• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mkoa wa Kagera Wazindua Mradi wa Kuleta Mapinduzi ya Kilimo Katika Mazao ya Maharage Mihogo na Mahindi Kumnufaisha Mkulima

Imewekwa : June 28th, 2018

Mkoa wa Kagera wazindua rasmi mradi Tija Tanzania mradi ambao unaolenga kuongeza uzalishaji na Usalama wa chakula pia na kuinua kipato cha wakulima kwenye  mazao matatu ya Maharage, Mihogo na Mahindi katika Halmashauri za Wilaya za Karagwe, Missenyi, Muleba na Kyerwa.

Mradi wa Tija Tanzania unaofadhiliwa na  Shirika la Mapinduzi ya Kijani Afrika (AGRA) unajikita katika mazao matatu yaliyotajwa hapo juu (Maharage, Mahindi na Mihogo) katika kuahakikisha kwamba mkulima kupitia mazao hayo anafundishwa na kuelekezwa kuzalisha kwa ufanisi ili kuongeza uhakika wa chakula, lakini pia kuunganishwa na masoko ya uhakika ili kuuza ziada kwa faida na kuongeza kipato kwenye kaya.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu akizindua mradi huo rasmi Juni 27, 2018 katika Hoteli ya Bukoba ELCT alilishukuru Shirika la AGRA kwa kufadhili mradi wa Tija Tanzania na kusema kuwa sasa utakuwa mradi wa Tija Kagera  kwa kuongeza uzalishaji na uhakika wa chakula pia  na kuinua kipato cha mkulima wa Mkoa wa  Kagera.

“Uzalishaji wetu Kagera kwa mazao ya Mahindi, Maharage na Mihogo bado ni mdogo ambapo tija ya uzalishaji kwa hekta kwa mazao hayo ni wastani wa tani moja ya maharage, tani 2.5 za mahindi na tani 10 za mihogo. Uzalishaji huo ni mdogo mno ukilinganisha na fursa ya kilimo inayopatikana katika mkoa wa Kagera, hivyo tunapopata fursa ya kuwa na mradi kama Tija Tanzania ni lazima tuitumie vizuri.” Alisisitiza Mhe. Kijuu

Naye Bwana Thiery Ngonga mwakilishi wa Rais wa AGRA kutoka Nairobi nchini Kenya alisema nchi ya Tanzania ni moja wapo kati ya nchi kumi na moja zinazofadhiliwa na Shirika la Mapinduzi ya Kijani Afrika (AGRA) lakini bado Tanzania ilikuwa haifanyi vizuri katika kilimo na kusema kuwa sasa wameweka mkakati wa kuhakikisha Tanzania inafanya vizuri katika mazao ya Mahindi, maharage na Mihogo kupitia Mkoa wa Kagera.

Mradi wa Tija Tanzania tangu uanze Mkoani Kagera sasa umetimiza miezi sita na unatarajia kuwafikia wakulima 200,000 ambapo Mkuu wa Mkoa Mhe. Kijuu alisema mradi huo ni lazima kuwafikia wakulima zaidi ya hao kwa kuwapatia mbegu za kisasa za Mahindi, Maharage na Mihogo ili kuongeza tija katika uzalishaji wa mazao hayo.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa