• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mkuu wa Mkoa Awaagiza TRA Kutofunga Maduka ya Wafanyabiashara Mkoani Kagera Badala Yake Waelimishwe Ili Kulipa Kodi ya Serikali

Imewekwa : January 12th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti awaagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Kagera (TRA) kuanzia Januari 11, 2019 kuacha tabia za kufunga biashara za wananchi kwasababu ya kodi badala yake wajikite katika kutoa elimu na kuwaelimisha wafanyabiashara kulipa kodi kwa utashi bila kushurutishwa pia waweke mkakati wa kuwapata walipakodi wapya.

Maagizo hayo yalitolewa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Gaguti katika kikao cha Baraza la Wafanyabiashara kilichofanyika katika Ukumbi wa Manispaa ya Bukoba Januari 11, 2019 ambapo aliwaita wafanyabiashara hao kuwasikikiliza kero zao ili kuboresha ulipaji wa kodi katika Mkoa wa Kagera ikiwa ni pamoja na kufikia malengo ya ukusanyaji wa kodi kwa mwaka 2018/2019 kwa asilimia 100%.

Kabla ya Mkuu wa Mkoa kutoa maagizo hayo aliwapa nafasi wafanyabiashara kuchangia namna bora ya kuhakikisha kodi inakusanywa kwa asilimia 100% katika Mkoa wa Kagera na kuhakikisha wafanyabiashara wote wanafikiwa ili kodi rafiki ilipwe katika mazingira mazuri ya kufanya biashara bila bughudha zozote.

Wafanyabiashara waliopata nafasi ya kuchangia katika kikao hicho walilalamika juu ya utendaji kazi wa  Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuwa wanakusanyatu kodi bila kutoa elimu na hawajengi mazingira mazuri yakuwasikiliza wafanyabiashara ili walipe kodi kwa utashi hasa katika Mkoa wa Kagera jambo ambalo limepelekea wafanayabisahara wengi kufunga biashara zao.

Mara baada ya kuwasikiliza Mkuu wa Mkoa Gaguti alisema kuwa anataka katika Mkoa wa Kagera kuwe na mazingira mazuri ya wafanyabiashara kufanya biashara zao  na kulipa kodi bila kushurutishwa na kila mfanyabiashara atambuliwe ili kuwa na takwimu sahihi za wananchi wote wanaojishughulisha na biashara.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alitoa siku kumi na nne kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa kuwatumia Viongozi na Watendaji katika ngazi za Kata hadi Vijiji kuwatambua wafanyabiashara wote wawe wakubwa au wadogo ili kuwe na takwimu sahihi ya mkoa kuhusu wananchi wanaojishughulisha na biashara kwani  katika Mkoa wa Kagera ulipaji kodi ni asilimia 0.4% tu.

Aidha, Mkuu wa Mkoa Gaguti aliitaka TRA Mkoa wa Kagera kutanua wigo katika kukusanya kodi hasa kodi za majengo na ardhi. Pia aliwataka wafanyabiashara kuwa wakweli katika kutoa takwimu zao za biashara ili wasikwepe kodi na wala wasionewe. Mwisho Mhe. Gaguti aliitangaza tarehe 25 hadi 30 Machi, 2019 kuwa itakuwa wiki ya Kagera na kuwaomba wananchi katika Sekta zote kushiriki kuutangaza Mkoa wa Kagera katika wiki hiyo.

Katika hatua nyingine Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Prof. Faustine Kamuzora aliyehudhuria kikao hicho aliwahakikishia Wafanyabiashara kuwa sasa uongozi wa mkoa umejipanga kuondoa vikwazo vyote vinavyorudisha juhudi za wafanyabiashara kusonga mbele ambapo alisema kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inataka kuona kila mwananchi anatajirika katika nchi yake mahali popote alipo.

Profesa Kamuzora alisema kuwa atahakikisha anaimarisha Mabaraza ya Wfananyabiashara ya Wilaya na Mkoa ili kuhakikisha Sekta binafsi inashirikiana na Serikali kikamilifu katika kuchumi wa Mkoa na Taifa kwa ujumla

“Jana wakati nimefika hapa mkoani niwauliza wenzangu kuwa mkoa wetu hivi leo unacheza ngazi gani ya ligi nikaambiwa unacheza ndondo cup, wakati ule sisi Kagera ndiyo tulikuwa tunawika na kucheza Premiere League lakini sasa Ndondo? Hapana! Jambo hili inaenda mbali hadi kwenye maendeleo sisi hatutakiwi kuwa ndondo tunatakiwa Premiere.” Alisissitiza Katibu Tawala wa Mkoa Prof. Kamuzora

Mara baadaya kikao cha Baraza la Biashara la Mkoa wa Kagera kumalizika Mkuu wa Mkoa na Ktibu Tawala wa Mkoa pamoja na viongozi wengine walitemblea baadhi ya Wafanyabiashara katika Mtaa wa One Way na Soko Kuu Manispaa ya Bukoba kusikiliza Changamoto wanazokumbana nazo ili kuzitafutia ufumbuzi na kuweka mazingira rafiki ya kufanya biashara na kulipa kodi stahiki kwa utashi.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa