 ambapo kati hivyo viwanda vikubwa ni tisa (9), vya kati ni 16 na viwanda vidogo ni 477.

Aidha, Mkuu wa Mkoa Gaguti anasema kuwa Mkoa unaendelea na juhudi za kuwakaribisha wawekezaji wa ndani naje nchi kuja Kagera kuwekeza ambapo tayari uongozi umetenga maeneo ya uwekezaji na ujenzi wa viwanda yenye ukubwa wa Hekta 58,000 katika maeneo mbalimbali kupitia kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa.

Unaweza kuona Mkoa wa Kagera unavyozidi kujipanga vyema kuimarisha uchumi wake na kutoa ajira kwa wananchi kupitia Kagera ya Viwanda. Msomaji wetu tutakuwa tukikuletea makala kama hizi za Uchumi wa Viwanda Mkoani ili uone Mkoa ulivyojidhatiti katika Viwanda. Je ni Kiwanda kipi unahisi tutakuletea na hutegemei kama kiwanda hicho kinaweza kuwa katika Mkoa wetu wa Kagera? Usikose kufuatilia.

Announcements

  • No records found
  • View All

Latest News

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • View All

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
More Videos

Quick Links

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Radio Stations in Kagera Region
  • Kagera Regional Commissioners Since Independence 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Related Links

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • National Bureau of Statistics (NBS)
  • Government of Tanzania Website
  • Open Data Tanzania

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Location Map

Contact Us

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Postal Address: S.L.P 299 BUKOBA

    Telephone: 255 28 2220215/17

    Mobile:

    Email: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • FAQ
    • Sitemap
    • Service
    • Hakimiliki

Copyright ©2017 GWF . All rights reserved.