• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Kagera Kuibua Vipaji Vipya Katika Michezo Mbalimbali Umiseta 2019 Yafunguliwa Rasmi Kuunda Timu Bora ya Kunyakua Ushindi Kitaifa Mtwara.

Imewekwa : May 30th, 2019

Mashindano ya Michezo kwa wananfunzi wa shule za Sekondari UMISETA Mkoa Kagera yafunguliwa rasmi ili kuibua vipaji katika michezo mbalimbali na kuunda timu ya mkoa itakayokwenda kuuwakilisha mkoa katika mashindano hayo  ngazi ya Taifa mkoani Mtwara.

Akifungua mashindano hayo kwaniaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Bw. Isaya Tendega Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji aliwataka wananfunzi wanaounda kambi hiyo kucheza kwa nidhamu kubwa na kuonesha vipaji vyao wakifuata maekezo ya walimu wao ili kuunda timu imara na bora itakayoleta ushindani katika mashindano hayo Kitaifa.

Bw. Tendega aliwataka wanafunzi hao kuwa wazalendo, kwa kuwa wakakamavu, waadilifu kuwa na nidhamu pia uzalendo wanaposhiriki mashindano hayo kwani michezo si ugomvi bali ni upendo na kucheza kwa upendo ndipo kipaji cha mchezaji huonekana vyema zaidi. Pia aliwaasa waamuzi wa michezo yote kuamua bila upendeleo ili kupata vipaji vinavyolengwa vitakavyouwakilisha mkoa vyema kitaifa.

Aidha, katika hotuba yake Katibu Tawala wa Mkoa Profesa Faustin Kamzora aliwaagiza Wakurugenzi Watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuhakikisha idara za michezo katika Halmashauri zao zinawezeshwa kwa vifaa na fedha ili kuendeshea michezo na kukuza vipaji katika mkoa wa Kagera kwani hivi sasa michezo ni ajira.

“Michezo imewasaidia vijana wengi kuepukana na mdawa ya kulevya kama bangi, mirungi, cocaine na mengineyo lazima tuitilie mkazo sana ili vijana wetu wasiharibikiwe. Pili kumbukeni kuwa Michezo ni ajira mfano katika mkoa wetu tunaye mwamuzi wa mpira wa miguu tena mama anachezesha liku ligi kuu ya Tanzania ni kwasababu aliichukulia michezo kwa kipaumbele na amepata ajira ya kudumu sasa.” Alisisitiza Bw. Tendega kwaniaba ya Katibu Tawala Mkoa wa Kagera.

Aidha, Bw. Kepha Elias Afisa Michezo Mkoa wa Kagera ambaye ni meneja wa kambi ya UMISETA katika Shule ya Sekondari Nyakato Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba alisema kuwa kuna jumla ya wananfunzi wanamichezo 640  wavulana wakiwa 341 na wasichana 306  na wanamichezo hao wanashiriki katika michezo ya soka, fani za ndani, kwaya, mpira wa wavu, mpira wa pete, mpira wa mikono na riadha.

Naye Bw. Mbaraka Maya aliyemwakilisha Afisa Elimu Mkoa katika ufunguzi huo wa mashindano ya UMISETA mkoa wa Kagera alisema kuwa Maafisa Elimu wote wa Wilaya wapo katika kambi hiyo ya Shule ya Sekondari Nyakato kusimamia nidhamu ya wanafunzi wanamichezo ili kupata timu bora ya mashindano hayo itakayoleta changamoto katika michezo mbalimbali Kitafa mkoani Mtwara.

Ikumbukwe kuwa Mashindano ya michezo kwa wanafunzi wa Shule za Sekondari UMISETA na Shule za Msingi UMITASHUMTA yaliwahi kusitishwa mwaka 2000 na Waziri aliyekuwa na dhamana ya Michezo wakati huo wa Awamu ya Tatu Mhe. Joseph Mungai na yalirejeshwa kwa majaribio mwaka 2007 na Mhe. Magreth Sitta akiwa waziri mwenye dhamana ya michezo wakati huo.

Mashindano hayo kwa shule za Sekondari UMISETA na Msingi UMITASHUMTA yaliporejeshwa tena mwaka 2007 na yalifanyika majaribio kwa Mikoa mitatu tu ya Dar es Salaam, Morogoro na Tanga na yalifanyikia Kibaha Mkoani Pwani. Aidha, Serikali iliamua kuyarejesha rasmi mashindano hayo mwaka 2009 kwa waraka namba 1 wa mwaka 2009.

Katika Mkoa wa Kagera Mashindano ya wanafunzi kwa shule za Sekondari UMISETA yanafanyika katika Shule ya Sekondari Nyakato Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba ambapo yalianza Mei 25, 2019 na  yanatarajia kukamilika Juni 7, 2019.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa