• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Hifadhi ya Brigi-Chato Sasa Kumekucha ni Baada ya Mfalme wa Pori Kupokelewa na Familia Yake Kutawala Eneo Hilo

Imewekwa : February 7th, 2020
  • Je Wajua Kuwa Nusu ya Simba Wote Duniani Wapo Tanzania?

Brigi- Chato kumekucha sasa  Mfalme wa Pori  (Simba) na familia yake awasili katika hifadhi hiyo ya Taifa  ili kutawala eneo hilo muhimu la utalii katika ukanda wa Kaskazini Magharibi mwa Tanzania. Ni ukoo mmoja wa simba 20 ukiwa na simba wazima 17 na simba watoto 3 wapokelewa  katika lango la Nyungwe Hifadhi ya Taifa ya Brigi-Chato Februari 6, 2020 na Mkuu wa Mkoa  wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti.

Katika Simba hao 20 Baba anaitwa Brigi na mama anaitwa Chato wakiwa na familia yao ya simba wengine 18 waliwasili Nyungwe katika Hifadhi ya Brigi-Chato majira ya saa 5:00 asubuhi wakisafirishwa kutoka katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti Mkoani Mara na dhumuni la kuwaleta simba hao ni kuhakikisha hifadhi ya Brigi- Chato inakuwa na wanyamapori  wote hasa wale wakubwa watano ili kuvutia zaidi utalii.

Kwaniaba  ya wananchi wa Mkoa wa Kagera na Geita mara baada ya kuwapokea Simba hao 20 wakiongozwa na baba Brigi na Mama Chato Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa neno  la kumshukuru Rais John Pombe Magufuli kwa kuamua  kuanzisha Hifadhi ya Taifa Brigi-Chato katika ukanda wa Kaskazini Magharibi  ili kufufu upya uchumi wa mikoa ya Kagera na Geita kupitia utalii.

“Sisi wananchi wa Kagera tunayo furaha sana kuwapokea Simba hawa kwani katika eneo hili uchumi wetu utakua kwa kasi, lakini nimshuru tena Mhe. Rais Magufuli  kwa maamuzi yake sahihi kuanzisha hifadhi hii kumesaidia sana, hakuna asiyejua kuwa miaka ya nyuma kulikuwa na hatari sana katika maeneo haya ya Brigi kwa majambazi kutumia hifadhi hii kuteka wananchi l pia kuendesha vitendo vya kiharamia lakini sasa hakuna tena.” Alisisitiza Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwashukuru pia uongozi wa Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa kuamua Hifadhi ya Serengeti itoe Simba 20 ili waletwe katika Hifadhi ya Taifa ya Brigi-Chato ambapo aliwahaidi yeye kwakushirikiana na wananchi wa mkoa wa Kagera watahakikisha kuwa hakutakuwepo na changamoto zozote zitakazojitokeza ambazo ziliwahi kujitokeza katika Hifadhi nyingine za Taifa.

Kamishina  wa Uhifadhi  Martin Loibooki ambaye ni  Mkuu wa Kanda ya Magharibi kwaniaba ya Kamishna Mkuu Dkt.  Allan Kijazi akieleza sababu za kuhamisha simba 20 kutoka Serengeti kuja Brigi-Chato alisema kuwa katika hali ya kawaida kuna wanyama wanaokula nyasi na kuna wanayama kama simba wanakula nyama au wanakula wanyama wezao na hilo linasaidia katika ekolojia ya wanyamapori .

Kamishna Loibooki alisema pia katika Hifadhi ya Taifa ya Brgi-Chato siyo mara ya kwanza hifadhi hiyo kuwa na Simba na ndiyo maana kuna maeneo katika hifadhi hiyo  yanajulikana kwa jina la Mllima wa Simba lakini kutokana na shughuli za kibinadamu na uvamizi wa hifadhi hizo simba waliweza kutoweka kwa kuuawa na binadamu ili wasidhurike na ndiyo maana simba wakatoweka.

Naye Dkt. Denis Itanda Mtafiti Mkuu wa wanyamapori aliyeongoza jopo la Madaktari na wataalam kuhakikisha simba 20 kwanza wanakamatwa kule Serngeti wananwekwa kwenye vitenga na kusafirishwa salama hadi katika Hifadhi ya Brigi-Chato alisema kuwa Tanzania ina (simba 15000 waliopo ndani ya mipaka ya Tanzania) nusu  ya Simba wote duniani jambo  ambalo ni la lakujivunia pia nchi ya pili kwa wingi wanyamapori  duniani.

Dkt, Denisi alisema kuwa Hifadhi ya Taifa  ya Serengeti  ndiyo hifadhi yenye Simba bora duniani na katika miaka mitano Simaba wameongezeka kwa kiwango kikubwa baada ya Serikali kuamua kupambana na ujangiri na uwindaji haramu katika hifadhi zote nchini na ndiyo maana Serikali imeamua kuhamisha Simba 20 kuja katika hifadhi za Brigi-Chato.

Simba hao 20 tayari wamewekewa vifaa maalum vya kuhakikisha kila mara walipo kama ni salama lakini pia vifaa hivyo vitasaidia kuwaongoza watalii kujua Simba hoa wapo wapi kwa siku husika ili wakawaone kirahisi.  Dkt. Denisi anasema kuwa mara baada ya simba 20 kufikishwa eneo wanalotakiwa kuachiwa watawekwa kwenye uzio na kuwa chini ya uangalizi wa wataaalam kwa wiki mbili na baadae watakuwa wanaachiwa wachache wachache.

Kwaniaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. More Msua Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori alimshukuru Mkuu wa Mkoa Kagera kukubali kuwapokea Simba hao pia alimhakikishia Mkuu wa Mkoa huyo kuwa Wizara imejipanga kuhakikisha Wanyamapori  wakubwa watao (The Big 5) wataletwa katika Hifadhi ya Taifa ya Brigi-Chato ili kuhakikisha watalii wanapofika ktika hifadhi hiyo wanawaona wanyama hao wote.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo  Saada Malunde akishiriki katika zoezi la kupokea simba 20 alisema wananchi wa Biharamulo wapo tayari kuwalinda wanyamapori hao kwa kushirikiana na TANAPA ili Hifadhi ya Brigi-Chato iweze kushamiri. Hifadhi ya Brigi- Chato ina ukubwa  wa kilometa za mraba 470.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa