• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Baadhi ya Wabunge wa Mkoa wa Kagera Wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa (Hayupo Pichani) Katika Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoani Kagera.

Imewekwa : March 8th, 2018

Mkuu wa Mkoa Kagera Aagiza Mkandarasi Kukamatwa na Kufikishwa Ofisini Kwake Akiwa na Pingu Mikononi Baada ya Kuitia Serikali Hasara

Mkuu wa Mkoa wa Kagera aagiza  Mkandarasi wa Kampuni ya MECCO aliyeshinda zabuni  ya ujenzi wa barabara zenye thamani ya shilingi bilioni saba na kukataa kusaini mkataba wa kuanza ujenzi katika Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba kukamatwa  na kufikishwa  Ofisini kwake akiwa na pingu mikononi ili kutoa sababu za kuitia Serikali hasara.

Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu alitoa agizo hilo kwa Kamanda wa Polisi Mkoa kwenye kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika Mkoani Kagera Machi 8, 2018 ambapo katika kuwasilisha hoja Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba Chief Karumuna  kumuomba Mkuu Mkoa kumchukulia hatua Mkandarasi huyo baada ya kugoma kusaini mkataba wakati alishinda zabuni ya ujenzi wa barabara hizo.

Chief Karumuna alisema kuwa Manispaa ya Bukoba imepata hasara baada ya Mkandarasi kukataa kusaini mkataba wa kuanza ujenzi wa barabara zenye thamani ya shilingi bilioni saba na zabuni kutangazwa tena upya, pia alisistiza kuwa fedha hizo zilitolewa na Benki ya Dunia na utekelezaji wa miradi yake ni wa kipindi maalumu kwa hiyo Mkandarasi huyo amechelewesha muda wa utekelezaji.

Katika kikao hicho ambacho Mkuu wa Mkoa ni Mwenyekiti aliwasistiza Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini TARURA Mkoa wa Kagera kuhakikisha wanatengeneza barabara za mipakani ili kuimarsha ulinzi na usalaama wa mkoa na na chi kwa ujmla. Barabara hizo ni Bubale-Missenyi Runch- Kakunyu  Kilomita 32.5, Bubale – Kamwema Kilomita 17.8  Wilayani missenyi na barabara ya Nyabishenge-Nyakanoni-Ibanda Game Reserve kilomita 15 Wilayani Kyerwa.

Vilevile Meneja wa Wakala wa Umeme na Ufundi (TEMESA) Mkoa wa Kagera ameagizwa na kikao hicho kusitisha mara moja tozo ya shilingi 80,000/= ya ukaguzi wa magari ya Serikali pale yanapotakiwa kukaguliwa ili yakatengenezwe baada ya wajumbe kuwasilisha sheria kikaoni inayoelekeza kuwa magari ya Serikali yanatakiwa kukaguliwa bure. Hadi Mkuu wa mkoa atakapopata walaka unaoruhusu kutoza magari ya Serikali.

Mkoa wa Kagera unahudumia barabara zenye mtandao wenye jumla ya kilomita 7,505.42 kati ya hizo, kilometa 675.46 ni barabara za lami, kilometa 2,791.56 barabara za changarawe na kilometa 4,038.96 zikiwa in barabara za udongo.

Mkoa wa Kagera kwa mwaka wa fedha 2017/18 uliidhinishiwa shilingi Bilioni 10,710.05 kwajili ya matengenezo ya kazi za barabara na ujenzi wa madaraja. Pia mkoa umeidhinishiwa shilingi bilioni 14,180.937 kwa ajili ya matengenezo ya Barabara Kuu na Barabara za Mkoa kwa mwaka wa fedha 2017/18

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Mkoani Kagera Mkuu wa Mkoa wa Kagera amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Godfrey Mheluka kumkamata na kumpeleka ofisini kwake kijana anayemtesa mama yake mzazi kwa kutaka kumnyanganya shamba lake na mama huyo ameshinda kijana huyo mara mbili Mahakamani.

“Mtafute kijana huyo na kumleta kwangu nijue ana matatizo gani ili tumsaidie maana atamuua mama yake, hana uchungu na mama yake mzazi. Mama huyoaliwasilisha kilio chake katika mkutano wa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi Mhe. Lukuvi Wilayani Karagwe lakini kijana huyo bado anaendelea kumsumbua mama yake mzazi.” Alifafanua Mkuu wa Mkoa Kijuu.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa