• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

Imewekwa : March 17th, 2025

Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera (RCC) katika kikao cha dharura imepitisha kwa kauli moja mapendekezo ya Kamati ya ushauri ya Wilaya ya Missenyi ya kubadili jina la Jimbo la uchaguzi la Nkenge ili liitwe Jimbo la Missenyi jina litakalowagusa wananchi wote katika Wilaya hiyo yenye Jimbo la uchaguzi moja.

Kikao hichokilichofanyika Machi 17, 2025 katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera na  kuongozwa na Mwenyekiti wake ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Hajjat Fatma Mwassa kilikuwa na ajenda kuu moja ya kugawa Majimbo na kubadili majina ya majimbo ya uchaguzi katika Mkoa wa Kagera.

Kati ya Majimbo tisa ya uchaguzi yaliyopo mkoani Kagera ni Jimbo moja la Nkenge linalopatikana Wilayani Missenyi lilipendekezwa kubadilishwa jina na kuitwa Jimbo la Missenyi na mapendekezo hayo yaliungwa mkono na wajumbe wote wa kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa kama ilivyopendekezwa na kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Missenyi.

Wakitaja sababu kuu ya kupendekeza kubadilisha jina la Jimbo la uchaguzi la Nkenge  Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Missenyi walisema kuwa jina la Nkenge limekuwa likitumika tu kwa Jimbo lakini hakuna taasisi yoyote ya Serikali au binafsi inatumia jina hilo la Nkenge, lakini pia mawasiliano yote ya Kiserikali yamekuwa yakitumia jina la Missenyi na siyo Nkenge.

Aidha, Katika hoja ya kugawa Majimbo ya uchaguzi  yaliwasilishwa mapendekezo ya kugawanywa kwa Majimbo ya Uchaguzi ya Biharamulo Magharibi na Jimbo la Ngara lakini kutokana na kutokukidhi vigezo vya kugawanywa Majimbo hayo Wajumbe wa kikao walikubaliana baada kupiga kura mara mbili kuwa mchakato wa kuyagawanywa majimbo hayo usitishwe hadi hapo baadae kwa sababu ya kutokidhi vigezo vilivyo wekwa na Tume Huru ya Uchaguzi.

Akifafanua vigezo hivyo Mkuu wa Mkoa Hajjat Fatma Mwassa Mwenyekiti wa kikao alisema kuwa vigezo vikuu ni uchumi mkubwa wa Jimbo la Uchaguzi linalotakiwa kugawanywa, Wingi wa watu wasiopungua 400,000 lakini kati ya majimbo hayo  mawili ya uchaguzi ya Biharamulo na Ngara yaliyopendekezwa kugawanywa hayakizi vigezo hivyo.

Mkoa wa Kagera unayo Majimbo ya uchaguzi jumla Tisa ya Uchguzi ya Bukoba Mjini, Bukoba Vijijini, Muleba Kasikazini, Muleba Kusini, Biharamulo Magharibi, Ngara, Karagwe, Kyerwa na Jimbo la Nkenge linalopendekezwa kubadilishwa jina na kuwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa