• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Bibi Restuta Tibalila Kaimu Katibu Tawala Wilaya ya Bukoba Akifungua Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Mkoani Kagera

Imewekwa : May 4th, 2018

Waandishi wa Habari Wakumbushwa Kuzama Chini Kwenye Jamii Kuandika Habari za Wananchi Zenye Vyanzo Sahihi

Waandishi wa Habari Mkoani Kagera wakumbushwa kwenda kwa wnanchi katika ngazi za chini kabisa hasa vijijini kuona matatizo ya wananchi na kuyaibua kwa kuandika habari zao zitakazolenga kutafuta ufumbuzi wa matatizo yao na kuwatoa sehemu moja na kupiga hatua ya maendeleo kuliko kuandika habari za mijini tu ambazo zimezoeleka.

Hayo yalisemwa na Bibi Restuta Tibalila Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya ya Bukoba alipomwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Bukoba  Mhe. Deodatus Kinawilo katika ufunguzi wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya  Habari ambayo huadhimishwa  kila mwaka Mei 3 ambapo  Waandishi wa Habari Mkoani Kagera walijumuika na wenzao Duniani kuadhimisha siku hiyo katika ukumbi wa Hoteli ya Bukoba Coop Manispaa ya Bukoba .

Katika hotuba yake Mkuu wa Wilaya ya Bukoba iliyosomwa na Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya alivipongeza vyombo vya Habari na Waandishi wa Habari Mkoani Kagera kwa kuchangia sehemu kubwa ya maendeleo ya mkoa kwa kuandika habari ambazo zinaelimisha jamii juu ya masuala mbalimbali yanayolenga kuinua uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na mkoa kwa ujumla.

Vilevile Mkuu wa Wilaya Bukoba katika hotuba yake aliwashukuru wamiliki wa vyombo vya Habari kuendelea kufanya uwekezaji katika Vyombo vya Habari na masuala ya habari kama kuanzisha Redio za Kijamii na magazeti ambapo vinachangia sehemu kubwa kwa wananchi kupata habari mbalimbali zinazohusu mkoa wao na kwa wakati.

Aidha, Mkuu wa Wilaya katika hotuba yake aliwahakikishia Waandishi wa Habari kuwa Serikali Mkoani Kagera itaendelea kuheshimu uhuru wa vyombo vya habari ili vitimize wajibu wake pia Serikali itaendelea kutoa ushirikiano wa karibu  ili wananchi ambao ni walaji wapate habari sahihi na zenye uhakika.

Katika Maadhimisho hayo yaliyoratibiwa na Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Kagera pia walialikwa wadau mbalimbali ambao walishirikiana na waandishi wa Habari na Wamiliki wa Vyombo vya Habari kujadili na kuchambua mada isemayo  “Uhuru wa Habari ni Chachu ya Uwajibikaji kwa maendeleo ya Mkoa.”

Wadau wakichangia mada hiyo waliwashauri Waandishi wa Habari kuhakikisha wanaandika habari zenye vyanzo vyenye uhakika na zenye maslahi mapana na jamii ili kubadili mtazamo wa jamii kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine ya maendeleo.

Pia  Waandishi wa Habari walishauriwa kuhakikisha wanazama chini katika jamii kuandika habari za wananchi wa kawaida au kuandaa vipindi ambavyo vinawagusa wananchi wa chini kabisa ambao wangependa kuona mabadiliko chanya katika maisha yao kwa kuelimishwa kupitia vyombo vya habari.

Chanagamoto kubwa waliopewa waandishi wa Habari ni kujiendeleza kielimu ili kuhakikisha wanankuwa na ufahamu wa kutosha na masuala mbalimbali ambayo wanayaandika au kuandaa vipindi juu ya masuala hayo pia kuendana na matakwa ya Sheria ya Vyombo vya Habari ya mwaka 2016.

Kwasasa Mkoa wa Kagera unavyo vituo vya  redio vipatavyo tisa, Kasibante, Fadeco, Karagwe, Shinuz, KCR, Vision, Kwizera, Bukoba na redio Mbiu. Pamoja na Redio nyingine nyingi ambazo zinasikika katika Mkoa wa Kagera zikirusha matangazo yake kutoka nje ya mkoa.

Pamoja na Redio kuna magazeti, mitandao ya kijamii, Cable TV, ambavyo vinautangaza mkoa wetu wa Kagera na kuwapasha wananchi wake kupitia Waandishi wa habari ambao wametapakaa mkoa mzima wakiandika habari mbalimbali za michezo, kuichumi, kijamii, Elimu, Utalii, Uwekezaji na nyinginezo nyingi.

Siku ya Mei 3 ilitangazwa na Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuwa Siku ya Uhuru wa Vyombo vya  Habari Duniani. Siku ya Uhuru wa Vyombo vya  Habari Duniani huongeza ufahamu wa umuhimu wa uhuru wa vyombo vya habari na kuikumbusha Serikali wajibu wake wa kuheshimu na kuhakikisha haki ya uhuru wa kujieleza inaheshimika  chini ya Ibara ya 19 ya Azimio la Kimataifa la Haki za Binadamu la 1948. Pia katika Siku hiyo Hukumbukwa Waandishi waliotangulia Mbele za Haki.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa