• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mkuu wa Mkoa Awaapisha Wajumbe wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Bukoba Ili Kupunguza Migogoro ya Ardhi Katika Mkoa a Kagera

Imewekwa : May 5th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu amewaapisha wajumbe wanne wapya wa Baraza la Aardhi na Nyumba la Bukoba na kukamilisha wajumbe sita wanaotakiwa katika Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya ili kuongeza ufanisi katika baraza na kuondoa migogoro ya ardhi mkoani Kagera.

Akiwaapisha ofisini kwake Mkuu wa Mkoa Mei 4, 2017 aliwaasa wajumbe hao kuzingatia miiko ambayo imo katika Kanuni za Mahakama za Migogoro ya Ardhi, Tangazo la Serikali namba 174 ya mwaka 2003 ambazo ni; Moja, Mjumbe wa Baraza awe mtu mwenye kujishimu na heshima yake ionekane kwake na kwa Baraza.

Pili, Aishi na aonekane kuwa ni mtu asiye na upendeleo wa aina yoyote na waadawa (Pande zinazoshitakiana)  wakimuona waondoe shaka kuwa ni mtu mwenye kuweza kupendelea. Tatu, Asishiriki kutoa maamuzi au kusikiliza kesi yoyote inayomhusu yeye binafsi au mtu yeyote katika familia yake. Nne, Ajue mipaka ya kazi yake na kwa namna yoyote asijaribu au kuonyesha umma kuwa yeye anafanya kazi za Mwenyekiti.

Tano, Mjumbe wa Baraza wakati wote awe msiri kuhusiana na kesi ambazo bado kutolewa uamuzi. Harusiwi kusema nje ya Baraza, chochote kinachohusu undani wa kesi ambayo bado haijaamuliwa. Sita, Hairuhusiwi kuwa na urafiki na upande wowote katika kesi inayoendelea kusikilizwa. Saba, Ajiepushe kuzungumza au kufanya mawasiliano yoyote na wadaawa katika eneo la Baraza na kwa hali yoyote haruhusiwi kutoka nje ya jengo la Baraza na kwenda kuzungumza na wadaawa au jamaa zao kabla au baada ya saa za kazi.

Nane, Mjumbe haruhusiwi kuwa wakili wa upande wowote katika kesi, haruhusiwi kutoa ushauri au kuwaandikia wadaawa kitu chochote.Tisa, Awahi na kuhudhuria katika vikao kama itakavyokuwa imepangwa na Mwenyekiti na asikose kuhudhuria mfululizo wa vikao kwa kipindi kinachozidi mwezi mmoja bila sababu ya kuridhisha.

Kumi, Mjumbe asimshawishi Mwenyekiti wa Baraza ili apangiwe kuketi katika kesi fulani. Kumi na Moja, Baada ya kukamilika kesi yoyote, mjumbe atatoa maoni yake kwa maandishi bila kuchelewa. Mwisho Mjumbe asipokee au kuomba zawadi kama hongo au takrima kutoka upande wowote wa waadawa.

Akitoa shukrani Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya ya Bukoba Mheshimiwa Rogate Assey alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa  kuwaapisha wajumbe pia aliwasistiza wajumbe hao walioapishwa kuzingatia miiko na kuzingatia viapo vyao katika kutekeleza majukumu yao.

Mhe.  Assey alimweleza Mkuu wa Mkoa kuwa Mkoa wa Kagera ni mkoa wenye migogoro mingi ya ardhi lakini kutokana na umakini katika utendaji wa Baraza la ardhi na Nyumba la Bukoba umeimarika na kupitia Baraza hilo migogoro mingi ya ardhi imetatuliwa kwa kiwango kikubwa, mlundikano wa Kesi umepunguzwa sana aidha, malalamiko na kero za wananchi kuhusu ardhi zimetatuliwa.

Pia alitoa rai kwa wajumbe kuwa hawaruhusiwi kushawishi kwa njia yoyote isipokuwa watekeleze wajibu wao kulingana na kanuni na taratibu za sheria na kuzingatia miiko waliosomewa na Mkuu wa Mkoa.

Wajumbe walioapishwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera ni Bw. Nestory Makwaya, Bw. Henry Mutayanga, Bi Fortunata Rutabanzibwa na Bi Leonada Mpanju. Katika Mkoa wa Kagera kuna Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya Manne ambayo ni Bukoba, Muleba, Ngara na Karagwe. Aidha Baraza la Ardhi na Nyumba la Wilaya Karagwe linahudumia pia Wilaya ya Kyerwa. Wajumbe wa Mabaraza hayo wanachaguliwa na kudumu kwa kipindi cha miaka mitatu na wanaruhusiwa kuteuliwa zaidi ya muhula mmoja.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa