• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

MKUU WA MKOA KAGERA

Imewekwa : February 14th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Kagera kuinusuru Misitu ya Hifadhi ya Biharamulo, Nyantakala Wilayani Biharamulo na Msitu wa Hifadhi wa Rwiga Wilayani Muleba ambayo imeharibiwa kwa kiwango kikubwa na shughuli za kibinadamu ambazo ni kilimo, ufugaji, ukataji wa mbao na uchomaji wa mkaa katika misitu hiyo.

Meja Jenerali Mstaafu Salum Mstafa Kijuu Mkuu wa Mkoa wa Kagera alitembelea Misitu hiyo ya Hifadhi za Taifa tarehe 30 hadi 31 Januari, 2017 na kujionea uharibifu mkubwa katika misitu hiyo unatokana na shughuli za kibinadamu zinazofanyika kinyume cha sheria.

Mhe. Kijuu alishuhudia eneo la Msitu wa Hifadhi wa Biharamulo katika Kijiji cha Kabale  Kata Rusahunga mita chache kutoka barabara kuu iendayo Dar es Salaam kunaendeshwa kilimo cha mpunga na mahindi katika chanzo cha maji na kupelekea uhaba mkubwa wa maji kutoka katika chanzo hicho kwa sababu ya umwagiliaji unaofanyika kumwagilia mazao hayo.

Katika Misitu hiyo ya Biharamulo na Nyantakala shughuli kuu zinazoendeshwa ni kilimo cha mpunga na mashamba makubwa ya mahindi pia na uchomaji wa mkaa ambapo imepelekea miti mingi kukatwa na kuacha misitu hiyo ikiwa wazi wakati ikiwa ni kinyume cha sheria.

Mkuu wa Mkoa alishuhudia baadhi ya wananchi wakiwa wanaendelea na kilimo ikiwa ni pamoja na kufyeka miti kwa ajili ya kuandaa mashamba katika misitu hiyo. Aidha, imefikia hatua baadhi ya wananchi wameanza kuwakodisha wananchi wenzao ardhi ya kulima katika misitu hiyo ya hifadhi na wanawatoza fedha.

Katika Msitu wa Hifadhi wa Rwiga Wilayani Muleba uharibifu mkubwa unatokana na ukataji miti kwaajili ya uchomaji wa mkaa na ukataji wa mbao ambapo ukiangalia katika maeneo yaliyopo karibu na barabara utaona miti lakini katikati ya msitu uharibifu ni mkubwa sana jambo linalihashiria kuwa kama hatua hazitachukuliwa msitu huo unaweza kuisha ndani ya muda mfupi ujao.

Kutokana na uharibifu huo mkuu wa mkoa wa Kagera alitoa maagizo sita kwa Halmashauri za Wilaya za Biharamulo na Muleba pamoja na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kuwa; Kwanza,  kuanzia sasa Halmashauri hizo zishirikianae na Wakala wa Huduma za Misitu katika kufanya doria za mara kwa mara kuhakikisha katika misitu hiyo hakuna shughuli za kibinadamu zinazoendelea.

Pili, kufyeka mazao yote yaliyopandwa katika chanzo cha maji eneo la Kijiji Kabale kata ya Nyakanazi Wilayani Biharamulo ili kukitunza chanzo hicho amabacho kinamwaga maji yake katika Ziwa Victoria pia na maji yake kutumika kuwasaidia wananchi katika matumizi ya kawaida.

Tatu, Wananchi wote waliolima katika Misitu ya Hifadhi ya Taifa watambuliwe mara moja na kuandkiwa barua ya kuacha mara moja kuendesha shughuli za kilimo katika misitu hiyo. Aidha Mkuu wa Mkoa aliwaruhursu wananchi hao kuvuna mazao yao ambayo wamelima katika misitu hiyo  na mara baada ya kuvuna wasiruhuswe tena kulima isipokuwa wapande miti ya asili kuirejesha ile waliyoikata.

Nne, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania waandike vibao vikubwa vinavyoonyesha kuwa hairusiwi kufanya shughuli zozote za kibinadamu katika Hifadhi za Misitu za Taifa. Pia watoe eimu kwa wananchi wanaozunguka katika hifadhi hizo kueleza umuhimu wa kuitunza misitu hiyo.

Tano, zifanyike operesheni za mara kwa mara  katika misitu hiyo ili kuliinda na uharibifu wa shughuli za kibinadamu jambo amabalo linapelekea hali ya hewa kubadika na kuleta majanga kama ukame kwasababu ya kukata miti hovyo.

Sita, Halmashauri za Wilaya za Biharamulo na Muleba  ziliagizwa kuweka vizuizi vya barabarani vya kustukiza mara kwa mara ili kukamata mkaa unaobebwa na Baiskeli na pikipiki mara baada ya magari kuwa yanakamatwa mara kwa mara na ikaanza kutumika mbinu ya kutumia pikipiki, pia kuwakamata wafanyabiashara wa mkaa wote ambao hawana leseni za biashara hiyo.

Angalizo; Mkuu wa Mkoa Mhe. Kijuu alitoa angalizo kwa viongozi wa ngazi zote katika maeneo hayo na watumishi wananohusika na utunzaji wa Misitu ya Hifadhi ya Taifa kuwa hatasita kuchukua hatua kali ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria na kuwafukuza kazi kwa yeyeyote ambaye atalichukulia suala hilo kimzaa bila kutimiza wajibu wake.

Bi Hafsa Galitano Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo alimshukuru sana Mkuu wa Mkoa kwa kuingilia kati suala hilo la uharibifu wa Misitu ya Biharamulo na Nyantakara na alisema Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ndiyo waliopelekea misitu hiyo kufikia kiwango hicho cha uharibifu kutokana na migongano wao na Halmashuri.

“Mkuu wa Mkoa nakushukuru sana Wakala wa Huduma za Misitu ndiyo waliotufikisha hapa, lakini kwa maagizo yako Mkuu sisi tupo tayari kushirikiana kikamilifu nao na kuanzia sasa hatutakubali misitu yetu iharibiwe tena. Alimalizia Bi Hafsa Galiatano.

Naye Kaimu Meneja Wakala wa Huduma za Misitu Kanda ya Ziwa Bw. Hamza Omari alisema kuwa ofisi yake itashirikiana na Halmashaurikikamilifu katika  kuilinda Misitu ya Hifadhi. Aidha, alisema kuwa baada ya Ofisi yake kusaini randama ya makubaliano na Ofisi ya Rais TAMISEMI hakuna tena mkanganyikokati ya ofisi yake  na Halmashauri.

Wito, kutokana na tabia nchi kubadilika duniani kote na hasa katika mkoa wetu wa Kagera ambako tumekuwa tukipata mvua karibu kwa mwaka mzima lakini mwaka 2016 hali ya ukame imeukumba mkoa wetu wa Kagera pia na nchi nzima, wananchi tunao wajibu mkubwa wa kuhakikisha tunalinda misitu yetu ya hifadhi ili kulinda mazingira.

Kwa upande wa mifugo Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Kijuu alisema utaratibu unaandaliwa wa kuondoa mifugo yote katika Misitu na Mapaori ya Hifadhi za Taifa na ukikamilika Serikali itatangaza jinsi ya zoezi la kuondoa mifugo hiyo litakavyofanyika .

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa