• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Mamlaka za Serikali za Mitaa
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Maji
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kulia Akimpoza Daktari Bingwa Kwa Kutoa Huduma Kwa Wananchi wa Kagera

Imewekwa : October 6th, 2017

Wananchi Wajitokeza Kwawingi Kunufaika na Huduma za Madaktari Bingwa Mkoani Kagera

Uongozi wa Mkoa wa Kagera wafanikisha zoezi la kutoa huduma ya afya ya Madaktari Bingwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa mjini Bukoba na kuwahudumia wananchi 3146 waliokuwa na magonjwa yaliyowasumbua kwa muda mrefu na yalihitaji huduma za kibingwa.

Katika huduma hiyo iliyokuwa imekusudiwa kutolewa kwa siku saba kuanzia tarehe 18 hadi 24 Septemba, 2017  kutokana na wingi wa wananchi wenye matatizo iliongezwa siku hadi tarehe 28 Septemba, 2017 ambapo wananchi walikuwa na matatizo mablimbali ya kiafya 5700 walijitokeza kuhudumiwa.

Akitoa taarifa mara baada ya zoezi hilo Mganga  Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa Kagera Dk. John Mwombeki alisema wananchi walijitokeza kwa wingi juu ya makadirio yao ya awali jambo ambalo lilipelekea baadhi ya wagonjwa zaidi ya 2000 waliojiandikisha kutowaona Madaktari Bingwa.

Dk. Mwombeki alisema kati ya wananchi 5700 waliojiandikisha ni 3146 walioonwa na Madaktari Bingwa na kuhudumiwa katika maganjwa ya Makoromeo, Sikio na Pua, Macho, Meno, Magonjwa ya wakinamama, Magonjwa ya ndani, Mifupa, Magonjwa ya watoto na Magonjwa ya mfumo wa mkojo kwa wanaume.

Aidha, kati ya wagonjwa 3146 walioonwa na Madaktari Bingwa  wagonjwa 446 walifanyiwa upasuaji mkubwa. Gharama za kuwaona Madaktari Bingwa hao ilikuwa ni Shilingi 5000 kujiandikisha na shilingi 30,000 kwa wagonjwa ambao walishauriwa kufanyiwa upasuaji.

Akizungumzia zoezi hilo lilivyofanikishwa  Mganga Mkuu wa Mkoa Dk. Thomas Rutachunzibwa alisema zoezi hilo lilifanikiwa kutokana na kufunga mfumo wa mapato katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera na kuanza kukusanya kiasi kikubwa cha fedha ambazo zilizopelekea kusogeza huduma hiyo karibu na wananchi wa Mkoa wa Kagera.

Pia katika zoezi hilo lililofanyika kwa siku kumi kiasi cha shilingi milioni 34,886,338 taslimu zilikusanywa pamoja na wagonjwa 1,010  kati ya 3,146 walipata huduma za matibabu na kulipia huduma hizo kwa njia ya Bima ya Taifa (NHIF) na Bima za Mashirika mengine kama AAR, TANESCO, NSSF na STRATEGES.

Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Kamishina Diwani Athumani akizungumzia zoezi hilo alisema kuwa jukumu la Serikali ni Kusogeza huduma za kijamii karibu na wananchi, pia alisema kuwa  baada ya kupokea ombi la kuleta huduma za Madaktari  Bingwa Mkoani Kagera  kutoka kwa Mganga Mkuu wa Mkoa alihakikisha kuwa vifaa na miundombinu yote iliyohitajika inakamilika ili Madaktari Bingwa hao waweze kutekeleza majukumu yao ipasavo.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu mara baada ya kukagua zoezi hilo la Madaktari Bingwa wakiwahudumia wagonjwa alisema kuwa zoezi hilo linatakiwa kuwa endelevu ili wananchi waweze kuhudumiwa kwa gharama ndogo na uhuhitaji wa wananchi ni mkubwa sana.

“Zoezi hili linatakiwa kwenda mpaka katika ngazi ya Halmashauri za Wilaya kwasababu kuna wananchi wengi ambao hawakupata fursa ya kufika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera na wana matatizo makubwa kama tulivyoona hapa.” Alisistiza Mkuu wa Mkoa Kijuu.

Naye Jovinus Rweikiza  kutoka katika Kijiji cha Kasharu Bukoba Vijiji aliyefanyiwa upasuaji wa tezidume na Madaktari Bingwa hao akiwa wodini alitoa ushuhuda jinsi alivyokuwa amehangaika katika Hospitali mbalimbali ili aweze kupata huduma na kupewa rufaa za kwenda Hospitali ya Rufaa ya Bugando lakini ilikuwa inashindikana kutokana na gharama kubwa za matibabu hayo.

Serikali ya Mkoa wa Kagera inatoa rai kwa wananchi waliokuwa wamejiandikisha na kulipa fedha zao ili kuonana na Madaktari bingwa lakini hawakufanikiwa kuonana nao kutokana na wingi wa wagonjwa na muda wao kuwa mfupi,  zoezi hilo litakapofanyika tena watapewa kipaumbele na kupewa huduma hiyo bila kulipia tena shilingi 5000 za kujiandikisha kwani tayari mafaili yao yapo.

Matangazo

  • Online Content - inception report for CSA training programme in Kagera region August 19, 2022
  • Kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru Kuhitimishwa Mkoani Kagera Oktoba 14, 2022 August 23, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Mkoa wa Kagera Wapokea Magari Matano Kusaidi Kufanikisha Zoezi la Sensa ya Watu na Makazi

    August 24, 2022
  • Mkuu wa Mkoa Chamila Akagua Miradi na Kuongea na Makarani Wa Sensa ya Watu na Makazi Kagera

    August 23, 2022
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Wanakagera Wakumbushwa Kuendelea Kuilinda Amani ya Tanzania Ili Kufikia Miaka 100 ya Uhuru

    December 08, 2021
  • Tazama zote

Video

Kijue Chuo Kipya cha Kisasa cha Ufundi Stadi VETA Mkoani Kagera Kazi Inaendelea.....
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa