• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Maafisa Kilimo na Ugani ni Mwisho Kukaa Ofisini Sasa Umfika Wakati wa Kutoa Elimu Kwa Wakulima Mashambani – Mkuu wa Mkoa Gaguti

Imewekwa : August 10th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Marco E. Gaguti awaagiza Maafisa Kilimo na Maafisa Ugani kutokaa Ofisini bali wakawatembelee kuwafundisha na kutoa elimu ya kilimo chenye tija wakulima  katika Mkoa wa Kagera wenye fursa ya kustawisha mazao ya aina mbalimbali na masoko ya mazao hayo yapo ya kutosha.

Mkuu wa Mkoa Gaguti aliyasema hayo akifunga Maonesho ya Wakulima ya Nane Nane yaliyoadhimishwa kimkoa katika viwanja vya Kyakailabwa Manispaa ya Bukoba ambapo mara baada ya kutembelea mabanda mbalimbali ya wadau wa kilimo alisema sasa umefika wakati wa Wataalam wa kilimo kuwafuata wakulima na kuwapa elimu katika maeneo yao kuliko wakulima kuwafuata wataalam.

“Ninayo taarifa kuwa Kagera tunavyo viwanda vikubwa tisa lakini vinazalisha chini ya kiwango kutokana na kukosa mali ghafi zinazotakiwa kuzalishwa kutokana na kutopatikana kwa wingi. Sasa umefika wakati wakulima kuachana na kilimo cha mazoea cha kulima ekari kumi na kupata gunia 10 bali mkulima alime ekari moja avune gunia 20 za mazao, pia kuachana na ufugaji wa kufuga ng’ombe kumi na kupata lita 10 za maziwa bali mfugaji afuge ng’ombe mmoja apate lita 20 za maziwa.” Alifafanua Mhe. Gaguti

Mkuu wa Mkoa Gaguti alifafanua zaidi kuwa mkoa wa Kagera unayo fursa kubwa zaidi ya kilimo kwani hali ya hewa na ardhi yake inaruhusu kilimo cha zao lolote kwa hiyo wananchi wanatakiwa kuitumia fursa hiyo kuhakikisha wananlima mazao mbalimbali kwa wingi na masoko ya mazo hayo yapo kwakuwa Kagera inapakana na nchi tano ambazo ni fursa ya masoko ya mazao yanayolimwa.

Aidha, Mkuu wa Mkoa Gaguti aliwahakikishia wananchi katika maonesho hayo kuwa sasa Serikali inafanya upya tathimini ya Vyama vya Ushirika kuhakikisha vinamsaidia mkulima na vinakuwa na nyenzo kubwa ya kuhakikisha mazao ya wakulima yanapata masoko kwa wakati lakini si Vyama hivyo vya Ushirika kushiriki kuwanyonya wakulima.

Katika Hatua nyingine Mwenyekiti wa Maandalizi ya Maonesho ya Nane Nane Mkoa wa Kagera Bw. Isaya Tendega ambaye ni Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Uchumi na Uzalishaji Ofisi ya Mkuu wa Mkoa alisema kuwa changamoto kubwa katika maonesho hayo ni baadhi ya Taasisi muhimu za Serikali kutoshiriki katika maonesho hayo na wananchi wangependa kupata elimu kutoka kwao.

Akizitaja baadhi ya Taasisi hizo Bw. Isaya alisema kuwa ni pamoja na Taasisi ya Bima, Wakala wa Vipimo Tanzania, Wakala wa Majengo, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Wakala wa Barabara Tanzania (TANROAD), Poilsi na Wengineo. Bw. Isaya alisisitiza kuwa Taasisi hizo ni muhimu sana kushiriki katika maonesho hayo kwani zinatoa huduma kwa wananchi na wangependa kupata elimu juu ya huduma zao.

Mkuu wa Mkoa Gaguti akifafanua namna ya kutatua changamoto ya Taasisi mbalimbali sa Serikali kushiriki katika Maonesho ya Nane Nane alitoa agizo kuwa lazima mwakani 2019 Taasisi za Serikali zinazotoa huduma kwa wananchi zishiriki ili kuwaelimisha wananchi kuhusu huduma wanazozitoa ili iwe rahisi kwao kupata elimu juu ya huduma hizo muhimu.

Kaulimbiu ya maonesho ya Nane Nane mwaka 2018 ilikuwa inasema “Wekeza katika Kilimo kwa Maendeleo ya Viwanda” na Mkoa wa Kagera ulikuwa unaadhimisha Maonesho ya Nane Nane kwa mara ya 11 mfurulizo ambapo wadau mbalimbali walishiri na mshindi wa kwanza katika maonesho hayo ni Kampuni ya Kagera Sukari inayotekeleza vizuri sera ya Tanzania ya Viwanda kwa kulima kisasa na kuzalisha Sukari.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa