• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Balozi wa Tanzania Nchini Rwanda Atembelea Mkoa Wa Kagera na Kuwahamasisha Wanakagera Kuchangamkia Fursa za Kiuchumi Nchini Rwanda

Imewekwa : June 27th, 2018

Balozi wa Tanzania Nchini Rwanda Mheshimiwa Ernest Mangu afanya ziara ya siku mbili Mkoani Kagera na kukutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa Mkoa kuhusu kuchangamkia  fursa za kiuchumi nchini Rwanda kati ya wananchi wa Mkoa wa Kagera na nchi ya Rwanda.

Balozi Ernest Mangu akiwasili Mkoani Kagera kupitia mpaka wa Tanzania na Rwanda Rusumo Julai 25, 2018  na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Salum M.  Kijuu aliweza kufanya mazungumzo na watumishi wa Kituo cha kutoa huduma kwa Pamoja cha Rusumo (OSBP) upande wa Tanzania na kuwaelekeza namna bora ya kuboresha huduma katika kituo hicho ili wananchi wa nchi mbili wanufaike zaidi.

Katika mpaka wa Rusumo Kituo cha kutoa huduma kwa pamoja (OSBP) kinahudumia magari 350 na watu 450 kwa siku ambapo Balozi Mangu alitaka kujua watu wanaohudumiwa kwa siku wengi wanatoka Tanzania kwenda Rwanda au kutoka Rwanda kuja Tanzania ili kama wengi wanatoka Rwanda kuja Tanzania ajue ni kwanini Watanzania hasa wa Mkoa wa Kagera hawachangamkii fursa za kibiashara nchini Rwanda.

Pia Balozi Mangu alitoa changamoto kwa uongozi wa Mkoa wa Kagera kuwa Rwanda kuna fursa nyingi za kiuchumi hasa biashara ambapo Wanyarwanda wengi wanapendelea kwenda Nchini Uganda Jijini Kampala kununua bidhaa  mbalimbali kutokana na bidhaa hizo nyingi kupatikana Jijini Dar es Salaam ambako ni mbali sana kutoka Kigali.

Ili kutatua changamoto hiyo na kuwavutia Wanyarwanda Wafanyabiashara wa Tanzania hasa wa Mkoa wa Kagera wanatakiwa kuanzisha maduka makubwa ya bidhaa mbaimbali za jumla katika mpaka wa Rusumo upande wa Tanzania ili kuwavutia Wafanyabiashara kutoka Rwanda ambapo Rusumo ni karibu sana kuliko Jijini Kampala nchini Uganda. “Rusumo inaweza kuwa Dar es Salaam ya Kigali na Wanyarwanda wakaishia hapa.” Alisisitiza Balozi Mangu.

“Wanyarwanda wanapenda sana mchele kutoka Kahama, wanapenda sana dagaa  na Samaki kutoka Ziwa Viktoria na si Kigali tu bali na nchi ya Kongo bidhaa hizo ni adimu sana jambo linalopelekea kuwa na soko kubwa lakini sijaona zikiuzwa kwa biashara rasmi bali kimagendomagendo tu, sasa hiyo ni fursa kwa Wafanyabiashara wa Kagera kufungua maghara makubwa hapa Rusumo ili biashara hiyo ifanyike hapa na kodi ilipwe na kunufaisha nchi zote mbili.” Alifafanua Balozi Mangu.

Katika hatua nyingine Balozi Mangu alikutana na Wafanyabiashara mjini Ngara na kusikiliza changamoto zao zinazowakwaza kufanya biashara na nchi ya Rwanda na kuhaidi kuzifanyia kazi ili pande zote mbili wananchi wake wanufaike kiuchumi kutokana na fursa ya kuwepo mpaka kati ya nchi hizo.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu alimuhaidi Balozi Mangu kuhakikisha anayafanyia kazi maelekezo yake yote ili kuhakikisha wananchi wa Mkoa wa Kagera hasa Wafanyabiashara wananufaike kiuchumi na fursa ya kuwepo mpaka wa Rusumo ambao unaziunganisha nchi za Rwanda na Tanzania.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa