• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Fursa za Uwekezaji Zachambuliwa Kisomi Kwenye Kongamano la Wiki la Uwekezaji Kagera Kuonesha Mwanga wa Kuelekea Katika Uchumi Mpya wa Mkoa

Imewekwa : August 15th, 2019

Baada ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa kuzindua rasmi Wiki ya Uwekezaji Kagera Agosti 14, 2019 akizindua pia Kongamano la Uwekezaji na kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera  leo Agosti 15, 219 wadau mbalimbali wa uwekezaji na wafanyabiashara katika kongamano walijadili fursa mbalimbali za uwekezaji kwa kuzichambua kwa undani zaidi.

Katika Kongamano hilo la Wiki ya Uwekezaji Kagera jumla ya mada nane ziliwasilishwa na wataalam kutoka Sekta mbalimbali za umma na Sekta binafsi kwa kuzichambua na kujadili kwa kina kupata mwelekeo wa uwekezaji hasa majadiliano yakilenga namna bora ya kuondoa vikwazo na kusonga mbele katika kuinua uchumi wa mkoa wa Kagera

Mada nane zilizowasilishwa na wasomi wabobezi na wajasiliamali wenye uzoefu mkubwa katika ujasiliamali na kuzichambua kwa undani kuonesha fursa zilipo na zinaweza kufikikaje ni pamoja na mada ya  Ujue Mkoa wa Kagera iliyowasilishwa na Askofu Msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba Method Kilaini ambaye ni mbobezi katika masuala ya historia ambapo aliuchambua mkoa wa Kagera kihistoria miaka ya nyuma na kwa sasa mkoa ulipo.

Mada nyinginezo ni; Mazingira ya jumla ya kibiashara na jukumu la mamlaka za kisheria katika kusaidia uwekezaji, Tatu; Mkoa wa kagera kama kitovu cha biashara katika nchi za Afrika Mashariki na Kati (Biashara za Mipakani), Nne, Kutumia fursa za uwekezaji Kagera katika sekta za kilimo, mifugo, uvuvi na Viwanda, Tano; Ni namna gani changamoto ya lishe katika mkoa wa Kagera inaweza kutumika kama fursa ya uwekezaji.
Aidha, mada nyingine zilizojadiliwa ni pamoja na; Ni namna gani fursa za utalii ambazo hazijatumika ipasavyo zinaweza kutumika katika uwekezaji kwenye mkoa wa Kagera, Saba; Nafasi ya huduma za kijamii kwa ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Kagera. Mada ya mwisho ilikuwa ni huduma za kifedha kama kichocheo cha uwekezaji na ukuaji wa uchumi.
Mara baada ya mawasilisho ya mada tajwa hapo juu ikiwa ni pamoja na uchambuzi wa hali ya juu kuhusu mada hizo na washiriki kuchangia kwa kuonesha ni fursa gani zinapatika na zinafikikaje katika mkoa wa Kagera Wafanyabiasha kutoka nchi za Rwanda na Burundi walipata nafasi ya kukutana Wafanyabiashara wa Mkoa wa Kagera na kuwa na mazungumzo ya kibiashara (B2B Discution) kulingana na mtu kavutiwaje.
Baada ya Wiki ya Uwekezaji Kagera kufika mwisho uongozi wa Mkoa wa Kagera utakuwa na orodha ya jumla ya biashara ambazo wafanyabiashara kutoka nje ya nchi watakuwa wameingia makubaliano na wenzao kutoka nchi jirani ili kufanya ufuatiliaji na kuhakikisha fursa hizo zinafikika na kutumika.
Wiki ya Uwekezaji Kagera inatarajiwa Kufungwa rasmi tarehe 16/08/2019 lakini maoonesho ya bidhaa mbalimbali yatakuwa yanaendelea katika viwanja vya Gymkhana Manispaa ya Bukoba hadi tarehe 18/08/2019 na Wadau mbalimbali wa uwekezaji watapata fursa za kwenda kutembelea vivutio mbalimbali vya uwekezaji katika mkoa wa Kagera.
 

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa