• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Aridhishwa Namna Waandishi na Vyombo Vya Habari Vilivyoshiriki Kuitangaza Wiki ya Uwekezaji Kuvutia Wawekezaji

Imewekwa : August 29th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti ashukuru na kutoa vyeti vya ushiriki kwa  Waandishi wa Habari na vyombo mbalimbali vya Habari Mkoani Kagera(Redio za Mkoani Kagera) kwa namna vilivyojitoa katika kuhakikisha Wiki ya Uwekezaji inafanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Akizungumza na Waandishi, Wahariri na baadhi ya wamiliki wa Vyombo vya habari Mkoani Kagera ofisini kwake Agosti 29, 2019 Mhe. Gaguti alisema anatoa shukrani kubwa kwa kila mwandishi na vyombo vyote vilivyoshiriki Wiki ya Uwekezaji Kagera kwa kujitoa kikamilifu kuitangaza wiki hiyo na kuhakikisha inafanikiwa.

“Kupitia fursa hii nawashukurua sana wote lakini niseme tu kuwa sasa kazi ndiyo imeanza kwani baada ya kufungua milango na madirisha ya mkoa wetu katika uwekezaji tutakuwa na mipango mingi ya kukaa na wawekezaji kuona namna gani uwekezaji unafanyika niombe tuendelee kushirikiana na kutangaza kwa nguvu zaidi juhudi hizi ili tufikie tunapopahitaji.” Alishukuru na kusisitiza Mhe. Gaguti

Naye Katibu wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Kagera na Mwandishi wa Gazeti la Mwananchi Bw. Phinias Bashaya kwaniaba ya waandishi waliohudhuria alimshukuru Mkuu  wa Mkoa na uongozi wote kwa kuwashirikisha waandishi wa habari kuanzia maandalizi hadi kilele cha Wiki ya Uwekezaji Kagera ikiwa ni pamoja na waandishi kupatiwa banda maalum la kuchakatia habari zao wakati wote wa Wiki ya Uwekezaji Kagera.

Bw. Bashaya pia alsema kuwa kupitia Wiki ya Uwekezaji Kagera Waandishi wa habari walipata fursa mbalimbali ikiwemo  fursa ya kwenda katika Mgodi wa STAMIGOLD Wilayani Biharamulo kupata mafunzo ya siku tatu kujifunza namna Mgodi huo pekee nchini unavyoendeshwa na Watanzania Wazalendo baada ya kuendeshwa na wazungu kipindi cha miaka ya nyuma.

Mkoa wa Kagera tayari umeanza kunufaika na Wiki ya Uwekezaji iliyofanyika tarehe 12 hadi 17 Agosti, 2019 kwani Kampuni ya Chai ya Kagera Tea imepata soko la chai nchini Rwanda, Kampuni ya Hirwa  Group Ltd ya utengezaji wa Akandi Beverages imepata soko la kuuza bidhaa hizo tani 10 kila mwezi nchini Rwanda, Wafanyabiashara wa Dagaa Wilayani Muleba wamepata soko la kusafirisha tani 30 za dagaa kila mwezi nchini Rwanda.

Fursa nyingine ni ujenzi wa masoko ya kimkakati na maghara katika mipaka ya Rusumo na Kabanga Wilayani Ngara  ambapo Mohamed Dewij na Kampuni yake ya Mohamed Enterprises tayari wameonesha nia, Muhoja Kabaru  wa Kahama Oil Mills Company Ltd tayari ameonesha nia ya kuanzisha kilimo cha alizeti na kujenga kiwanda cha kusindika alizeti hizo pia na wawekezaji wengine wengi wanaendelea kuonesha nia katika fursa mbalimbali, Kagera inasonga mbele.

 

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa