• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Barabara ya Kyaka Bugene Iliyozinduliwa Rasmi Novemba 07,2017 na Rais John Pombe Magufuli Wilayani Karagwe Mkoani Kagera

Imewekwa : November 7th, 2017

Rais Magufuli Azindua Rasmi Barabara ya Kyaka Bugene na Kuhaidi Kumalizia Kipande Kilichobaki Hadi Kasulo Ngara

Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amezindua rasmi barabara ya Kyaka Bugene yenye urefu wa kilometa 59.1 iliyojengwa kwa kiwango cha lami kwa gharama ya shilingi bilioni 81.597 fedha zilizogharamiwa kwa asilimia 100 na Serikali ya Tanzania.

Rais Magufuli kabla ya kuzindua barabara hiyo ya Kyaka Bugene inayoziunganisha Wilaya mbili za Missenyi na Karagwe akiongea na wananchi alisema kuwa Serikali itaendelea kujenga kipande kilichobaki hadi Kasulo Wilayani Ngara na Kukamilisha jumla ya kilometa 183.1

Akitoa Taarifa ya ujenzi wa barabara hiyo Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini TANROADS Bw.Patrick Mfugale alisema kuwa barabara hiyo imesimamiwa na Watanzania baada ya Kampuni  kutoka India iliyokuwa imepewa tenda ya  kusimamia kushindwa kazi na na Serikali kuamua kuifukuza kazi.

Aidha, Bw. Mfugale alisema Kampuni hiyo kama ingefanya kazi mpaka mwisho wa kukamilisha barabara hiyo ingelipwa shilingi bilioni 4 lakini baada ya kuisimamishwa kazi na kupewa Watanzania ambao wamesimamia mpaka barabara kukamilika wamelipwa shilingi milioni 500 tu na kuokoa shilingi bilioni 3.5

Katika hatua nyingine Rais Magufuli aliwahakikishia wananchi wa Wilaya ya Karagwe kuwa Serikali tayari imeiweka kwenye mpango  wa ujenzi barabara ya Omugakorongo Mulongo ili ijengwe kwa kiwango cha rami kusudi wananchi waweze kufanya biashara na nchi jiarani ya Uganda.

Rais Magufuli akiongelea kero za wananchi wa Wilaya ya Karagwe alisema anajua kuwa kero ya maji Karagwe ni ya muda mrefu, ambapo alisema kuwa serikali imeainisha  miji 17  na Karagwe ikiwemo na tayari Serikali imepata mkopo wa fedha Dola Milioni 500 kutoka nchi ya India na Wilaya ya Karagwe imetengewa Dola milioni 70 kwajili ya ujenzi wa mradi wa maji.

Pia Rais Magufuli alisema kuwa anajua kuwa Karagwe kuna Kero kubwa ya ardhi na kuwataka wananchi wote waliovamia vyanzo vya maji kuondoka mara moja na kuuagiza uongozi wa Mkoa kuhakikisha unasimamia kikamilifu na kuhakikisha unawatafutia maeneo mbadala ya kuishi.

“Jamani najua kuna sheria za mazingira lakini tukiamua kuzisimamia sheria hizo kwa karibu sana wananchi watakosa mahala pa kuishi, kama wananchi wanalima kandokando ya mito pengine wakati wa kiangazi wakitekeleza sera ya hapa kazi tu waacheni walime kwani hawazuii maji yaliyoletwa na Mungu kutirirka.” Alisistiza Rais Magufuli.

Rais Magufuli alitolea mfano wa kijana mmoja aliyetoa kero yake kwake wakati akisalimia wananchi eneo la Kyaka Wilayani Missenyi akielekea Wilayani Karagwe  kuwa kijana huyo alifukuzwa kando kando ya Mto Kagera wakati akilima mahindi yake. Rais Magufuli aliagiza kijana huyo kuendelea kulima na wananchi wengine isipokuwa watakaolima  kwenye vyanzo vya  maji ndiyo wachukuliwe hatua za kisheria.

Mwisho Rais Magufuli aliwapongeza Waandishi wa Habari kwa kazi kubwa wanayoifanya pia na vyombo vya habari kwa kufanya kazi kubwa ya kuwahaabarisha wananchi. Rais Magufulia ataendelea na ziara yake Wilayani Missenyi katika kiwanda cha Kagera Sukari kesho Novemba 8. 2017.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa