• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Wambali Akiwa na Ujumbe Wake Katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kumsalimia Mhe. Kijuu

Imewekwa : January 6th, 2018

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Afanya Ziara Mkoani Kagera Kuona Utendaji wa Mahakama Kanda ya Bukoba

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand L. K. Wambali afanya ziara Mkoani Kagera kukagua mwenendo wa mashauri katika Mahakama kuona kama mashauri hayo yanaendeshwa kulingana malengo yaliyowekwa  ambapo Mhe. Wambali atatembele Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Bukoba, Mahakama ya Hakimu Mkazi, Mahakama za Wilaya za  Karagwe na Muleba pamoja na Mahakama za Mwanzo mbili katika Wilaya hizo.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu akiongea na Jaji Kiongozi Mhe. Wambali alipowasili ofisini kwake kumsalimia leo January 6, 2018 alimweleza Mhe. Jaji Kiongozi kuwa katika Mkoa wa Kagera kuna changamoto katika Wilaya mbili za Kyerwa na Missenyi kutokuwa na Mahakama za Wilaya na kusababisha kesi nyingi kutoka katika Wilaya hizo kupelekwa Bukoba na Karagwe.

Mheshimiwa Wambali katika kueleza lengo kuu la ziara yake Mkoani Kagera alisema kuwa amekuja kuona kama Nguzo kuu tatu zilizowekwa na Mahakama katika utoaji wa haki zinasimamiwa kikamilifu katika Mkoa wa Kagera ambapo Nguzo ya kwanza ni Utawala Bora, Uajibikaji na Usimamizi wa Raslimali Watu.

Katika Nguzo hiyo ya kwanza Mhe. Wambali alisema kuwa Mahakama zinatakiwa kusikiliza kesi za wananchi na kutoa maamuzi kwa muda muafaka mfano Kesi katika Mahakama ya mwanzo haitakiwi kuzidi miezi sita bila kutolewa maamuzi, Mahakama ya Wilaya mwaka mmoja, na Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani miaka miwili.

Aidha, ukumu katika Mahakama ya Mwanzo inatakiwa kutolewa ndani ya siku 90, nakala ya hukumu inatakiwa kutolewa ndani ya siku 21 na mwenendo wa kesi unatakiwa kutolewa ndani ya siku 30.

Nguzo ya pili, ni kuboresha miundombinu ya Mahakama ili watumishi na wananchi waweze kutoa na  kupata huduma za Mahakama katika mazingira yanayoridhisha. Mhe. Wambali pia alimweleza Mkuu wa Mkoa kuwa Mahakama zinendelea kujengwa nchi nzima lakini kwa kutoa vipaumbele hasa katika maeneo yenye tatizo kubwa.

Nguzo ya tatu aliyoitaja Mhe. Wambali ni Mahakama kuimarisha imani ya wananchi juu ya Mahakama hasa watumishi katika Mahakama kuzingatia maadili na kuepukana na vitendo vya rushwa. Mhe. Wambali alisema hilo llinafanyika kupitia matangazo mbalimbali kama vipeperushi, kuwauliza wananchi juu ya huduma za Mahakama wakati wa maadhimisho ya Siku ya Sheria na Kuunda Kamati za Maadili ya Mahakama ambapo Mwenyekiti wake ni Mkuu wa Mkoa katika Mkoa husika.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Mhe. Ferdinand L. K. Wambali amefika Mkoani Kagera tarehe 6 Januari, 2018 na anatarajia kuhitimisha ziara yake mkoani hapa tarehe 9 Januari, 2018 siku ya Jumanne.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa