• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Kamishna Generali wa Magereza Nchini Ampongeza RC Gaguti Kudumisha Ulinzi na Usalama na Kagera Pia Aguswa na Ushirikiano na Jeshi la Magereza

Imewekwa : July 10th, 2019

Kamishna Generali wa Magereza nchini Tanzania Phaustine Kasike afurahishwa na ushirikiano wa Serikali ya Mkoa wa Kagera chini ya Mkuu wa Mkoa Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti na Jeshi la Magereza mkoani humo namna wanavyoshirikiana kutatua changamoto mbalimbali za Jeshi hilo katika kuweka mazingira bora ya utendaji kazi.

Akiwa ofisini kwa Mkuu wa Mkoa Kamishna Generali Kasike Julai 10, 2019 alipofika kumsalimia Mkuu wa Mkoa Gaguti alimpongeza yeye binafsi pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kwa kudumisha ulinzi na usalama hasa kwa kipindi hiki ambacho sasa mkoa wa Kagera umetulia kwa matukio mbalimbali makubwa  ya utekaji barabarani.

Kamishna Generali Kasike alisema kuwa yupo Mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi hasa kufuatilia maelekezo mahususi yaliyotolewa na kwa Jeshi hilo ya kuhakikisha Jeshi la Magereza linazalisha chakula cha kutosha kuwalisha wafungwa lakini pia ikiwezekana kuzalisha ziada ya chakula kwani nguvu kazi ya kuzalisha chakula hicho ipo ambao ni wafungwa katika Magereza.

“Sisi Jeshi la Magereza Tumeweka mkakati maalumu wa kuzalisha chakula cha kutosha kulisha Magereza yote nchini na katika mkakati huo tulibainisha Magereza kumi nchi nzima ambapo na Gereza la Kitengure la hapa mkoani Kagera lipo kati ya hayo kumi kwani Gereza hilo linazalisha chakula kwa misimu miwili ya vuli na masika.” Alifafanua Jenerali Kasike.

Pia Kamishna Jenerali Kasike alisema katika kuboresha makazi ya Maafisa wa Jeshi la Magereza wanao mpango mkakati wa Kila Gereza kuzalisha tofali hasa zile za kuchoma ili kujenga makazi mapya ya Maafisa na kukarabati miundombinu ambayo tayari imechoka.

Kwaniaba ya wananchi wa Mkoa wa Kagera Mkuu wa Mkoa Gaguti alimshukuru Kamishna Generali Kasike kwa kuamua kufanya ziara Mkoani Kagera kuja kuona changamoto mbalimbali hasa kwa upande wa chakula cha wafungwa na makazi ya Maafisa wa Jeshi hilo la Magereza.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alimhakikishia Jenerali Kasike kuendelea kutoa ushirikiano wa kutosha hasa katika ujenzi wa makazi bora ya Maafisa wa Magereza ili kuboresha zaidi utendaji kazi wa Maafisa hao katika kutekeleza majukumu yao.

Aidha, uongozi wa mkoa utaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Jeshi la  Magereza Mkoani Kagera Kagera katika kuzalisha chakula cha kujitosheleza kwa Wafungwa lakini pia kuzalisha chakula cha ziada kwa Magereza ya nje ya Mkoa kwa kuwa Mkoa wa Kagera unayo fursa nzuri ya kilimo na kupelekea uzalishaji wa chakula kuwezekana kwa mimisimu miwili taofauti.

Mwisho Kamishna Jenerali Kasike alisema kuwa ziara yake ni ya mafanikio makubwa mkoani Kagera kwa jinsi alivyopokelewa na uongozi wa mkoa pia alivyohakikishiwa ushirikiano na Mkuu wa Mkoa Gaguti katika kutatua changamoto mbalimbali za Jeshi la Magereza.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa