• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Kampeini ya Msaada wa Kisheria Kwa Wananchi wa Kagera Yazinduliwa Rasmi Gymkhana Zaidi ya Wananchi 2000 Kuhudumiwa - RC Gaguti

Imewekwa : July 1st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti azindua rasmi Kampeini ya siku tatu ya Msaada wa Kisheria kwa wananachi wenye kero au migogogro ya Ardhi, Mirathi, Kunyanyaswa kijinsia na kutelekezewa watoto kwa kusikilizwa na kutatuliwa kero zao.

Akizindua Kampeini hiyo Julai 1, 2019 Mkuu wa Mkoa Gaguti baada ya kutemblea ofisi za Wataalam kutoka idara mbalimbali zilizohamishiwa katika Viwanja vya Gymkhana Manispaa ya Bukoba alisema aliamua kufanya utatuzi wa kero za wananchi kwa pamoja kutokana na kero nyingi katika maeneo yaliyotajwa kufika mara kwa mara ofisini kwake kulalamika lakini ufumbuzi wa kero hizo unahitaji idara zaidi ya moja.

“Katika utatuzi huu wa kero za wananchi tukishirikiana na Shirika la MHOLA tumeamua kuleta msaada wa kisheria kwa wananchi kutatua kero za muda mrefu. Pia hapa tunao Wanasheria zaidi ya 15, tunao Maafisa wa Dawati la Jinsia na Upelelezi kutoka Jeshi la Polisi, Maafisa Kutoka TAKUKURU, Ustawi wa Jamii, Idara za Ardhi  pia Ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri za Bukoba na Manispaa ili kuhakikisha kero zote zinatatuliwa.” Alieleza Mhe. Gaguti  

Aidha, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa pia ilihamishiwa katika viwanja hivyo vya Gymkhana ili kero zinazoshindikana kwa watendaji wa ngazi mbalimbali na kutakiwa kusikilizwa moja kwa moja na Mkuu wa Mkoa mwenyewe ambapo Mhe. Gaguti alizisikiliza papo kwa hapo na kuzitolea ufumbuzi au kuelekeza utatuzi wake kwa mamlaka husika.

Hadi kufikia muda wa saa 7:00 mchana wakati Mkuu wa Mkoa Gaguti akiongea na Vyombo vya Habari tayari wananchi 140 walikuwa wamehudumiwa wanaume wakiwa 72, wanawake 68 na kati ya hao 140 wananchi 69 sawa na asilimia 49% walikuwa na kero za ardhi. Wananchi 46 sawa na asilimia 33% walikuwa na kero za Unyanyasaji wa kijinsia na kero nyingizo. Pia kwa upande wa malalamiko ya Mirathi wallijitokeza wananchi 25 sawa na asilimia 18%

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Gerazius Byakanwa alifika katika Viwanja vya Gymkhana kuona wananchi wa Mkoa wa Kagera wanavyopatiwa huduma za Msaada wa Kisheria chini ya uratibu wa Mkuu wa Mkoa na alitoa pongezi kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera namna kero za wananchi zinavyotatuliwa kwa mfumo wa kisasa na wenye ubunifu mkubwa kuliko ilivyokuwa zamani.

“Mtwara tunasikiliza kero za wananchi na kuzitatua lakini si kwa mfumo huu wa kukusanya idara zote husika na kuletwa pamoja kwa siku maalum ili kutatua kero hizo, siwezi kusema kuwa nitamuiga Mkuu wa Mkoa ila nimejifunza jambo kwake. Pia huko nyuma kero za wananchi zilikuwa hazisikilizwi ila kwasasa Serikali ipo karibu na wananchi wake ambao ni jambo jema.”  Alipongeza Mhe. Byakanwa.

Kampeini ya Msaada wa Kisheria kwa wananchi wa Mkoa wa Kagera imeanza Julai Mosi, 2019 na ni Kampeini ya siku tatu mfulrilizo ambapo wananchi zaidi ya 2000 wanatarajiwa kuhudumiwa pia Mkuu wa Mkoa Gaguti anaendelea kutoa wito kwa wananchi ambao wana kero wafike katika viwanja vya Gymkhana Manispaa ya Bukoba ili watatuliwe kero zao.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa