• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Mkoani Kagera - Karagwe

Imewekwa : March 9th, 2017

KAGERA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KWA KUWAINUA WAJANE NA KUWAHIMIZA WAJASILIAMALI KUFIKIA TANZANIA YA VIWANDA

Mkoa wa Kagera waadhimisha Siku ya Wanawake Duniani kwa kuwatia moyo na kuwahimiza  wanawake wanaojishughulisha katika shughuli za ujasiliamali kuongeza juhudi kufikia lengo la Serikali la Tanzania kuwa nchi ya viwanda. Aidha, wanawake wenyewe wamehamasishana kuwasaidia wenzao ambao ni wajane na wenye matatizo hasa ya kukosa makazi kutokana na sababu mbalimbali.

Maadhimisho hayo yaliadhimishwa kimkoa Wilayani Karagwe katika Mji mdogo wa Kayanga na kuhudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo ambayo huadhimishwa  Machi, 8 kila mwaka.

Katika maadhimisho hayo Mkuu wa Mkoa Kijuu alimtembelea Mama Cineth Patrick katika eneo la Omulushaka ambaye ni Fundi Seremala na anamiliki kiwanda cha kutengeneza samani za kisasa zikiwemo sofa. Mama Cineth ameajili vijana wakiwemo wasichana ambao ni mafundi aliowafundisha kazi yeye mwenyewe na anashirikiana nao kutengeneza samani katika kiwanda chake.

Mama Cineth anasema mara baada ya kuhitimu ufundi wa uselemala katika Chuo cha Ufundi Karagwemwaka 2014 aliamua kujiajili mwenyewe ambapo tayari amepata faida ya kazi yake kwani kwasasa anasomesha watoto wake watatu, amejenga nyumba ya kuishi na familia yake na ameweza kujenga vyumba vinne vya kupangisha  ili kuongeza kipato.

Mkuu wa Mkoa baada ya kutembelea na kukagua kiwanda pamoja na samani anazozitengeneza alimshukuru kwa kujituma kuliko hata wananume. Pia alimweleza kuwa viwanda vinavyohimizwa na Serikali kila siku vinaanzia katika viwanda vidogo vidogo na baadae vinakuwa vikubwa. Aidha alimsistiza kuongeza juhudi ili kiwanda chake siku moja kiwe kiwanda kikubwa zaidi ya kilivyo sasa na kutoa ajira zaidi.

Mara baada ya kumtembelea mama Cineth alimtembelea Mama Mjane ambaye nyumba yake ilingushwa na upepo mkali uliombatana na  mvua  tarehe 21/02/2017 na kumfanya mama huyo kukosa makazi na kuishi kwenye hema. Wanawake Wilayani Karagwe wakishirikiana na Mfuko wa Maafa wa Wilaya waliamua kumchangia mama huyo fedha na kuanza kumjengea upya nyumba yake.

Wakati alipofika kwa mama huyo mjane Juliana Novath Kayanga katika kitongoji cha Nsheshe Mkuu wa Mkoa alikuta ujenzi wa msingi unaendelea ambapo alimchangia bati ishirini ili kuunga mkono juhudi za akina mama kwa mama Juliana apate makazi imara ambapo nyumba yake ili ikamilike  itagharimu shilingi 8,700,000/=

Pamoja na michezo na ushuhuda wa akina mama wajasiliamali katika maadhimisho hayo pia wananchi mbalimbali walihamasishwa na kuchangia damu kwa ajili ya wahitaji ambao wapo katika Hospitali mbalimbali na wana uhitaji wa damu ili kunusuru maisha yao.

Katika hatua nyingine akiwahutubia wananchi waliohudhuria katika maadhimisho hayo Mhe. Kijuu aliwaasa wanawake kuchapa kazi kwa bidii kwani wao ni msingi wa mabadiliko ya uchumi kama kaulimbiu isemavyo. Pia aliagiza kila Wilaya kuhakikisha inapambana na wale wote wanaojihusha na madawa ya kulevya kuwakamata na kuwachukuila hatua kali za kisheria.

Kaulimbiu ya mwaka huu inasema “Tanzania ya Viwanda Wanawake ni Msingi wa Mabadiliko ya Uchumi.” Maadhimisho ya Siku ya  Wanawake yalianza kuadhimishwa  tangu mwaka 1911 huko nchini Marekani, wanawake walipoandamana kudai haki zao na tangu haposiku hiyo  huadhimishwa kote duniana tarehe 8 Machi kila mwaka  ili kupima ufanisi wa  matamko mbalimbali ya wanawake duniani.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa