• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Mmea wa Pamba Ukiwa Shambani Umestawi

Imewekwa : October 23rd, 2017

Serikali Mkoani Kagera Yaweka Mikakati Thabiti ya Kufufua Zao la Pamba Wilayani Biharamulo na Muleba

Mkoa wa Kagera waweka mikakati ya kuhakikisha kuwa zao la pamba linafufuliwa upya na kupewa kipaumbele kama zao la biashara kwa wakulima na kuhakikisha kuwa zao hilo linalimwa kwa kiwango kikubwa hasa katika Halmashauri za Wilaya za Biharamulo na Muleba zilizokuwa zinalima zao hilo hapo awali.

Katika kuhakikisha zao la pamba Mkoani Kagera linafufuliwa upya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali  Mstaafu Salum M. Kijuu aliwatembelea Wakaulima katika Wilaya za Biharamulo na Muleba na kuzindua ugawaji wa mbegu bora za pamba kwa wakulima Katika Halmashauri ya Wilaya ya Muleba kwa ajili ya msimu huu wa mwaka 2017/2018.

Mkuu wa Mkoa Kijuu  akiwa katika Wilaya ya Biharamulo Kata ya Nyamigogo Tarafa Nyarubungo na Wilayani Muleba katika Kata ya Nyakabango Tarafa ya Kimwani alikutana na wananchi na wakulima wa zao la pamba na kuwahamasisha wananchi hao kuanza tena kulipa kipaumbele zao la pamba kama zao biashara.

“Serikali ya Awamu ya Tano imejipanga kuhakikiksha kuwa zao la pamba linafufuliwa upya, aidha Serikali inaliangalia na kulipa kipaumbele zao la pamba kama zao mojawapo kuu la biashara ambalo kama likipewa kipaumbele na kuangaliwa kwa ukaribu litaweza kuinua pato la Taifa na wananchi kwa ujumla ambao ni wakulima wetu.”  Alisistiza Mhe. Kijuu.

Mkuu wa Mkoa aliwatoa wasiwasi wananchi juu ya upatikanaji wa masoko na kusema kuwa sasa Serikali imeanzisha viwanda pia na kuhakikisha kuwa viwanda vyote vya pamba vinafufuliwa ili viweze kufanya kazi na pamba kupata soko la kutosha.” Jukumu lenu ninyi wakulima mnatakiwa kulima kwanguvu sana sasa zao la Pamba.”Alisistiza Mhe. Kijuu

Mikakati ya Mkoa kuhakikisha  zao la Pamba linafufuliwa.

Mkuu wa mkoa wa Mkoa aliziagiza Halmashauri  za Wilaya za Biharamulo na Muleba kuhakikisha zinawapatia mbegu bora wakulima wa zao la pamba kwa utaratibu wa kuwakopesha mbegu hizo katika msimu huu wa 2017/2018 na kuanza kujipanga vizuri zaidi kwa msimu wa mwaka 2018/2019.

Halmashauri za Wilaya za Biharamulo Muleba na kupitia Maafisa Ushirika wahakikishe wanaimarisha vikundi vya AMCOS kwa ajili ya kuviweka tayari katika kushughulikia mchakato wa kulifufua zao la pamba.

Maafisa Kilimo, Watendaji na Wataalamu waliopo wawe na mashmba darasa au mashamba ya mfano hasa katika ngazi za Vijiji na Kata. Aidha,  Maafisa Watendaji wa Kata na Vijiji watumike kuhamasisha wakulima maeneo ambayo wataalamu wa kilimo hawapo.

Akihitimisha ziara yake aliyoifanya katika Halmashauri za Wilaya za Biharamulo na Muleba tarehe 18 hadi 19 Oktoba, 2017 Mhe.  Kijuu pia aliwakumbusha wananchi na viongozi wa ngazi zote katika Mkoa kuhakikisha kila kaya inakuwa na ekari ya zao moja la biashara hususani Pamba na ekari moja ya zao la chakula kwaajili ya kujikinga na janga la njaa lakini pia wanannchi hususani wakulima kujiingizia kipato kwa zao la biashara.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa