• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mkuu wa Mkoa Kagera Awashauri SUMA JKT Kutekeleza Miradi ya Serikali Kwa Gharama Ndogo na Kuikamilisha Kwa Wakati

Imewekwa : September 19th, 2019

Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli inafanya kazi usiku na mchana kuwahudumia wananchi wake hasa kusogezea karibu huduma za kijamii kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo katika mikoa, Wilaya hadi vijiji.

Katika kuhakikisha kuwa miradi ya kutolea huduma kwa wananchi inasimamiwa na kutekelezwa kwa viwango stahiki ili itoe huduma iliyokusudiwa pia Serikali imekuwa ikiboresha  mazingira ya watendaji wake wanaosimamia miradi hiyo ya maendeleo kwa kuwajengea miundombinu bora inayowawekea mazingira bora pia ya kutekeleza majukumu yao ikiwemo ofisi na makazi yao.

Miradi hiyo ya Serikali yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni mbili (2) katika Mkoa wa Kagera ni pamoja na ujenzi wa  Ofisi za Wakuu wa Wilaya mpya tatu za Biaharamulo, Muleba na Kyerwa, ujenzi wa nyumba ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Kyerwa, pia  ujenzi wa ofisi tano za Maafisa Tarafa katika Wilaya za Kyerwa, Biharamulo, Karagwe, Muleba na Bukoba vijijini.

Akikagua miradi ya ujenzi wa Ofisi za Wakuu wa Wilaya Biharamulo na Muleba Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti Septemba 18, 2019 aliridhishwa na viwango pia ubora wa majengo hayo mawili yanayoendelea kujengwa  na kampuni ya SUMA  JKT na kusema kuwa majengo hayo yanaonesha thamani halisi ya kiasi cha fedha zilizotumika.

Katika ukaguzi huo Mkuu wa Mkoa Gaguti alito wito kwa Kampuni ya ujenzi ya SUMA JKT ihakikishe inaendela kutekeleza miradi yake kwa ubora unaotakiwa lakini pia ikamilishe miradi iliyopewa kwa wakati bila visingizio vyovyote vinavyoweza kuchelewesha miradi hiyo kukamilika kwa muda na wakati wakati uliopangwa au matarjio ya Serikali.

Pili, Mkuu wa Mkoa Gaguti aliishauri Kampuni hiyo ya SUMA JKT kuona namna bora ya kupunguza gharama zake za ujenzi na kutekeleza miradi mingi ya Serikali ikiwa yenye viwango kwasababu nayo pia ni Kampuni ya Serikali haitakiwi kutengeza faida kubwa katika miradi. Mhe. Gaguti aalitoa mfano wa ujenzi wa vituo vya afya na hospitali za wilaya zilizojengwa na fedha kidogo lakini kwa viwango na kukamilika kwa wakati.

“Mimi ni Mwananjeshi kama ninyi na hii Kampuni ya SUMA JKT ambayo na mimi ni mhusika lakini lazima sisi tuwe wa mfano kwa makampuni mengine, kwa kutekeleza miradi ya Serikali kwa gharama ndogo lakini yenye viwango na hapo tutapata kazi nyingi za Serikali na tukumbuke kuwa huo ni uzalendo tunatakiwa kutengeneza faida kidogo kwani hatufanyi biashara.” Alisisitiza Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Serikali ya Awamu ya Tano tayari imetoa  fedha za ujenzi za ofisi za Wakuu wa Wilaya za Biharamulo shilingi milioni 295, Muleba shilingi milioni 690, Kyerwa shilingi milioni 541. Ujenzi wa nyumba ya Katibu Tawala Kyerwa shilingi milioni 159, ujenzi wa ofisi za Maafisa Tarafa tano shilingi milioni 326, ujenzi wa miundombinu hiyo upo katika hatua mbalimbali za ukamilishwaji.

Aidha, katika mkoa wa Kagera Serikali imetoa fedha za kutekeleza pia miradi ya kutolea huduma za jamii na utekelezaji wake unaendelea, Serikali ilitoa shilingi bilioni 4.5 za ujenzi wa Hospitali za Wilaya za Bukoba (vijijni), Karagwe na Kyerwa tayari hospitali zimekamilika. Serikali ilitoa shilingi milioni 169 za upanuzi wa wodi ya wazazi na kujenga vyumba viwili vya upasuaji katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Kagera,  ujenzi upo katika hatua za mwisho kukamilika ili kuanza kutoa huduma kwa wananchi akina mama wajawazito.

Vilevile katika kusogeza karibu huduma kwa wananchi Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais John Magufuli ilitoa shilingi bilioni 5.9 za ujenzi wa vituo 14 vya afya katika mkoa wa kagera ambavyo vimejengwa na kukamilika na tayari vinatao huduma kwa wananchi wa Kagera. Wito kwa wananchi ni kuendelea kushirikiana na Serikali kutekeleza miradi ya maendeleo pia kuitunza miradi hiyo ili idumu na kuendelea kutoa huduma stahiki.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa