• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mhudumu wa Afya Akitoa Chanjo ya Saratani ya Malango wa Kizazi Kwa Msichana Aliyetimiza Umri wa Miaka 14

Imewekwa : April 23rd, 2018

Mkoa wa Kagera Wazindua Utoaji wa Chanjo Mpya ya Kujikinga na Saratani na Mlango wa Kizazi Kwa Wasichana Waliotimiza Umri wa Miaka 14 

Mkoa wa Kagera wazindua rasmi utoaji wa Chanjo Mpya ya Kujikinga na Saratani ya Mlango wa Kizazi kwa wasichana waliotimiza umri wa miaka ya 14 na uzinduzi huo umefanywa na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu Katika Kituo cha Afya Kaigara Wilayani Muleba Aprili 23, 2018.

Akiwahutubia wananchi na wanafunzi waliohudhuria kituoni hapo kupata chanjo  ya Saratani ya Mlango wa Kizazi Mhe. Kijuu alisema kuwa kila mwaka wiki ya mwisho ya mwezi Aprili huwa ni wiki ya chanjo ulimwenguni, lakini kwa mwaka huu 2018 maadhimisho ya Wiki ya chanjo Serikali imeamua kuanza kutoa chanjo mpya ya kinga ya Saratani ya Mlango wa Kizazi.

Mhe. Kijuu alisema kuwa Serikali inatarajia kutoa chanjo ya kinga ya Saratani ya Mlango wa Kizazi kwa wasichana waliotimiza miaka 14 na waliosajiliwa ambao jumla ni 35,917 kwa Mkoa wa Kagera na chanjo hiyo ya kinga itatolewa bure na Serikali bila mwananchi kuchangia chochote.

“Saratani ya Mlango wa Kizazi ni ugonjwa unaoongoza kwa kuwaua akina mama katika nchi yetu,  Serikali imegharamia chanjo ya kinga ya ugonjwa huo itatolewa bure kwa watoto wetu wasichan waliotimiza umri wa miaka 14 nipende kuwahamasisha wazazi wa watoto kuhakikisha watoto wanachanjwa kujikinga na Saratani ya Mlango wa Kizazi,”  Alisisitiza Mhe. Kijuu

Katika hatua nyingine Mkuu wa Wilaya ya Muleba akitoa salamu za Wilaya alisema kuwa Wilaya ya Muleba imejipanga vizuri kutekeleza zoezi hilo kwa ufanisi kwa kuwahamasisha wananchi ambao ni wazazi na katika Wilaya hiyo ya Muleba  wanatarajiwa kuchanjwa wasichana waliotimiza umri wa miaka jumla 5,911.

Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dk. Siliacus Mtabuzi amabaye ni mwangalizi wa zoezi hilo alisema kuwa alifurahishwa na mwamko wa wasichana katika uzinduzi Kaigara pia Wilaya zote alizopita kuona maandalizi ya  utoaji wa chanjo hiyo aliridhishwa na maandalizi katika vituo ambapo aliupongeza mkoa na kusema kuwa anaona dalili za Kagera kufanya vizuri katika chanjo hiyo.

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera Dk. Thomas Rutachunzibwa alisema kuwa Idara ya Afya imejipanga vizuri kuhakikisha wasichana wote 35,917 watapatiwa chanjo mpya ya kujikinga na Saratani ya Mlango wa Kizazi na tayari timu mbalimbali za ufutailiaji zimeundwa kuhakikisha kila Halmashauri ya Wilaya inafanya vizuri katika zoezi zima  na kutatua changamoto zitakazojitokeza kwenye zoezi.

Angalizo, Mkuu wa Mkoa wa Kagera alitoa angalizo katika uzinduzi huo kwa watu ambao watajaribu kupotosha maana ya zoezi hilo kuwa watachukuliwa hatua kali za kisheria ambapo pia aliwaagiza na Wakuu wa Wilaya ambao ni Wenyeviti wa Kamati za Ulinzi na Usalaama katika maeneo yao kuhakikisha wanashughulika na wote watakaojaribu kupotosha maana ya zoezi la utoaji wa chanjo hiyo.

Chanjo Mpya ya Kujikinga na Saratani ya Mlango wa Kizazi ambayo husababishwa na virusi vijulikanavyo kama Human Papilloma Virus inatolewa kwa wasichana waliotimiza umri wa miaka 14, majaribio ya chanjo hiyo yalifanyika mkoani Kilimanjaro tangu mwaka 2014. Chanjo hiyo inatolewa mara mbili kwanza msichana anapofikisha umri wa miaka 14 pia dozi ya pili ni baada ya miezi sita.

Aidha, zoezi la utoaji Chajo Mpya ya Kujikinga na Saratani ya Mlango wa Kizazi ni zoezi endelevu kwa wasichana watakaokuwa wanatimiza miaka 14 kila mwezi. Kagera chanjo hiyo inatolewa katika vituo 1,182 ambavyo ni vya kawaida vya kutolea huduma za afya, baadhi ya shule zilizochzguliwa na katika baadhi ya maeneo ya kijamii yaliyochaguliwa chanjo hiyo itatolewa kwa njia za huduma za mkoba.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa