• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mabaraza ya Ardhi na Nyumba Mkoani Kagera Yaaswa Kutenda Haki Ili Yaaminiwe na Wananchi ni Baada ya Wajumbe Wake Wanne Kula Kiapo Mbele ya RC Gaguti

Imewekwa : April 12th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti awaapisha na kuwaasa wajumbe wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba Mkoani Kagera kutekeleza majukumu yao kwa uaminifu, uadilifu pia kwa kutenda haki na kufuata sheria ili waweze kuaminika kwa wananchi wanaowahudumia.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema hayo April 12, 2019 wakati akiwaapisha wajumbe wanne wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya za Ngara na Karagwe ambapo aliwataka wajumbe hao kujikana wenyewe na kujitoa kikamilifu katika kazi zao ili kutenda haki kwa wananchi.

“Viongozi wengi wanaofanya  kazi katika Mabaraza ya Ardhi na Nyumba Mkoani Kagera wamekosa uhalali kwa wananchi wanaowahudumia kutokana na kutotenda haki, sasa nawaasa ninyi mlioapishwa kuhakikisha mnatekeleza kazi zenu kwa kutenda haki ili muweze kuwa halali kwa wananchi wenu.” Alisistiza Mkuu wa Mkoa Gaguti

Aidha, Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa katika Ofisi yake asilimia 80% hadi 90% ya malalamiko ya wananchi ni kuhusu migogoro ya ardhi, pia alisema kuwa hata katika ziara wilayani au viongozi wa Kitaifa wanapofika Mkoani Kagera malalamiko makubwa ya wananchi ni ya ardhi kutokana na Mabaraza ya ardhi na Nyumba ya Wilaya kutokutekeleza majukumu yake ipasavyo.

Vilevile Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa wananchi wa Mkoa wa Kagera wamekuwa masikini kwa kupoteza fedha nyingi kwasababu ya kufuatilia kesi za ardhi katika Mahakama za chini hadi Mahakama za juu ambapo kama Mabaraza ya Ardhi na Nyumba yangekuwa yanatekeleza wajibu wake vizuri wananchi wasingekuwa wanapoteza fedha zao na muda kutafuta haki hadi Mahakama za juu.

Mwisho, Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa rai kwa Viongozi wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya kutoa elimu kwa wananchi kuliko kujikita sana katika mashauri, pia alisisitiza Mabaraza ya  ngazi za chini mfano ya Vijiji na Kata kufanya kazi zake kupunguza migogoro ya ardhi jambo linalopelekea wananchi kujichukulia sheria mikononi kutokana kutoridhika na maamuzi yanayotolewa na kuufanya mkoa wa Kagera kuwa miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa mauaji na kujichukulia sheria mikononi.

Katika hatua nyingine Jaji Lucia Gamuya Kairo Jaji Mfawidhi wa Mhakama Kuu Kanda ya Bukoba aliwakumbusha wajumbe wanne walioapishwa kutekeleza majukumu yao kwa kutenda haki tena kwa uaminifu na uadilifu ili kutatua na kumaliza migogoro ya ardhi Mkoani Kagera

Jaji Kairo alisema kuwa Mabara ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya hayapo chini ya Mahakama lakini kwasababu yanashughulika na kutoa haki wananchi wanajua kuwa nayo ni sehemu ya Mahakama ambapo alisistiza kuwa kwa miaka minne aliyokaa Kagera ardhi imekuwa na malalamiko mengi na Mabaraza hayo yapo katika nafasi tatu za mwanzo kwa kulalamikiwa na wananchi katika kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Jaji Kairo alisema kuwa Rushwa inapofusha utoaji wa haki na kuwataka wajumbe wasijiingize katika vitendo vya rushwa na kuwakumbusha kuwa Haki iliyocheleweshwa ni sawa na haki iliyopotea na Haki iliyoharakishwa ni sawa na haki iliyopotea ambapo aliwataka wajumbe hao kutekeleza majukumu yao kwa ulinganifu bila kuchelewesha au kuwaisha haki katika maauzi yao.

Wajumbe walioapishwa na Mkuu wa Mkoa Gaguti Aprili 12, 2019 ni Bw. Charles Mbeikya na Bi Christina Mugasha Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ya Ngara, wengine ni Bw. Longino Frederick na Bi Lucletia Shubilo Saulo Balaza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ya Karagwe. Katika Mkoa wa Kagera Kuna jumla ya Mabaraza ya Ardhi na Nyumba manne katika Wilaya za Bukoba, Muleba, Karagwe na Ngara.

Aidha, wajumbe wa Baraza la Ardhi na Nyumba huchaguliwa kila baada ya kipindi cha miaka mitatu na Baraza moja linaweza kuwa na wajumbe sita hadi saba lakini Mwenyekiti wa Baraza anatakiwa kuwa na wajumbe wasiopungua wawili wakati akisikiliza na kuendesha mashauri.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa