• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba Mhe. Salvatory Bongole Akitoa Hotuba Yake Katika Kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Sheria Mkoani Kagera

Imewekwa : February 1st, 2018

Mkoa wa Kagera Waadhimisha Kilele Cha Wiki ya Sheria Kwa Wadau Kuchambua Ufanisi wa Matumizi ya Tehama Katika Mahakama

Mkoa wa Kagera waadhimisha kilele cha wiki ya Sheria  kwa wadau mbalimbali kuchambua, kutoa ufafanuzi  na uelewa kwa wananchi juu ya kaulimbiu ya mwaka huu isemayo “Matumizi ya TEHAMA Katika Utoaji Haki kwa Wakati na Kuzingatia Maadili”

Akitoa salamu za Serikali Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu wakati wa kilele cha wiki ya Sheria katika viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba alisema kuwa ni Muhimu sana Mahakama kutumia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ili kuwafanya wananchi wasipoteze muda mwingi Mahakamani badala yake watumie muda huo kufanya shughuliza kiuchumi.

Mhe. Kijuu aliwaomba Viongozi  wa dini kuendelea kuhubiri amani katika nyumba za ibada ili wananchi waendelee  kuwa na upendo na kudumisha amani na kuacha vurugu za kupelekana Mahakamani  ili zibakie kesi au mashauri ya msingi tu na yashughulikiwe na kumalizika kwa wakati.

Pia  Mhe. Kijuu alitoa wito kwa wananchi kuacha kujichukulia sheria mikononi  pia kuheshimu maamuzi ya Mahakama na waache tabia za kukata rufaa za kesi zilizoamuliwa kihalali jambo ambalo linazifanya Mahakama kuwa na msongamano wa kesi na kuchelewesha maamuzi kwa kesi ambazo tayari zilishaamuliwa.

Aidha, Jaji Mfawidhi wa Mahakama  Kuu Kanda ya Bukoba Mhe. Salvatory Bongole alisema kuwa Mpango Mkakati mkuu uliowekwa na  Mahakama wa mwaka 2016 hadi 2020 umejikita katika shabaha kuu sita za TEHAMA Katika Mahakama. Shabaha ya kwanza ni kufunga au ujenzi wa miundombinu ya TEHAMA katika Majengo ya Mahakama.

Pili ni kuwa na Mahakama ya Kielektroniki  (E-Judiciary), Tatu kuwa na mtoa huduma mmoja wa internet ambaye ataziunganisha Mahakama zote nchini, Nne ni kununua vifaa vya Video Conferencing pamoja na mobile recording system kwa Mahakama zilizochaguliwa, Tano kuanzisha mfumo wa kuratibu nyaraka za kielektroniki,  Sita kuanzisha mfumo utakaoratibu raslilimali za Mahakama.  Jaji Bongole alisema kuwa shabaha zote sita zipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji kwa sasa.

Naye Mwanansheria Mkuu wa Serikali Mkoa wa Kagera Hashim Ngole alisema kuanzishwa kwa TEHAMA katika Mahakama kutaleta faida nyingi ikiwa ni pamoja na kupunguza muda wa kushughulikia mashauri mahakamani na kupunguza matumizi makubwa ya karatasi (Paper work), Kurahisisha utumaji wa taarifa kwa wakati na kwa kipindi maalum.

Mhe. Ngole pia alisema kuwa TEHAMA katika Mahakama itarahisisha utaratibu wa kurekodi mienendo ya mashauri Mahakamani kwa kumbukumbu sahihi za baadae kuliko ilivyo sasa. Pia Kuwafanya mashahidi wa kesi kutoa ushahidi mahala papote walipo kwa njia ya Video Conference kuliko ilivyo sasa kuwa lazima shahidi afike mahakamani.

Faida nyingine zilizotajwa za kuanzisha TEHAMA katika Mahakama ni Mawakili kuwawakilisha wateja wao mahakamani bila wao kuwepo, kupunguza mianya ya rushwa Mahakamani. Hukumu, machapisho na sheria mbalimbali kupatikana kwa urahisi katika mitandao ili kuwasaidia Mawakili katika kuendesha mashauri Mahakani.

 Katika Hatua nyingine Mwenyekiti wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (Tanganyika Law Society) Mkoa wa Kagera Wakili Aron Kabunga alishauri kuwa ili kuifanya Mahakama kuwa ya Kielektroniki lazima baadhi ya vifungu vya sheria virekebishwe ili kuruhusu matumizi ya TEHAMA kuwa na ufanisi katika Mahakama.

Vilevile Wakili Kabunga alisisitiza kuwa na tahadhari kubwa kuhusu madhara ya TEHAMA kama udukuzi wa nyaraka kwa njia za mitandao, Vifaa kama kompyuta kuingiliwa na wadudu (Virus) au wataalamu  na kuharibu mfumo mzima na kupelekea nyaraka muhimu kama hukumu au ushahidi kupotea au kubadilishwa kwa matakwa ya upande mmoja.

Maadhimisho ya Kilele cha Wiki ya Sheria Mkoani Kagera yaliadhimishwa katika Viwanja vya Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba na Mgeni Rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa