• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Baada ya Tetemeko Kagera Sasa ni Shule ya Sekondari Ihungo Mpya ya Kisasa Yenye Ubora wa Miundombinu Safi Kwa Elimu – Rc Gaguti

Imewekwa : August 25th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti atembelea Shule ya Sekondari Ihungo na kuona maendeleo ya ukamilishwa wa baadhi ya miundombinu midogomidogo katika majengo baada ya Serikali kuamua na kuijenga upya shule hiyo iliyoharibiwa vibaya na Tetemeko la Ardhi lililotokea Mkoani Kagera Septemba 10, 2016

Mkuu wa Mkoa Gaguti mara baada ya kufanya ukaguzi na kuridhishwa na ujenzi wa shule hiyo Agosti 25, 2018 alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Pombe Magufuri kwa kufanya uamuzi sahihi wa kujenga upya shule hiyo ya Ihungo na kukarabati baadhi ya majengo  kwa gharama ya shilingi bilioni 10.45 na kuifanya shule hiyo iwe shule bora na ya kisasa nchini inayovutia elimu bora kwa wanafunzi.

Mara baada ya Shule ya Sekondari Ihungo kukamilika ujenzi wake kwa asilimiazaidi ya 90% Serikali tayari imewarudisha wanafunzi walikokuwa wamehamishiwa katika Shule ya Sekondari Omumwani Manispaa ya Bukoba na Chuo cha Ruhija Halmashauri ya Wilaya Bukoba ili wakaendelee na masomo yao katika shule yao ya Ihungo Sekondari.

Katika kukamilisha ujenzi wa miundombinu midogo midogo iliyobakia katika katika shule hiyo Mkuu wa Mkoa wa Mkoa Gaguti alisema kuwa yeye jukumu lake ni kufuatilia na kuhakikisha kila kilichopangwa kujengwa katika shule hiyo lazima kijengwe na kukamilshwa na Kampuni ya Tanzania Building Agency (TBA).

Tetemeko la Ardhi Mkoani Kagera lilisababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu yote ya Shule ya Sekondari Ihungo  ikiwemo Madarasa, Mabweni, Maabara, Bwalo, Jiko, Vyoo na Mabafu, Nyumba za Walimu, Jengo la Utawala, Kanisa, Msikiti, Maktaba na Mifumo ya maji na umeme. 

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imejenga majengo matatu ya madarasa yenye ghorofa moja kila moja, kila jengo lina vyumba 8 vya madarasa na ofisi 4 na kufanya jumla ya vyumba vya madarasa 24 yenye uwezo wa kuchukua wanafunzi 960 na jumla ya ofisi 12.

Serikali pia imejenga majengo 3 ya mabweni yenye ghorofa 2 kila moja, kila jengo lina uwezo wa kuchukua wanafunzi 384; hivyo majengo yote 3 ya mabweni yatachukua wanafunzi 1,152, vikiwemo vyoo na mabafu. Serikali pia inajenga nyumba mpya za wafanyakazi kwa matumizi ya familia 30.

Aidha, Serikali imefanya ukarabati wa Maktaba ya Shule, Jengo la Utawala, Maabara ya Kompyuta, Jengo la Kilimo, Bwalo, Jiko na Maabara za Fizikia, Kemia na Baologia.

Tayari Shule ya Sekondari Ihungo imepangiwa wanafunzi 679 wa Kidato cha Tano na tayari wanafunzi  556 wameripoti shuleni hapo tangu tarehe 16/7/2018 na wanafunzi hao ni wa michepuo ya PCB, PCM, CBG, EGM na HGE  na wanaendelea na masomo kadri ratiba ya shule ilivyopangwa.

Pamoja na changamoto za Tetemeko la Ardhi kuiharibu vibaya shule ya Ihungo Sekondari lakini wanafunzi na Walimu hawakukata tamaa kabisa bali walijifua vizuri na shule hiyo kuendelea kufanya vizuri katika mitihani ya Taifa  ya Kidato cha Sita mfano mwaka 2017 kati ya wanafunzi 372 waliofanya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Sita 54 walipata dalaja la kwanza, 133 daraja la pili, 167 daraja la tatu, 15 daraja la nne na watatu walipata sifuri.

Mwaka 2018 kati ya wanafunzi 364 walifanya Mtihani wa Taifa wa Kidato Sita 43, walipata dalaja la kwanza, 160 daraja la pili, 151 daraja la tatu, 8 daraja la nne na wawili walipata sifuri. Ikumbukwe kuwa Shule Sekondari Ihungo awali kabla ya Tetemeko kutokea ilikuwa ina uwezo wa kubeba wanafunzi 801 na kwasasa baada ya kujengwa upya inao uwezo wa kubeba wanafunzi 1,152.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa