• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mkoa wa Kagera Washiriki Katika Kikao Cha Kuboresha Usafirishaji wa Samaki Nje ya Nchi Kupitia Uwanja wa Ndege wa Mwanza

Imewekwa : June 2nd, 2020

Mkoa  wa Kagera washiriki katika kikao cha pamoja  cha kujadili mikakati ya usafirshaji samaki na mazao yake  nje ya nchi kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwanza ambapo kikao hicho  kilichofanyika Jijini Mwanza Juni 1, 2020 kilizishirikisha Wizara tatu za Viwanda na Biashara, Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano,  Mifugo na Uvuvi  pamoja na Mikoa ya Kagera Mwanza na Mara.

Waziri wa  Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe  ambaye aliongoza kikao hicho wakati wa ufunguzi  alisema kuwa lengo la kikao ilikuwa ni  kuondoa vikwazo vyote kwa kushirikisha sekta zote zikiwemo Wizara na mikoa kuhakikisha Samaki na mazao yake kutoka Tanzania yafika kwenye masoko duniani kwa wakati.

Waziri Kamwelwe alisema kuwa wanufaika wakubwa katika usafirishaji wa samaki na mazao yake ni Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Mamlaka ya udhibiti wa Hali ya Hewa pamoja na Mamlaka ya Mapato Tanzania lakini ikiwa ni pamoja na kuongeza ajira kwa wavuvi na kutoa fursa kwa viwanda vya ndani kusindika na kusafirisha  mzigo wa kutosha kwenda nchi za Ulaya.

“Lengo kuu la kutaka kuboresha usafirishaji wa Samaki ni kutaka pia kuongeza bidhaa nyingine za mifugo na kilimo, mfano katika Safari nne ambazo Shirika la Rwanda na Ethiopia yamefanya imebainika kuwa mashirika hayo yanahitaji kiwango kikubwa cha mzigo aidha, mzigo huo uwe wa uhakika”. Alisisitiza Waziri Kamwelwe.

Katika upande wa wasafirishaji au wamiliki wa Viwanda wanaiomba Serikali kupunguza tozo za usafirishaji ili kushindana na washindani wengine katika biashara ya usafirishaji wa Samaki na mazao yake . Mkoa wa Kagera katika Kikao hicho uliwakilishwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti

Kikao hicho kilikubaliana kuchukua hatua  za haraka ili kuhakikisha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa  Mwanza unatoa huduma bora hasa katika usafirishaji wa mizigo na makubaliano hayo ni kama ifuatavyo: Ujengwe uzio kuzunguka Uwanja wa Kimataifa wa Mwanza, Kuweka mpango Mkakati wa kuhakikisha tani 200 za samaki zinazozalishwa kila siku na viwanda vyote nchini zinasafirishwa kupitia uwanja wa Ndege wa Mwanza  badala ya tani 67 tu.

Aidha, wajumbe wa kikao hicho walikubaliana kupanua mnyororo wa thamani katika usafirishaji ili mashirika ya Ndege yapate mzigo wa kutosha hasa katika mazao ya kilimo na mifugo ambapo Wizara za Elimu, Mipango na fedha  pamoja na Kilimo zitashirikishwa katika vikao vijavyo ili kuhakikisha wanakuwa katika mpango mzima wa mnyororo wa thamani.

Mwisho kikosi kazi cha Makatibu Wakuu wa Wizara husika waliagizwa na Kikao kuanza kazi mara moja ili kuhakikisha makubaliano yote yanatekelezwa kwa wakati bila mkwamo wowote.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa