• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Nchini Awasili Mkoani Kagera Kwa Ziara ya Kikazi ya Siku Tatu Kutatua Changamoto Mbalimbali za Uhamiaji

Imewekwa : November 13th, 2019

Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala awasili Mkoani Kagera kwa ziara ya kikazi ya siku tatu mkoani hapa ambapo ziara yake itazihusisha Wilaya zote saba za Mkoa huo huku akishughulikia masuala mbaimbali yahusuyo Uhamiaji.

Akiongea na Waandishi wa Habari mara baada ya kupokelewa na Mkuu wa Mkoa ofisini kwake Dkt. Makakala alisema kuwa uwepo wa nchi jirani zinazopakana na Mkoa wa Kagera ni fursa kubwa  ya wananchi kufanya biashara na nchi hizo  mipakani lakini si fursa za uhamiaji haramu usiofuata sheria.

Dkt. Makakala akielezea namna Idara ya Uhamiaji walivyojipanga katika kipindi hiki cha uchaguzi hasa raia wasiokuwa Watanzania kushiriki katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa alisema kuwa kama ilivyo kwenye sheria ya uchaguzi pia uhamiaji wanayo sheria ya uraia kwajili ya kutoa elimu kwa wananchi ambao ni wapigakura na wagombea  kuhusu madhara ya wananchi wasio raia kupiga kura  au kuchaguliwa na wanaendelea kutoa elimu hiyo kwa wananchi.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti akielezea ujio wa Dkt. Makakala alisema amekuja kuongeza nguvu katika kazi ambayo imekuwa ikifanywa na uongozi wa mkoa kwa kushirikiana na Idara ya Uhamiaji kuondoa wahamiaji haramu pia kutoa elimu kwa wananchi kushirikiana na Serikali katika suala zima la uzalendo wa nchi yao.

“Katika kuhakikisha tunakomesha uhamiaji haramu sisi tumefanya kazi kubwa na Idara ya Uhamiaji imekuwa ya msaada mkubwa kwetu tumewabaini wengi na tumewarudisha makwao  kwa kufauata sheria, vilevile tulianzisha Mfumo wa Nyumba Kumi Bora za Usalama ili kuwajengea uwezo wananchi wenyewe kuhakikisha katika maeneo yao hakuna wahamiaji haramu  nahatua zinatakiwa kuchukuliwa kuanzia ngazi ya kaya. Alifafanua Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Ikumbukwe kuwa  Novemba 8, 2019 Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Gaguti  akiwa katika Kijiji na  Kata ya Rutoro Wilayani Muleba alitoa onyo kali kwa wahamiaji haramu na wananchi Watanzania wanaowakaribisha wahamiaji hao kwa kuwasaidia  kupata vibali vya kuishi nchini kuwa mkono wa sheria utawafikia mahali popote watakapokuwa na  watarudishwa  kwao kama walivyoingia hata kama watakuwa wamechuma mali wataziacha zote hapa nchini.

Wito kwa wananchi wa Mkoa wa Kagera ni kutumia fursa za mipaka ya nchi jirani kufanya biashara ili kukuza uchumi wa mkoa wao lakini pia kuhakikisha kuwa hawawakaribishi watu wasiokuwa raia ambao hafuati sheria kutaka kuishi nchini, lakini pia kama kuna raia asiyekuwa Mtanzania na angependa kuishi nchini afuate taratibu na sheria za nchi ili aweze kuishi  kisheria hapa Tanzania.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa