• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua Pepe za Watumishi |
KAGERA REGIONAL WEBSITE

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na SerikaliI za Mitaa Mkoa wa Kagera

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Sehemu/Vitengo
      • Sehemu
        • Usimamizi Ufuatiliaji na Ukaguzi
        • Miundombinu
        • Elimu
          • Elimu ya Msingi
          • Elimu ya Sekondari
          • Elimu ya Watu Wazima
          • Elimu ya Juu
          • Michezo
          • Vijana
        • Afya
          • Afya
          • Ustawi wa Jamii
        • Utawala na Rasilimali Watu
        • Mipango na Uratibu
          • Mipango
          • Takwimu
          • Maendeleo ya Jamii
          • TASAF
        • Uchumi na Uzalishaji
          • Kilimo cha Umwagiliaji
          • Viwanda na Biashara
          • Uvuvi
          • Mifugo
          • Maliasili, Utalii na Mazingira
          • Ushirika
          • Kilimo
        • Uwekezaji Viwanda na Biashara
      • Vitengo
        • TEHAMA
        • Sheria
        • Fedha na Uhasibu
        • Ukaguzi wa Ndani
        • Ugavi
        • Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Bukoba
      • Viongozi wa Bukoba
    • Biharamulo
      • Viongozi wa Biharamulo
    • Karagwe
      • Viongozi wa Karagwe
    • Kyerwa
      • Viongozi wa Kyerwa
    • Missenyi
      • Viongozi wa Missenyi
    • Muleba
      • Viongozi wa Muleba
    • Ngara
      • Viongozi wa Ngara
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo
    • Halmashauri ya Wilaya ya Karagwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Kyerwa
    • Halmashauri ya Wilaya ya Misseny
    • Halmashauri ya Wilaya ya Muleba
    • Halmashauri ya Wilaya ya Ngara
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Fursa za Ufugaji
    • Fursa za Kilimo
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma za Ufugaji
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Taarifa
    • Fomu Mbalimbali
    • Miongozo
    • Jarida
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Picha Mbalimbali

Naibu Waziri Dk. Faustine Ndungulile Akiongea na Mzee Anayeishi Katika Kituo cha Wazee Kiilima Wilayani Bukoba Mkoani Kagera

Imewekwa : February 23rd, 2018

Naibu Waziri Ndungulile Achangisha Zaidi ya Milioni 17 Kujenga Nyumba za Watumishi Kituo cha Wazee Kiilima Mkoani Kagera

Naibu Waziri wa Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia  Wazee na Watoto Dk. Faustine Ndungulile afanikisha  kupatikana kwa zaidi ya  shilingi milioni 17 kwenye harambee ya kuchangia ujenzi wa  Nyumba ya Watumishi katika Kituo cha Wazee Kiilima Kata ya Nyakato Wilayani Bukoba Mkoani Kagera.

Katika Harambee hiyo iliyofanyika Februari 22, 2018 katika Kituo cha Wazee Kiilima Dk. Ndungulile akiwa  Mgeni Rasmi alichangisha fedha taslimu milioni 7,000,000/= na kiasi cha shilingi milioni 11 zikiwa ahadi kutoka kwa wadau mbalimbali pamoja ahadi za vifaa kama magodoro, saruji,  baiskeli za wazee na mabati.

Katika hotuba yake kwa wananchi na wadau mbalimbali waliohudhuria harambee hiyo Naibu Waziri Dk. Ndungulile aliwasisitiza wananchi kuwa na moyo wa kujitolea kuchangia kituo hicho ili watumishi wanaowatunza wazee wapate mazingira mazuri ya kuishi baada ya kufanya kazi yao ya kuwahudumia wazee hao.

“Serikali itaendelea kuwaunga  mkono wananchi kwa kuleta fedha katika kituo hiki ili kikamilike ujenzi wake na Wazee wetu  waweze kuhudumiwa na watumishi  ambao watawaza ni wapi pa kuishi au kukaa salama mara baada ya kufanya kazi yao ya kuwahudumia Wazee wetu,” Alisisitiza Dk. Ndungulile.

Kituo cha Kutunza Wazee Kiilima ni kituo cha Serikali kilichopo chini ya Wizara ya  Afya , Maendeleo ya Jamii, Jinsia  Wazee na Watoto.  Kituo Hicho kilijengwa upya na Serikali baada ya kuathiriwa na Tetemeko la Ardhi lililotokea Septemba 10, 2016 Mkoani Kagera.

Majengo yaliyojengwa upya na Serikali ni pamoja na Mabweni mawili ya Wanaume na Wanawake, Jiko, stoo ya kutunzia chakula, Sehemu ya kulia chakula, sehemu ya kupumzikia wazee,  vyoo viwili vya wanawake na wanaume. Changamoto iliyokuwa imebaki ni nyumba za watumishi ambazo kwa sasa zina hali mbaya ya uchakavu na hazistahili tena kuishi watu.

Fedha zilizopatikana zinatarajiwa kujenga nyumba mbili za watumishi (Two in One) ili kutatua changamoto ya watumishi wanaoishi na kufanya kazi ya kuwahudumia wazee ili wapate mahali salama pa kuishi na kutimiza wajibu wao kikamilifu bila kuwa na changamoto za sehemu za kuishi.

Katika Hatua nyingine Naibu Waziri Dk. Ndungulile alimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu kwa juhudi zake za kuipatia Bohari ya Dawa (MSD)  kiwanja cha kujenga Bohari ya dawa katika Manispaa ya Bukoba na Mkoani Kagera ili kurahisisha upatikanaji wa dawa zote hapa Kagera.

Pia Dk. Ndungulile alimuomba Mkuu wa Mkoa kuhamasisha wananchi kuitikia wito wa kuwapeleka watoto wa kike miaka 4 hadi 9 kwenda kwenye vituo vitakavyokuwa vimepangwa kupata chanjo ya kansa ya shingo na uzazi kwani imeonekana kuwa kuna ongezeko kubwa la Kansa ya Shingo na uzazi katika mkoa wa Kagera.

Akimshukuru Naibu Waziri kwa kuamua kufanya ziara ya kukagua shughuli za afya Mkoani Kagera Mkuu wa Mkoa Kijuu aliomba Wizara ya Afya kuangalia upya tatizo la ugonjwa wa Malaria katika Mkoa wa Kagera kwani pamoja na juhudi zote zinazofanyika laikini kiwango cha ugonjwa huo kinazidi kupanda ambapo Naibu Waziri Dk. Ndungulile alisema tayari Wizara imeliona hilo na linafanyiwa kazi.

Naibu Waziri Dk. Ndungulile akiwa Mkoani hapa katika ziara yake ya siku mbili alivitembelea pia vituo vya Afya Kabyaile Wilayani Missenyi, Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera, Kituo cha Afya Kaigara na Kituo cha Afya Kimeya Wilayani Muleba ili kukagua huduma za Afya zinavyotolewa kwa wananchi na kuongea na watumishi katika maeneo hayo.

Matangazo

  • No records found
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Kagera Yaridhia Jimbo la Uchaguzi la Nkenge Kuitwa Jimbo la Uchaguzi Missenyi

    March 17, 2025
  • Mkuu wa Mkoa wa Mwassa Awashukuru Wabunge Kupitisha Fedha za Miradi ya Mapinduzi ya Kiuchumi Kagera

    March 14, 2025
  • Viongozi wa Dini Wahimizwa Kudumisha Mshikamano Ili Kukuza Uchumi wa Mkoa wa Kagera – RC Mwassa

    March 14, 2025
  • TULIPE KODI-RC MWASSA

    October 07, 2023
  • Tazama zote

Video

KAGERA REGION DOCUMENTARY
Video zaidi

Kurasa za Karibu

  • Taratibu za biashara ya ndani
  • Barabara Kuu na ndogo za Mkoa
  • Vituo vya Redio Katika Mkoa wa Kagera
  • Wakuu wa Mkoa wa Kagera Tangu Uhuru Mwaka 1961
  • Matokeo ya Darasa la VII 2018, Wanafunzi 10 Bora, Shule 10 Bora, Watakaojiunga Kidato cha I, 2019
  • Kitabu cha Mwongozo wa Uwekezaji Kagera 2019
  • FOMU YA USAJILI WA WAFANYABIASAHARA NA WADAU WA MKOA WA KAGERA, ZIARA YA KUTEMBELEA NCHI ZA AFRIKA MASHARIKI NA KATI KWA LENGO LA KUTAFUTA FURSA ZA BIASHARA NA UWEKEZAJI NOVEMBER, 2019.

Tovuti Mashuhuri

  • Ikulu
  • Utumishi
  • TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Takwimu Huria

Wafuatiliaji Kimataifa

world map hits counter

Kaunta ya Wageni

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera

    Anwani: S.L.P 299 BUKOBA

    Simu ya Mezani: 255 28 2220215/17

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ras.kagera@tamisemi.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu
    • Hakimiliki

Haki zote zimehifadhiwa