• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Msimu wa Kahawa Kagera Wafunguliwa Rasmi Wakulima Kulipwa Ndani ya Saa 48 Serikali Kusimamia Haki Zao

Imewekwa : June 9th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco E. Gaguti azindua rasmi msimu wa Kahawa wa mwaka 2020/2021 ikiwa ni pamoja na kutangaza bei  ya malipo ya awali shilingi 1200 kila kilo ya kahawa ya maganda kwa  Vyama Vikuu vya Ushirika vya KCU 1990 Limited,  KDCU Limited na Ngara Farmers.

Mkuu wa Mkoa Gaguti akitangaza ufunguzi wa msimu katika  Chama cha  Msingi cha Mabira Wilayani Kyerwa Juni 9, 2020 alisema kuwa jukumu kuu la Serikali ni kuhakikisha mkulima analindwa haki zake asipunjwe katika bei  pia muda wa kupata malipo yake uwe mfupi kutoka wiki moja hadi masaa 48 tangu mkulima kufikisha kahawa yake katika Chama cha Msingi.

Mkuu wa Mkoa Gaguti alitumia fursa hiyo kurudia kauli yake kuwa kama kuna mfanyabaiashara yeyote ambaye yupo tayari kununua kahawa kwa wakulima kwa bei nzuri ajitokeze na kutangaza bei yake ili akapatiwe kahawa. “Kufikia tarehe 8.06.2020 tumepokea maombi ya wafanyabiashara wanane na kati ya hao wawili tu waliwasilisha maombi kwa barua na mmoja ndiye aliomba kununua kahawa kwa shilingi 1100 tu.”  Alieleza Mkuu wa Mkoa Gaguti.

Mkuu huyo wa Mkoa pia alitoa rai kwa wakulima kuhakikisha wanatunza ubora wa kahawa yao kabla ya kuipeleka katika  Vyama vya Msingi ili kuhakikisha kahawa kutoka Mkoani Kagera inafika kwenye soko ikiwa na ubora unaotakiwa  ambapo katika msimu huu 2020/2021 zinatarajiwa kukusanywa takribani kilo milioni 60 juu ya kiasi cha msimu uliopita ambapo zilikusanywa kilo milioni 52.

Naye Mtendaji Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) Bw. Japhet Justine katika hafla hiyo ya ufunguzi wa msimu wa kahawa mwaka 2020/2021 alisema kuwa Vyama Vikuu vya Ushirika Mkoani Kagera vimekuwa viaminifu tangu mwaka 2018 benki ya TADB ilipoanza kuvipa mkopo ambapo msimu wa mwaka 2018 Benki hiyo ilitoa   bilioni 30 na zililipwa zote, msimu 2019 Benki ilitoa bilioni 23 na zote zililipwa.

“Aidha, msimu huu wa 2020/2021 tayari tumeweka shilingi  bilioni  7.7 katika akaunti za Vyama Vikuu vya KDCU Limited na KCU 1990 Limited kwaajili ya kukusanya kahawa ya wakulima na bila kuchelewesha malipo yao. Ndiyo maana baada ya kuona uaminifu wa vyama hivyo vikuu tumeamua kupunguza riba kutoka asilimia 12 na mwaka huu tunatoa mkopo kwa asilimia tisa tu (9%).” Alifafanua Bw. Japhet

Kuanzia Juni 9, 2020 wakulima wa zao la kahawa Mkoani Kagera wanahamasishwa kuanza kukusanya kahawa katika Vyama  vyao vya Msingi na fedha ya malipo ya awali ipo tayari kwaajili ya  kuwalipa.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa