• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Karagwe Wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Kagera (hayupo pichani) Kwa Umakini

Imewekwa : May 31st, 2018

Watumishi Wawili Halmashuri ya Wilaya ya Karagwe Wasimamishwa Kazi Kupisha Uchunguzi wa Upotevu Wa Zaidi ya Shilingi Milioni 500

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu leo Mei 31, 2018 awasimamisha kazi watendaji wawili wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe kufuatia utendaji usioridhisha wa ukusanyaji wa mapato kwa njia ya kieletroniki na kusababisha upotevu wa kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 500 katika Halmashauri hiyo.

Hatua hiyo imechukuliwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera baada ya Katibu Tawala wa Mkoa CP Diwani Athuman kuunda tume ya uchunguzi wa upotevu wa fedha hizo kutokana na ripoti ya Mkaguzi wa ndani wa Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe ambapo tume hiyo ilifanya kazi ya uchunguzi kwa siku nne tu na kubaini upotevu fedha cha shilingi 500,000,000/=

Uamuazi wa kuwasimamisha kazi watumishi wawili Afisa TEHAMA Bw. Beatus Nyarugenda na Mhasibu wa Mapato Bw. Innocent Kakulima ulitolewa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Kijuu katika kikao cha Kamati ya Fedha cha Halmashauri hiyo ambapo alitoa maagizo kama ifutavyo;

Moja, Uchunguzi wa kina ufanyike kwa kila Maafisa walioomba na kuidhinisha marekebisho au miamala ya mapato ya ndani katika mfumo bila kuwa na kibali cha Afisa Masuuli na kiasi cha fedha kinachohusika katika eneo hilo ni Shilingi 427,027,430.49/=

Pili, Watumishi waliokusanya mapato na hawajapeleka benki fedha walizokusanya jumla ya Shilingi 127,094,900/= hadi tarehe 14 Aprili, 2018 waziwasilishe katika akaunti ya mapato ya Halmashauri ndani ya siku 7, na vielelezo vihakikiwe na Katibu Tawala wa Wilaya ya Karagwe na watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo sheria ichukue mkondo wake.

Tatu, Afisa TEHAMA Bw.Beatus Nyarugenda tume ilimbaini kuwa hakuwa makini kwa kukiuka usalama wa mtandao kwa kutoa haki kwa Afisa mmoja kukamilisha muamala mzima wa kufuta ama kubadili tarakimu za fedha katika mtandao. Mkuu wa Mkoa aliagiza utaratibu huo uachwe mara moja na Mkuu wa TEHAMA wa Mkoa kuhakikisha usalama wa mfumo unawekwa vizuri mara moja.

Nne, Mhasibu wa Mapato Bw. Innocent Kakulima tume ilimbaini kutokuwa na uthibitisho wa kupeleka benki shilingi 23,216,400/= fedha ambazo alizichukua kutoka kwa wakusanyaji. Aidha katika ufuatiliaji ilibainika kuwa katika Halmashauri ya Karagwe kuna vituo vya ukusanyaji (POS) 39, hivyo inahitajika uchunguzi zaidi ili kuwa na uhakika katika vituo vyote kama Mhasibu huyo hakukusanya fedha.

Baada ya maagizo hayo Mkuu wa Mkoa Mhe. Kijuu alimwagiza Kamanda wa TAKUKURU Mkoa kupokea taarifa hiyo kwa ajili ya kuifanyia uchunguzi ambao utatoa majibu sahihi ya kushuka kwa mapato ya Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe.

Aidha, wakati uchunguzi unafanyika Mkuu wa Mkoa Mhe. Kijuu aliagiza Afisa TEHAMA Bw. Beatus Nyarugenda na aliyekuwa Mhasibu wa Mapato Bw. Innocent Kakulima wasimame kazi kupisha uchunguzi huo. Pia aliagiza kuwa wakati uchunguzi unaendelea watuhumiwa wengine watakaobainika kuwa wanaweza kuingilia uchunguzi wawapo maeneo yao ya kazi ajulishwe haraka ili nao wahusishwe kupisha uchunguzi.

Mkuu wa Mkoa Mhe. Kijuu alihitimisha kwa kurudia kumuagiza Kamanda wa TAKUKURU Mkoa kufanya Uchunguzi na kuukamilisha haraka pia na kuzitahadharisha Halmashauri nyingine za Wilaya za Mkoa wa Kagera hususani Wakurugenzi Watendaji na Watumishi wengine kufanya kazi kwa uadilifu na uaminifu mkubwa bila kujihusisha na vitendo vya kuyahujumu mapoto hasa mapato ya ndani ya Serikali.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa