• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Waziri Jenista Mhagama akishiriki ujenzi wa Zahanati ya Rwele Kata Kikuru Wilaya ya Kyerwa ikiwa awamu ya tatu ya urejeshaji hali baada ya Tetemeko Kagera

Imewekwa : July 13th, 2017

Waziri Mhagama Asitisha Awamu ya Pili ya Ujeshaji wa Miundombinu ya Huduma za Jimii Baada ya Tetemeko la Ardhi Kagera Septemba 2016

  • Majengo Yakamilika na Kukabidhiwa Kwenye Halmashauri za Wilaya Tayari Kutoa huduma 

Hatimaye Serikali yahitimisha awamu ya pili ya urejeshaji miundombinu ya huduma za jamii iliyoharibiwa na Tetemeko la Ardhi lililotokea Septemba 10, 2016 baada ya kuridhishwa na kazi iliyofanyika kuonekana inaendana na thamani ya fedha zilizotolewa katika maeneo mbalimbali kwenye Halmashauri za Wilaya Mkoani Kagera.

Akiwa Mkoani  Kagera katika ziara ya siku mbili Julai 11 hadi 12, 2017 Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Ajira na Watu Wenye Ulemavu Jenista Mhagama alitembelea miradi mkubwa mitano katika Halmashauri za Bukoba, Karagwe, Kyerwa Misenyi na Manispaa ya Bukoba ambayo imekuwa ikitekelezwa ili kurejesha huduma za jamii baada ya kuharibiwa na Tetemeko mwaka 2016.

Akiwa Wilayani Kyerwa Mhe. Mhagama alitembelea na kukagua ujenzi wa Zahanati mpya ya Rwele inayojengwa katika Kijiji cha Kikuru Kata Kikuru itakayogharimu zaidi ya milioni 125. Wilayani Karagwe pia alitembelaea na Kukagua ujenzi wa wodi mpya ya wazazi, chumba cha kuhifadhia maiti na chumba cha jenereta  katika Kituo cha Afya Kayanga ambapo aliridhika na maendeleo ya ujenzi kulingana na kiasi cha fedha kilichotolewa.

Katika Kituo cha Afya kayanga wodi ya wazazi, chumba chumba cha kuhifadhia maiti na chumba cha jenereta  vitagharimu jumla ya shilingi 170,714,521/= ujenzi utakapokamilika. Aidha, Waziri Mhagama alihaidi kuongeza kiasi cha shilingi 100,000,000/= ili kujenga wodi nyingine katika kituo hicho kutokana na kutoa huduma kwa wananchi wengi. Miradi ya afya ya Kyerwa na Karagwe itakamilika Mwezi Septemba na Octoba 2017.

Baada ya kukagua na kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi Waziri Mhagama alikabidhi majukumu yote ya ujenzi kwenye Halmashauri za Wilaya za Karagwe na  Kyerwa chini ya Usimamizi wa Ofisi ya mkuu wa Mkoa ambapo alisitisha awamu ya pili ambayo usimamizi ulikuwa unafanywa na ofisi yake lakini kwasasa majukumu  yote yamerudishwa kwa Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri na hiyo ndiyo awamu ya tatu ya urejeshaji miundombinu.

Katika Wilaya ya Missenyi Kikosi Kazi cha Jeshi la Wananchi Tanzania kilichokuwa kinajenga Kituo cha Afya Kabyaile kilikabidhi Majengo 11 ambayo yamekamilika tayari kwa kutumika ambapo majengo hayo yalikabidhiwa kwa Katibu Tawala wa Mkoa Bw. Diwani Athuman  naye akamkabidhi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi mbele ya Waziri Mhagama  Viongozi wa Mkoa na Wananchi.

Waziri Mhagama akiongea na wananchi alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi kuhakikisha anamalizia kazi ndogo ndogo ambazo zimebakia na kufikia mwezi Desemba 2017 kazi zote zinatakiwa kuwa zimekamilika ili wananchi wapate huduma kikamilifu. Naye Mwakilishi wa Jeshi la Wananchi Tanzania kutoka Makao Makuu Kanali Sylvester Ghuliku aliwaasa wananchi kuyatunza majengo hayo ili yadumu na kutoa huduma kwajili ya kupata huduma.

Katika Wilaya ya Bukoba Waziri Mhagama alitembelea kituo cha Kulelea Wazee Kiilima na kujionea ukarabati wa majengo ya kituo hicho ambao uligharimu zaidi ya milioni 70 ambapo aliridhishwa na ukurabati huo ambapo aliagiza Mkoa na Halmashauri kuendelea kukiangalia kwa karibau kituoa hicho. Aidha, alimwagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Bukoba kutenga bajeti ya kujenga nyumba za watumishi katika kituo hicho.

Waziri Mhagama pia alishuhudia makabidhiano ya Mabweni mawili katika Shule ya Sekondari Omumwani  kati ya Kikosi kazi cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania na Katibu Tawala wa Mkoa pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba pia na makabidhiano ya shule hiyo iliyokuwa inamilikiwa na Jumuiya ya Wazazi wa Chama cha Mapinduzi na kurudishwa Serikalini na Rais John Pombe Magufuli Januari 2, 2017.

Waziri Mhagama akiwa katika ziara hiyo ujumbe mkubwa alioutoa kwa viongozi na wananchi wa Mkoa wa Kagera ni kutumia vizuri fedha zinazotolewa na Serikali kurejesha miundombinu ya huduma za jamii kwa kuzingatia matumizi na maelekezo ya fedha hizo bila kuzichezea fedha hizo kwani ni za moto na mtu akizichezea moto utamchoma .

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu akitoa pongezi kwa Waziri Mhagama aliishukuru Wizara yake kuwa karibu na uongozi wa Mkoa wa Kagera kuhakikisha Miundombinu ya huduma za jamii  zinarejea tangu Tetemeko lilipotokea Mwezi Septemba 2016. Pia alimhakikishia Waziri Mhagama kuwa miradi yote itaisimamia ikamilike ili iweze kutoa huduma safi kwa wananchi.

Aidha, Mkuu wa Mkoa aliwashukuru wananchi kwa uvumilivu wao tangu Tetemeko litokee hadi sasa na aliwashukuru kwa ushirikiano waliounesha kwa Kikosi Kazi cha Jeshi la Wananchi Tanzania kilichokuwa kinajenga Kituo cha Afya Kabyaile. Pia alikishukuru kikosi hicho kuwa kufanya kazi kwa weledi mkubwa aidha, kuto msaada kwa  wananchi hasa wa huduma za afya na maji safi na salama katika eneo linalozunguka  kabyaile.

Mwisho Mkuu wa Mkoa wa Kagera alimwomba Waziri Mhagama kuusaidia Mkoa katika kufuatilia vifaa vya afya kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kuletwa katika kituo cha Afya Kabyaile ili Majengoi hayo mapya yasiake bila vifaa ambavyo ni vya kisasa jambo ambalo linaweza kupelekea majengo hayo kuharibika kabla ya muda wake.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa